Project 2015: Mwinyi haoni uharaka wa Katiba Mpya



Mr. Zero:

Kwenye rangi nyekundu unampa points Mzee Mwinyi bila yeye kuja hapa. Unaomba mabadiliko ya katiba kwa kusikiliza mtu fulani. Wakati katiba yenyewe hujaisoma.

Na sio wewe peke yako ni watanzania wengi tu. Mpaka wabunge hawasomi na kuelewa katiba inasema nini.

Na kwa taarifa yako katiba ya sasa sio ya mkoloni. Katiba aliacha mkoloni ilitoa ruhusa ya vyama vingi. Ilitoa ruhusa ya mgombea huru. Ilitoa ruhusa mbunge kuhama kambi bila kupoteza ubunge wake.

Mapungufu yaliotolewa na jamaa yako hapo yanahitaji marekebisho ya katiba (amendments) na sio katiba mpya.
 
wasiwasi wa Mzee Mwinyi ni wa msingi.
1) Je hii ajenda ni ya Watanzania wengi, au ni ya kundi fulani la elites wanaodhani wanawakilisha maoni ya watanzania wengi?
2) Si kweli kwamba kutakuwa na katiba mpya asilimia mia moja , kuwa na katiba mpya kwa maana ya kuondoa vipengele vyote na kuleta vingine vipya hili haliwezekani, kinachowezekana ni kuifanyia katiba iliyopo mabadiriko makubwa sana.
3) Pamoja na kuonyesha mapungufu ya vipengele mbalimbali, je ni nini mbadala wa vipengele hivyo?, inawezekana mbadala huo ni mbaya kuliko vipengele vilivyopo. kwa hiyo ni dhahiri Suala la katiba ni suala la kuchangamsha akili, umakini wa hali ya juu, na si kukurupuka. Ninadhani wasiwasi wa Mzee Mwinyi ni katika mambo hayo.
 
Mwinyi and the likes sio future hawezi kutuamulia Tumpuuze,KATIBA A MUST!!!!
 
poleni mnaofuata mkumbo kopi ya katiba imo humu labda tuanze kusomeshana kuanzia kurasa hadi kurasa na tuwafahamishe na wengine halafu tuone jee tunataka katiba mpya au amendments
 
Mzee Mwinyi is either being disingenuous or misinformed. The clamour for a new constitution has been there since we went multiparty. That is why there have been many patches as my friend Zakumi claims. He is asking why now. I ask him when. If not now then when? When my grandson is 40 years old? As someone said elsewhere he is probably airing a message from the sitting President. He is in power now due to the inconsistencies in the current constitution. CCM is not interested in a new constitution because it will put them at par with other political contestants.
 
1. Umri wa mzee mwinyi umekwenda hata tukichinjana potelea mbali
2. Mzee mwinyi anaogopa kumalizia siku zake chache segerea
3. Mzee mwinyi ni miongoni mwa genge la watu waliojitwika usultani wa nchi hii wao, watoto wao, na wajukuu
4. Mzee mwinyi anamsemea jk wanafikiri sawa
5. Hofu mabadiliko ya katiba yatazua zahama na mashamba yake kutaifishwa
 
Mie mmoja napendekeza katiba mpya hio ni kutokana katiba ya Tanzania ni mbovu na imeshakuwa outdated.Mfano ni kifungu 64 chote pamoja na vitoto vyake.

Katiba ya 60's haiwezi kuwa valid sasa, ni lazima itupwe na iandikwe mpya kabisa.Kuna mizimu mingi ndani ya katiba iliopo.Moja jiulize wewe suali, ivi Tanzania kila chama kina sera yake kuhusu serekali ngapi pindipo kikishika madaraka.Kweli kitu hiki ni cha kuekwa kwenye political debate ?

Kurefraise, manaake katiba iliopo sasa CUF wakishinda kule Zanzibar ni serekali 3 nchi nzima....sawa na Chadema sera hii.Sasa hivi kama Tanganyika wameshinda CCM, na Zanzibar CUF ....Sera gani ifuatwe kuendesha Tanzania ?

