Profesa Tibaijuka: Trump kusitisha misaada ARVs zitaadimika Afrika. African Union iitishe kikao maalum kuweka mkakati

Profesa Tibaijuka: Trump kusitisha misaada ARVs zitaadimika Afrika. African Union iitishe kikao maalum kuweka mkakati

Daa, kama ni kweli basi Kuna baadhi ya Jf members hawataumaliza huu mwaka 2025
 
Dunia tunayoishi ina mambo Kweli Kweli

Vijana badala ya kusikitika Wao ndio kwanza wanampongeza Rais Trump Kwa kuzuia dawa za kufubaza virus Vya ukimwi zisiletwe Kwa msaada

Nimeshangaa sana 🐼
saivi watu wanachekacheka kama masihara flani ivi ila nkuhakikishie vilio vitakuja soon. mambo yatakuwa wazi muda uo.

maajaabu yatakuwa mengi sana. kuna watakaoshangaa kumbe hata wazazi wao au ndugu zao wa karibu kabisa kumbe nao wamo.

tatizo humu wengi wamezaliwa wakati dawa tayari zipo hawaijui ile JULIANA na mambo yake. ngoja tufike apo kwenye msururu wa matangazo ya tanzia yasiyoisha kila leo.
 
Mbunge wa zamani wa Muleba, Prof Tibaijuka amesema kitendo cha Rais Trump wa US kusimamisha msaada ya kimataifa kitaleta Kiama Tanzania na Afrika

Pia soma > Trump asimamisha misaada kwa nchi nyingine kwa siku 90 ili kupitiwa upya. Tanzania nayo kuathirika

Trump amezuia misaada ya sekta za afya nk Ili Kufanya ukaguzi kama misasda hiyo inatumika kwa usahihi au fedha zinaishia mifukoni mwa eahuni wachache

Ahsanteni sana

---
Kupitia ukurasa wake wa X (zamani Twitter), Prof. Tibaijuka amesema “Upatikanaji wa madawa ya kuongeza kinga za mwili ARVs utaathirika, ninashauri Wizara ya Afya kuufahamisha umma wa Watanzania je ni hatua gani za haraka zinachukuliwa kutathmini jambo hili na kuchukua hatua stahiki?, ikibidi African Union waitishe kikao maalum kuangalia suala hili na kuweka mkakati wa pamoja, Waathirika wa gonjwa hili la UKIMWI ni Waafrika na ugonjwa haujulikani ulitoka wapi?, tujitetee”

“Aidha juhudi za kuthibiti maambukizi ya virusi vya UKIMWI ziwekewe nguvu mpya, upatikanaji wa ARVs utakuwa mgumu na kununua ARVs kibiashara ni jambo litakalohitaji bajeti kubwa na uwezo wa taifa kwa ujumla ni mdogo na jambo limekuwa la ghafla, Waathirika wengi hawana uwezo kununua madawa hayo wenyewe maisha yao yote”

“Afya zao zikidhoofika itatumika gharama kubwa kuwauguza hivo kusababisha umaskini na vifo, pia bila ARVs maambukizi yatashika kasi mpya, tuwe macho”
Aisee
 
Mbunge wa zamani wa Muleba, Prof Tibaijuka amesema kitendo cha Rais Trump wa US kusimamisha msaada ya kimataifa kitaleta Kiama Tanzania na Afrika

Pia soma > Trump asimamisha misaada kwa nchi nyingine kwa siku 90 ili kupitiwa upya. Tanzania nayo kuathirika

Trump amezuia misaada ya sekta za afya nk Ili Kufanya ukaguzi kama misasda hiyo inatumika kwa usahihi au fedha zinaishia mifukoni mwa eahuni wachache

Ahsanteni sana

---
Kupitia ukurasa wake wa X (zamani Twitter), Prof. Tibaijuka amesema “Upatikanaji wa madawa ya kuongeza kinga za mwili ARVs utaathirika, ninashauri Wizara ya Afya kuufahamisha umma wa Watanzania je ni hatua gani za haraka zinachukuliwa kutathmini jambo hili na kuchukua hatua stahiki?, ikibidi African Union waitishe kikao maalum kuangalia suala hili na kuweka mkakati wa pamoja, Waathirika wa gonjwa hili la UKIMWI ni Waafrika na ugonjwa haujulikani ulitoka wapi?, tujitetee”

“Aidha juhudi za kuthibiti maambukizi ya virusi vya UKIMWI ziwekewe nguvu mpya, upatikanaji wa ARVs utakuwa mgumu na kununua ARVs kibiashara ni jambo litakalohitaji bajeti kubwa na uwezo wa taifa kwa ujumla ni mdogo na jambo limekuwa la ghafla, Waathirika wengi hawana uwezo kununua madawa hayo wenyewe maisha yao yote”

“Afya zao zikidhoofika itatumika gharama kubwa kuwauguza hivo kusababisha umaskini na vifo, pia bila ARVs maambukizi yatashika kasi mpya, tuwe macho”
Bajeti ya African Union huenda inachangiwa na hao hao watoa ARVs
 
Trump yupo sahihi, kila nchi ianze kujitambua na kuanza kujitegemea wao wenyewe Sasa, wasiendelee kuitegemea Marekani. Safi Sana hii, hii itawalazimisha Watu wengine waliopo duniani kote hususani Watu weusi kuanza kujitambua na kupata akili nzuri ya kuweza kujitegemea. Hatua hizi za Utawala wa Trump ni Kama 'Black Consciousness Campaign' kwa Watu weusi wote kabisa hapa duniani ili waache kutegemea Misaada kutoka Marekani. Ni mwanzo mzuri.

Kwanza Watawala wengi sana wa kutoka katika nchi za Afrika pamoja na Vibaraka wao daima wamekuwa wakiwasema vibaya sana Wazungu hususani Watu wa Marekani kuwa ni Mabeberu na Wapenda Ushoga, Sasa kwa hatua hizi za Utawala wa Trump zitasaidia Sana kukomeshwa kwa hiyo Misaada inayodaiwa kuwa eti 'imetoka na Mabeberu na Wapenda Ushoga.'
Watu wa Afrika (Watu weusi) hususani waTanzania sasa wanatakiwa waelekeze maombi yao ya Misaada kwenda kwa Marafiki zao wa nchi za Mashariki ambao wanawaona kuwa siyo Mabeberu na Wasiopenda Ushoga, nchi za China, Urusi, Korea ya Kaskazini, Belarus, n.k ili waweze kupatiwa Misaada kutoka huko.
Je Yeye Trump Na America Yake Wataacha Kuzinyonya Nchi Za Africa?Mi Nachojua Hiyo Misaafa Ni Sawa Na Kumchimbia Mtu Msingi Au Shimo Alafu Mshahara Ni Kukupa Chakula.
 
Back
Top Bottom