Pre GE2025 Professor Jay: Watanzania kumshambulia AY kwa kuonekana kwenye majukwaa ya CCM sio sawa. Wasanii wengi pia wapo CHADEMA

Pre GE2025 Professor Jay: Watanzania kumshambulia AY kwa kuonekana kwenye majukwaa ya CCM sio sawa. Wasanii wengi pia wapo CHADEMA

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Mindyou

JF-Expert Member
Joined
Sep 2, 2024
Posts
1,869
Reaction score
4,877
Wakuu


Msanii Profesa Jay amesema baadhi ya Watu wanaowashambulia Wasanii kama Ay na wengine kutokana na kupanda kwenye majukaa ya Vyama vya siasa, hawawatendei haki kwasababu Tanzania ni nchi ya Kidemokrasia.

Kwenye mahojiano maalum na Mtangazaji Millard Ayo, Profesa Jay ameeleza yafuatayo

“Hata Wasanii wenyewe pia wana upande wao na wanaruhusiwa kuwa na upande, Mtu wa CCM au CHADEMA popote anapoweza kuwa, ACT, akawa CUF, akawa NLD, akawa CHAUMMA na vitu vingine kama hivyo kwahiyo ni haki yake ya kimsingi, ameamua kui-support CCM ai-support CCM lakini sisi wengine tumeamua kubaki na CHADEMA kwa sababu ni haki yetu ya kimsingi pia”

“Utaona hata mimi nimesaidiwa sana na Watu wa CCM ingawa mimi niko CHADEMA kwa sababu ubinaadamu unakuwa upo mwanzo kwanza kabla ya vitu vingine kuendelea, cha kwanza ni utu"

"kwahiyo Watu kumshambulia AY kwa kuonekana kwenye majukwaa ya CCM sidhani kama ni haki, hawamtendei haki kwakweli kwa sababu ni haki yake ya kikatiba kuchagua upande anaoona yeye unafaa, hata sisi kuna Wasanii wengi wapo upande wa CHADEMA”

“Mimi pamoja na kwamba nipo CHADEMA lakini pia nilisaidiwa na Watu wa CCM wakiongozwa na Mwenyekiti wao Mama Samia Suluhu Hassan yeye alinisimamia matibabu yangu mwanzo mpaka mwisho lakini pia Makamu wa Rais Dr"

"Mpango alituchangia, Waziri Mkuu Majaliwa pamoja na kuja kuniona alituchangia milioni 10, Naibu Waziri Mkuu Dr. Biteko pia alituchangia milioni 10, tulienda Bungeni Dr. Tulia aliongoza Wabunge wakatuchangia milioni 5, lakini pia Katibu Mwenezi wa wakati ule Paul Makonda alituchangia milioni 20, Waziri wa Maji Aweso pia alituchangia milioni 10 yeye na Wizara ya maji”


 
Tatizo AY alijiweka daraja la juu sana kisha akasababisha masimango makali kwa wadada wa kibongo alipoenda kuoa mrwanda wakaenda zao marekani kuishi. Kaishiwa na kukimbiwa na mke ndo kakumbuka bongo ni nyumbani,na karudi kuwa chawa
 
Hapa Prof kapuyanga. Kuna vyama vya kushabikia lakini si CCM.

Wasanii wengi wamekimbilia CCM kwa Sababu ya Njaa. Tatizo linakuwa msanii kioo cha jamii anakua na uchawa mwingi kiasi cha kuwafanya waungwana wabaki mdomo wazi.

Mtu mzima mwenye akili timamu Kutembea na mabango ya ccm 🚮
 
Tatizo AY alijiweka daraja la juu sana kisha akasababisha masimango makali kwa wadada wa kibongo alipoenda kuoa mrwanda wakaenda zao marekani kuishi. Kaishiwa na kukimbiwa na mke ndo kakumbuka bongo ni nyumbani,na karudi kuwa chawa
Hahahaha ial wee dada umeongea kimipasho sna
 
Prof Jay yuko sahihi.
Kila mmoja anapambana kuunga mkono ule upande unaowezesha mkono kwenda kinywani
Ila AY siyo chawa ni chawa Pro max. Kubebeshwa libendera la mama na kuzunguka huko mikoani ni wehu. Mbaya zaidi alikuwa na fursa ya kubadili maisha yake pale alipokuwa na green card. Kurudi bongo lazima achekwe na mimi nasema achekwe tu. Haiwezekani leo eti ndiyo anakumbuka uchawa baada ya mambo kubuma.