Ndio wengine wakasema katiba haijitoshelezi!Iandikwe upya maana kiufungu hiki hakipo kabisa ndani ya katiba, why ? Jibu katiba ilipoandikwa ni miaka ya 60's, kule kulikuwa hakuna vyama vingi!

Jengine hapo kwenye uteuzi wa tume ya uchaguzi ndio mizimu mitupu.Yaani JK yeye ndie aliechagua nani awe referee wa uchaguzi!......
 
Nimejiuliza sana! Hivi ni kweli ni Uzee unasababisha uvivu wa kufikiri kiasi cha Mzee wetu Ruksa kutokuona umuhimu wa Katiba Mpya??
Hapana nadhani mzee anaogopa Katipa mpya itaweka mazingira mazuri na watu kuhoji juu la Loliondo Gate Issue!!
 
Kwanini unakuwa mzembe wa kupitia threads zingine. Thread kama hii imeshaanzidhwa.
 
Nimejiuliza sana! Hivi ni kweli ni Uzee unasababisha uvivu wa kufikiri kiasi cha Mzee wetu Ruksa kutokuona umuhimu wa Katiba Mpya??
Hapana nadhani mzee anaogopa Katipa mpya itaweka mazingira mazuri na watu kuhoji juu la Loliondo Gate Issue!!


Ana wasi wasi na mafao yake kwa sababu nchi masikini kama Tanzania haiwezi kuendelea kulipa mafao kwa Mizoga iliyotutia umasikini. Kuna kundi kubwa hapa la mawaziri wakuu, marais wastaafu ambao walijilimbikizia mali na hii katiba mpya ndio itakuwa kifagio cha kuondoa umangimeza. Vile vile wale waliotumia madaraka hovyo na kulitia hasara taifa lazima watetemeke kwa sababu Segerea inanukia wakati tutapata Rais asiyeiba kura i.e. rais Mwizi.
 
Mzee Mwinyi anaogopa katiba mpya itaondoa ndoto ya mwanae kuwa rais.
 
Achana naye huyu mzee. kwanza hoja zake hazina msingi hata wakuweza kuzijadili. Pili elimu yake ni yakutiliwa mashaka kuweza kutambua umuhimu wa katiba mpya. zaidi sana analinda masilahi yake na amepitwa na wakati jamani. We should not invest much on this mzee.
It is an absolute truth that the need to have a New Document with legal sanctity(Constitution) is irrebutable.
 
kwa hio ww unaona kuwa watu wa pwani ni watu wa mambo madogo ?


jiulize kwa nn mji mkuu wa tanzania uko pwani na sio bara ?

:target: uko dunia gani hujui mji mkuu wa tanzania upo wapi Pwani?????, u must be crazy
 
Kwanini Wazanzibari mnapenda saaana kutupangia na kutuamria ya kufanya juu ya mustakbari wa nchi yetu Tanganyika??? Zanzibar kubadilisha katiba ni sawa but kubadilisha ya bara....oohh haraka ya nini....mara oh why now...acheni ubinafsi,na haya mambo ndio yanafanya chokochoko za muungano zisiishe!!
 
Ananufaika na hii katiba MBOFUMBOFU ndo maana anaona mtamwagia ugali wake
 
Nadhani yeye katoa mawazo kama mtanzania mwingine. Na hayo ni mawazo siyo maamuzi, na kama ni hivyo hatuzuii sisi Wtz kuendelea na madai yetu ya katiba. Katiba mpya haitawafurahisha wengi ambao ni wachumia tumbo bila kuangalia maisha ya Wtz wengine ambao wana lala njaa, wanakosa matibabu na huduma nyingine lukuki kwa ajili ya mfumo mbovu wa kiutawala kwa baraka za katiba iliyopo. Kwa majibu yake AHM si kitu cha ajabu sana
 

Tunashukuru Mzee Mwinyi nawe kwa kulisemea hili, wewe ndio baba wa mageuzi na unaijua nchi yetu kwa kinaga ubaga. Hatuwezi kubadilisha katiba kwa shinikizo la wachache ambao wana uroho na uchu wa madaraka
 
Kama ulikua unadhani ya kwamba hili la Mzee Mwinyi juu ya Taifa la Tanzania kutaka kujiandikia KATIBA YAKE UPYA ni ajabu zaid basi ukajaribu kutazama picha kati ya MMBWA aliyeshiba na yule aliye na njaa kama kweli wanaweza wakacheza pamoja.

