TANZIA Profesa Mwandosya afiwa baba yake mdogo kwa ‘changamoto za upumuaji’

TANZIA Profesa Mwandosya afiwa baba yake mdogo kwa ‘changamoto za upumuaji’

Cannabis

JF-Expert Member
Joined
Jan 20, 2014
Posts
11,557
Reaction score
33,535
2692497_1613389145650.jpg

Waziri wa zamani katika serikali ya awamu ya nne, Profesa Mark Mwandosya ametangaza kifo cha baba yake mdogo, Agen Mwandosya kilichotokana na kile alichokiita kuwa ni “changamoto ya kupumua”.

Profesa Mwandosya ametoa tangazo hilo leo Februari 15 katika ukurasa wake wa Twitter huku akisema itakuwa pole na faraja kwao kama tangazo hilo litasaidia kuokoa maisha ya watu wengine.

Ameandika: “Nasikitika kuwatangazia kifo cha baba yangu mdogo, Agen Mwandosya, kilichotokea alfajiri ya leo baada kupata ‘changamoto ya kupumua’, kwa jina jingine Corona au Covid 19.

“Kama tangazo hili litasaidia kuokoa maisha ya Mtanzania hata mmoja tu, itakuwa pole tosha na faraja kwetu.”

Tangazo hilo la Profesa Mwandosya ni moja kati ya matangazo mengi ya vifo vinavyosababishwa na changamoto za upumuaji hapa nchini unaohusishwa na ugonjwa wa corona.

Baadhi ya wananchi wamempa pole katika ukurasa wake huku wakihimiza tahadhari zaidi kuchukuliwa dhidi ya virusi vya corona.

Mohammed Abbas ameandika: “Pole sana. Hali inasikitisha sana, nawajua wengi waliofariki katika miezi hii iliyopita, na kama nawajua wengi waliofariki mjini, ni dhahiri kwamba hali ni mbaya sana, vijijini ndo hatutajua kabisa.”

Chanzo: Mwananchi
 
Hapa suluhisho ni kupata chanjo vinginevyo tutamaliza wazee. Hapa nilipo tripu za kwenda kuzika zimekuwa nyingi sana.
 
Matangazo ya vifo kamwe hayawezi kuondoa korona, bali tunapaswa kufuata maelekezo ya wizara ya afya tujikinge hilo ndilo jambo la msingi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
cheti cha kifo ndivyo kinavyosomeka? kuwa kafa kwa corona? tuwekrwe ushahidi wa picha ya hicho cheti
 
Utadhani tunaishi sayari tofauti. Hivi wakisema ni Corona ipo nchini wataharibikiwa na nini. Tunamshukuru JPM kwa kufukuza Corona nchini.
 
Apumzike kwa amani.

Wenyewe wanasema covid19 hakuna Tanzania wala hawana nia ya kuokoa maisha hata ya watu wote.

Watahalalisha ilikuwa uzee. Laana kwao.

Pole kwao familia hiyo katika kipindi hiki kigumu.

Hata sisi wengine ni suala la muda tu.
 
Mwandosya huwa anaandika kwa misemo ya kivulana sana, vijembe sijui!!
 
Back
Top Bottom