Kwako dayaspora mstaafu uchwara.
 
AY na FA ni twins kwaiyo pacha wake kampa mchongo wa uchawa nae aje kulamba kitengo
 
Hana mvuto tena
...na usanii wake wa majukwaani, kama wasanii wengine.
jamiiforums1267461471_387x387-jpg.2572374

...alipenda kufokafoka(rap?) majukwaani
 
Watanzania wengi hawajui wanasiasa wapo kwa ajili ya kujitafutia kipato na si kuhangaika na mambo yanayowahusu wangekuwa na kiasi sana namna wanavyoongea na hasa wanamageuzi..

Tumewaona wengi wakishiba wangeuza maneno na kumshambulia mtu sio sawa hata kidogo..

Sasa Lema na Gambo wana tofauti gani?

Duniani siasa ni kazi sio maneno matupu.
 
Tatizo AY alijiweka daraja la juu sana kisha akasababisha masimango makali kwa wadada wa kibongo alipoenda kuoa mrwanda wakaenda zao marekani kuishi. Kaishiwa na kukimbiwa na mke ndo kakumbuka bongo ni nyumbani,na karudi kuwa chawa
Vijana mtaani wanakuambia Ay ana pesa kuliko Diamond!!!!!
Tz ina maajabu
 
Wakuu


Msanii Profesa Jay amesema baadhi ya Watu wanaowashambulia Wasanii kama Ay na wengine kutokana na kupanda kwenye majukaa ya Vyama vya siasa, hawawatendei haki kwasababu Tanzania ni nchi ya Kidemokrasia.

Kwenye mahojiano maalum na Mtangazaji Millard Ayo, Profesa Jay ameeleza yafuatayo

“Hata Wasanii wenyewe pia wana upande wao na wanaruhusiwa kuwa na upande, Mtu wa CCM au CHADEMA popote anapoweza kuwa, ACT, akawa CUF, akawa NLD, akawa CHAUMMA na vitu vingine kama hivyo kwahiyo ni haki yake ya kimsingi, ameamua kui-support CCM ai-support CCM lakini sisi wengine tumeamua kubaki na CHADEMA kwa sababu ni haki yetu ya kimsingi pia”

“Utaona hata mimi nimesaidiwa sana na Watu wa CCM ingawa mimi niko CHADEMA kwa sababu ubinaadamu unakuwa upo mwanzo kwanza kabla ya vitu vingine kuendelea, cha kwanza ni utu"

"kwahiyo Watu kumshambulia AY kwa kuonekana kwenye majukwaa ya CCM sidhani kama ni haki, hawamtendei haki kwakweli kwa sababu ni haki yake ya kikatiba kuchagua upande anaoona yeye unafaa, hata sisi kuna Wasanii wengi wapo upande wa CHADEMA”

“Mimi pamoja na kwamba nipo CHADEMA lakini pia nilisaidiwa na Watu wa CCM wakiongozwa na Mwenyekiti wao Mama Samia Suluhu Hassan yeye alinisimamia matibabu yangu mwanzo mpaka mwisho lakini pia Makamu wa Rais Dr"

"Mpango alituchangia, Waziri Mkuu Majaliwa pamoja na kuja kuniona alituchangia milioni 10, Naibu Waziri Mkuu Dr. Biteko pia alituchangia milioni 10, tulienda Bungeni Dr. Tulia aliongoza Wabunge wakatuchangia milioni 5, lakini pia Katibu Mwenezi wa wakati ule Paul Makonda alituchangia milioni 20, Waziri wa Maji Aweso pia alituchangia milioni 10 yeye na Wizara ya maji”


Mbona "Madee Ally "-Seneda, yupo CCM ila yeye hawamsimangi
 
Mimi pia sina tatizo na wasanii kuwa CCM ni haki yao na wengine wanafuata maokoto wacha wakaokote pia ni haki yao,tatizo langu ni wale wanaoitukana na kuikashifu Chadema kama yule mpumbavu Jimmy Mafufu alitukosea sana yeye kwanza hajawahi kuwa Chadema alikuwa anatafuta umaarufu na kupiga hela ya CCM kwa kujifanya ametokea Chadema.
 
Back
Top Bottom