Profesa Mohamed Bakari: Kikosi Kazi cha Rais Samia hakina uhalali wa Kisheria na Kikatiba

Profesa Mohamed Bakari: Kikosi Kazi cha Rais Samia hakina uhalali wa Kisheria na Kikatiba

BARD AI

JF-Expert Member
Joined
Jul 24, 2018
Posts
3,591
Reaction score
8,826
Profesa wa Sayansi ya Siasa wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Mohamed Bakari amekitahadharisha Chama Cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA kuwa makini na kikosi kazi, kwani kinaweza kuwa njia ya kuchelewesha maridhiano.

“CHADEMA wako sahihi kususia kikosi kazi kwa sababu hakina uhalali wa kisheria na kikatiba kama vyombo vingine, lakini kama tunataka tu kufanya mazungumzo basi ni jambo la heri.

“Ni njia fulani ya kufikia maridhiano, kwa hiyo kama kuna jambo zuri tutaliona. Lakini kikosi kazi kisije kikawa ni mkakati wa kuchelewesha hayo maridhiano yenyewe,” alisema.

Kauli ya Profesa Bakari imeungwa mkono na mchambuzi wa siasa, Bubelwa Kaiza aliyesema, “kikosi ni jitihada binafsi ya Rais Samia, kukisubiri kikosi kazi ni sawa na kukubaliana na Rais kuongoza nchi kwa maoni yake binafsi.

“Kwa kuwa CHADEMA hawako kwenye kikosi kazi, waendelee na kazi zao kwa kuwa zinatambuliwa na sheria na Katiba,” alisema.
 
Mungu ni mwema huu ndo muda sahihi sasa kutapisha watu tozo ktk mafao yangu kwani inaumiza sana
 
Hata kimantiki pia hakina maana.

Kilishafanya kazi kwa kujipendekeza kumwambia Rais Katiba Mpya haina umuhimu.

Baadae, CC ya CCM ilipokutana ikaamua tofauti, kwamba Katiba Mpya ni muhimu, CCM ikaamua mchakato uanze.

Hiki kikosi kazi ni kigenge tu cha wapiga dili mjini.
 
Profesa yupo sahihi sana.

Ili Tume ya Warioba ianze kukusanya maoni, mswada ulipelekwa Bungeni, na shetia ilitungwa.

Hii kamati iliyopachikwa jina la kamati ya kukusanya maoni kuhusiana na katiba, ni usanii tupu. Imetafutwa mbinu ya wateule kupata njia ya kutafuna tozo.

Wananchi tumekaa kimya na kuukubali huu ujinga wa kuwa na vikamati visivyo na vichwa wala miguu vinavyokula pesa yetu bila ya tija yoyote.

Suala la kukusanya maoni ya wananchi kuhusiana na katiba, Tume ya kisheria ya Waruoba ilimaliza kila kitu. Wanasiasa wanatufanyia usanii, nasi tunaona ji sawa.

Katiba ya Waruoba ndiyokatiba ya Wananchi wa Tanzania, mengine yote ni upuuzi mtupu.
 
Ninaona hii ni janja janja na kupoteza muda. Yaani has Jamaa naona wamezidiwa Sasa wanabuni mambo ya kuwachanganya watu na kupoteza muda watu wasahau upatioanaji was katiba mpya.

Upinzani jipangeni tupo nyuma yenu hivi vituko vyao vya kitunga achaneni navyo.

Tafuteni matukio ambayo mna ushahodi was kutosha ambayo yanaweza kuunganosha watanzania tukutane mahakamani.

Hayo mtukio yatokane na matenda ya serikali na chama chao cha CCM na kuendana na katiba iliyopo, wanavyoendesha nchi kinyume na katiba. Tafuteni mawakili wa kutosha.

Hizi familia zinazojisikia za kifalme zitatutesa Sana. Wao wabaki na jeshi lao la Polisi sisi tulindane wenyewe.
 
Hii ni sehemu nyingine ya matumizi yasiyo na tija ya pesa za walipa kodi, hapa nimetoka kupata meseji ya kukatwa tozo ya shilingi 4000/= kwenye akaunti yangu ya Equity ambayo kimsingi hakuna huduma yoyote niliyopewa hadi kuhalalisha kukata hiyo pesa. Tozo inayoenda kununua mabasi, viieite na kulipa wajumbe wa kikosi kazi cha mchongo...​
 
Profesa wa Sayansi ya Siasa wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Mohamed Bakari amekitahadharisha Chama Cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA kuwa makini na kikosi kazi, kwani kinaweza kuwa njia ya kuchelewesha maridhiano.

“CHADEMA wako sahihi kususia kikosi kazi kwa sababu hakina uhalali wa kisheria na kikatiba kama vyombo vingine, lakini kama tunataka tu kufanya mazungumzo basi ni jambo la heri.

“Ni njia fulani ya kufikia maridhiano, kwa hiyo kama kuna jambo zuri tutaliona. Lakini kikosi kazi kisije kikawa ni mkakati wa kuchelewesha hayo maridhiano yenyewe,” alisema.

Kauli ya Profesa Bakari imeungwa mkono na mchambuzi wa siasa, Bubelwa Kaiza aliyesema, “kikosi ni jitihada binafsi ya Rais Samia, kukisubiri kikosi kazi ni sawa na kukubaliana na Rais kuongoza nchi kwa maoni yake binafsi.

“Kwa kuwa CHADEMA hawako kwenye kikosi kazi, waendelee na kazi zao kwa kuwa zinatambuliwa na sheria na Katiba,” alisema.
Kikosi kazi 😅😅😅
 
Tozo, hela iliyopatikana isivyo halali, hutumika kwenye vikosi kazi visivyo halali na baadhi yetu Watanzania tunavyopenda visivyo na uhalali, hapo kikosi kazi cha Mkandala kimepiga kituo.
😅😅😅
 
Back
Top Bottom