Pre GE2025 Profesa Lipumba achaguliwa tena mwenyekiti CUF, aweka historia

Pre GE2025 Profesa Lipumba achaguliwa tena mwenyekiti CUF, aweka historia

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
2,060
Reaction score
5,648
Matumaini na imani ya wanachama wa Chama cha Wananchi (CUF), yamebaki vile vile kama ilivyokuwa miaka 25 iliyopita, baada ya kumchagua tena Profesa Ibrahim Lipumba kuwa mwenyekiti wao taifa.
IMG_1788.jpeg

Profesa Lipumba anaukwaa wadhifa huo, baada ya kupata kura 216 katika uchaguzi wa ndani wa chama hicho, akiwashinda wenzake saba waliokuwa wakichuana katika nafasi hiyo.

Soma, Pia: Profesa Lipumba ajitosa kwenye kinyang’anyiro cha Uenyekiti CUF

Hii inampa nafasi mwanasiasa huyo aliyebobea katika masuala ya uchumi ya kukiongoza chama hicho kwa miaka mitano ijayo na hivyo kuweka historia ya kuwa Mwenyekiti wa chama cha siasa kwa miaka 30 nchini.

Katika uchaguzi huo, uliofanyika jana Jumatano, Desemba 18, 2024, Profesa Lipumba ameshinda kwa kura 216 kati ya kura 592 halali zilizopigwa.

Kura zote zilizopigwa zilikuwa ni 596, kati ya hizo kura halali 592 na kura nne (4) ziliharibika

Katika uchaguzi huo uliokuwa na wagombea tisa (9) wagombea wengine walikuwa ni Ali Juma Khamis ambaye alijitoa 'dakika za mwisho', mgombea wa pili alikuwa ni Athman Kanali aliyepata kura tano (5), Hamadi Hamadi alipata kura 181, Juma Shaban alipata kura sita (6), Maftaha Abdallah Nachuma alipata kura 102, Wilfred Lwakatare amepata kura 78, Ngaitile Siwale amepata kura mbili (2) na Chifu Lutalosa Yemba amepata kura mbili (2)
 
Haya, subirini na mbowe achaguliwe tena kuwa mwenyekiti wa chadema. Cuf yenyewe imesinyaa haina mvuto kama zama zile za maalim seif. Cuf wangechagua mwenyekiti mwingine mwenye maono mapya
 
Nina hakika hata hao wanachama hawajijui kuwa ni wanachama. CUF ishajifia kitambo.

Lipumba ameishia kuwa kama John Cheyo na wote wataishia kuwa kama Mrema, kudata.
 
Matumaini na imani ya wanachama wa Chama cha Wananchi (CUF), yamebaki vile vile kama ilivyokuwa miaka 25 iliyopita, baada ya kumchagua tena Profesa Ibrahim Lipumba kuwa mwenyekiti wao taifa.
View attachment 3180014
Profesa Lipumba anaukwaa wadhifa huo, baada ya kupata kura 216 katika uchaguzi wa ndani wa chama hicho, akiwashinda wenzake saba waliokuwa wakichuana katika nafasi hiyo.

Soma, Pia: Profesa Lipumba ajitosa kwenye kinyang’anyiro cha Uenyekiti CUF

Hii inampa nafasi mwanasiasa huyo aliyebobea katika masuala ya uchumi ya kukiongoza chama hicho kwa miaka mitano ijayo na hivyo kuweka historia ya kuwa Mwenyekiti wa chama cha siasa kwa miaka 30 nchini.

Katika uchaguzi huo, uliofanyika jana Jumatano, Desemba 18, 2024, Profesa Lipumba ameshinda kwa kura 216 kati ya kura 592 halali zilizopigwa.
Alishaweka historia kwa kujiuzulu na baadae akarudi madarakani kinyemela. Mtaani kugumu sana.
 
Kulikuwa na uchaguzi na huku
Aligombea na nani katika Chama chake
 
Matumaini na imani ya wanachama wa Chama cha Wananchi (CUF), yamebaki vile vile kama ilivyokuwa miaka 25 iliyopita, baada ya kumchagua tena Profesa Ibrahim Lipumba kuwa mwenyekiti wao taifa.
View attachment 3180014
Profesa Lipumba anaukwaa wadhifa huo, baada ya kupata kura 216 katika uchaguzi wa ndani wa chama hicho, akiwashinda wenzake saba waliokuwa wakichuana katika nafasi hiyo.

Soma, Pia: Profesa Lipumba ajitosa kwenye kinyang’anyiro cha Uenyekiti CUF

Hii inampa nafasi mwanasiasa huyo aliyebobea katika masuala ya uchumi ya kukiongoza chama hicho kwa miaka mitano ijayo na hivyo kuweka historia ya kuwa Mwenyekiti wa chama cha siasa kwa miaka 30 nchini.

Katika uchaguzi huo, uliofanyika jana Jumatano, Desemba 18, 2024, Profesa Lipumba ameshinda kwa kura 216 kati ya kura 592 halali zilizopigwa.
Mbona uchaguzi wao haujasikika??? Au ni habari ya zamani
 
Matumaini na imani ya wanachama wa Chama cha Wananchi (CUF), yamebaki vile vile kama ilivyokuwa miaka 25 iliyopita, baada ya kumchagua tena Profesa Ibrahim Lipumba kuwa mwenyekiti wao taifa.
View attachment 3180014
Profesa Lipumba anaukwaa wadhifa huo, baada ya kupata kura 216 katika uchaguzi wa ndani wa chama hicho, akiwashinda wenzake saba waliokuwa wakichuana katika nafasi hiyo.

Soma, Pia: Profesa Lipumba ajitosa kwenye kinyang’anyiro cha Uenyekiti CUF

Hii inampa nafasi mwanasiasa huyo aliyebobea katika masuala ya uchumi ya kukiongoza chama hicho kwa miaka mitano ijayo na hivyo kuweka historia ya kuwa Mwenyekiti wa chama cha siasa kwa miaka 30 nchini.

Katika uchaguzi huo, uliofanyika jana Jumatano, Desemba 18, 2024, Profesa Lipumba ameshinda kwa kura 216 kati ya kura 592 halali zilizopigwa.
CUF hakuna chama pale
 
Nina hakika hata hao wanachama hawajijui kuwa ni wanachama. CUF ishajifia kitambo.

Lipumba ameishia kuwa kama John Cheyo na wote wataishia kuwa kama Mrema, kudata.
Hata Mbowe?
 
Back
Top Bottom