Professor Issa Gulam Hussein Shivji, Nje bunge la katiba!! Watanzania tumelogwa au.......?

Professor Issa Gulam Hussein Shivji, Nje bunge la katiba!! Watanzania tumelogwa au.......?

Katika mahali Raisi alipoonyesha kuwa yeye ayupo series na Taifa ni kumwacha huyu Gwiji. Haiingii akilini kumtupa nje mtu kama huyo na kuwaingiza watu kama kina kingunge. Yani inatia hasira sana na.... wacha tu niishie hapa.
 
Kikwete ni mtu muungwana mno. Hongera sana kwa kazi kubwa na ya kutukuka uliyofanya

Yani kati ya was...en..ge wewe ni raisi wao. huwezi sifia makitu kama hayo kama wewe sio mse..
 
Huyo ni Gwiji la sayansi ya sheria hususani katiba. Mchango wake ni mkubwa sana kwa Taifa hasa kipindi hiki katika kuyaframe mawazo ya Watanzania na kujadiliana jisi ya kuupata muundo wa kuandika katiba mpya.

Mkuu acha ushabiki kwenye mambo ya msingi wewe.

Mkuu tatizo la watanzania wengi ni kuwa wamelishwa sumu na ccm.mambo ya msingi ya katiba Wapo wanaleta ushabiki wa kisiasa.

Poor Tanzanians. Mungu atuondolee sumu hii .
 
Kwanza nakushukuru sana mleta hii threads,ila hata mimi naona kama wapenda mageuzi ya kweli tumechezewa shere,inabidi CHADEMA waliangalie hili kwa umakini na walitolee TAMKO,

Kwa faida ya Watanzania wote, nadhan tungeenda mbali zaidi kwa kutaja hata nafasi wanazoshika hao wanachama hai wa CCM,walijichomeka/waliochomekwa (hasa wale wanaoshika nyadhifa kubwa ndani ya chama kipindi hiki) kwenye makundi mengine nje ya lile la Vyama vyenye usajili wa kudumu,,

Mimi naanza kwa kutaja nafasi zao wanazoshika sasa katika chama cha CCM

Mzee Hassan Mohamed Wakasuvi-M/kiti CCM Mkoa wa Tabora
Bi Jesca Msambatavangu-M/kiti wa CCM-Mkoa wa Iringa
Paulo Makonda -Katibu wa UVCCM-Taifa,Uhamasishaji na Chipukizi

Mtabibu Zainabu Amir Gama-huyu alikuwa mbunge wa Jimbo la Kibaha mjini kipitia CCM,bunge lililopita.

Pia ni kweli mtu kama Kajubi Mukajangwa wa Baraza la Habari ana malengo sawa na watu vyama vya siasa?...

Hapa kuna USANII wa KUTISHA!!
 
hata mimi nimeshangaa sana yeye kumuacha Prof. Shivji
 
Sasa nimejua ngoma hii ni ya kuzuga tu,naona itaanza upya baada ya 2015
 
Wengi tulidhania kwamba mamlaka ya uteuzi ilipitiwa kwa kumsahau Prof Shivji kwenye tume ya Warioba, lakini kwa vile kosa hilo limefanywa tena, basi hakuna shaka kwamba limekusudiwa. Lakini pamoja na hayo, tupo wengi sana ambao tunaelimika vilivyo kwa kumsoma gwiji huyu anayetambulika kimataifa katika masuala ya constitutional Law, na hata pale Cambridge University alipochukua PhD yake miakza zaidi ya 30 iliyopita, Prof Shivji bado ni gumzo.

Long Live Prof, mchango wako unatambulika sana katika taifa na wengi tunaufanyia kazi, ipo siku utakuja kuona matokeo yake.
 
Mkuu tatizo la watanzania wengi ni kuwa wamelishwa sumu na ccm.mambo ya msingi ya katiba Wapo wanaleta ushabiki wa kisiasa.

Poor Tanzanians. Mungu atuondolee sumu hii .

Inavyoonekana mchawi wetu kafa.yani inasikitisha
 
Hiyo list ni ya kupooza machungu ya kuuliwa baba zao,ndiyo ikulu imeamua iwafute jasho kwa kuwapa ubunge wa muda Kolimba,Mvungi etc

Heshima kwenu wana jf,
Naomba mawazo yenu katika uteuzi wa wabunge wa bunge la katiba uliofanywa jana na Mkuu wa Nchi.

Katika majina 84 toka taasisi za Elimu Tanzania Bara Rahisi aliteuwa majina 13 kama sheria inavyomtaka afanye. Ila katika hayo majina 13 ambayo ni:-
Dr. Suzan Kolimba
Dr. Natuwa Mvungi

Dr. Domitila Bashemera
Dr. Francis Micael



MKuu unamanisha hawa au?
 
Uteuzi huu ni ili mradi liende tu. Inakatisha tamaa
 
Ameachwa nje ili asaidie akiwa nje kama Critic

Na pia atafanya kazi ya kuelimisha wananchi kwenye vyombo vya habari.
 
Watanzania mmeshasahau nini kiliwatokea kina Dr Sengondo Mvungi, Prof. Jwan Mwaikusa etc mnataka na Shivji nae yamtokee. muacheni Prof.shivji apumzike.
 
Huyo ni Gwiji la sayansi ya sheria hususani katiba. Mchango wake ni mkubwa sana kwa Taifa hasa kipindi hiki katika kuyaframe mawazo ya Watanzania na kujadiliana jisi ya kuupata muundo wa kuandika katiba mpya.

Mkuu acha ushabiki kwenye mambo ya msingi wewe.

We ndo unaandika kwa ushabiki. Huyo gwiji Prof.Shivji si alishiriki kwenye katiba hii tunayotaka kuizika kwa mafungufu kibao....
Acha na wengine watupe mawazo yao kwani mwenye uamzi keshaamua.

Wewe huwez kumchagulia Rais/serikali watu wa kushiriki.
 
Wala mimi sishangai Kinachoendea ni sanaa tu. Rais ,wapinzani wanajua Katiba mpya ni mpaka 2016 .subiri uone La muhimu tutoe haki ili tunda la amaNI lizidi sana
 
Back
Top Bottom