Katika taifa hili hili la kwetu ambako watu wengi tunashinda kwa mlo mmoja tu, wengine wetu huondoka mpaka mili sita yenye miraba mitatu kila kimoja. Yaani, si kusema tu kwamba wanakula cha kwao mpaka na cha watu wengine bali ukweli ni kwamba WANAKULA WANASHAZA na kushindilia.

Wanahistoria hutueleza jinsi gani ufedhuli wa majibu ya Malikia ulivyotokomesha kabisa mfumo wa kifalme nchini Ufaransa miaka mingi sana iliopita. Kwa mujibu wa maelezo hayo, siku moja Malkia wa Ufaransa alikua katika ziara binafsi mjini mara akakutana na umati mkubwa wa watu wakiandamana wakilalamikia kutokuepo mikate madukani na yeye kujibu kwa kejeli alipofahamishwa na dereva wake sababu za maandamano; akasema kama wanalalamikia mikate hao kwa nini wasipewe biskuti wakale. Majibu haya yaliweza kuwatia hasira wananchi na mapambano yakaenea nchi nzima. Matokeo yake mfalme ya familia yake yote ikauwawa na ndio ikawa ni mwisho wa mfumo huo nchini humo.

Nako hapa nyumbani kwetu, watu kama Mzee Mwinyi ambao ndio wazee waliobakia wa kutegemewa lakini cha ajabu kwao wao WAKILA CHAKULA MILO YOTE SITA YENYE MIRABA MITATU KILA KIMOJA WAKASHIBA NA FAMILIA ZAO basi wajihisi kwamba Wa-Tanzania wote nao tayari wameshiba kwa sababu wengine wameshawasaidia kula kwa niaba yao.

Kwamsingi huu inapotokea tena kwamba wanaamka na kuanza kudai kuandika MKATABA MPYA NA WATAWALA basi moja kwa moja wanaonekana ni watu wa ajabu kweli kweli. Hali hiyo inakua ya mshangao zaidi pindi Wa-Tanzania tunapodai katiba mpya HASA KWA WAKATI HUU ambao kwa maoni ya Mzee RUKSA nchi INAONEKANA KUJAA ASALI NA MAZIWA kila kona. Nadhani waandishi wa habari huenda walimkatisha tu kabla hajamalizia ya kwamba KATIBA TUNAWEZA TUKANDIKIWA TU VILEVILE katika karne hii ya 21 kama tulivyowahi kuandikiwa katiba nyinginezo 5 bila ya ushiriki wetu.

Sasa Wana-JF, kwa mzee wetu huyu nimepata kujifunza kitu kikubwa sana kutokana na kauli yake inayopingana na matakwa ya taifa zima. Nimegundua ya kwamba kadri kimbunga cha kudai katiba kinavyoendelea kutetemesha kila kona ya nchi na kwa watu wa matabaka yote mijini na vijijini, kuna (i) watu wanaoangalia KATIBA MPYA kwa msingi wa kitu gani ambacho BINAFSI huenda akaipoteza badala ya kuangalia mambo kwa misingi ya (ii) faida zipi ambazo UMMA wa Tanzania wanatarajia kupata kupitia mabadiliko hayo. Kwa mtaji huu ni vigumu sana wengine kupata kuelewana nao.

Bahati nzuri wa kusemea KATIBA si Mzee Mwinyi, Serikali, CHADEMA wala nani. Katiba ni mali yetu sisi Umma wa Tanzania na wala HAKUNA MAJIRA KATIKA MWAKA ambao ndio umeandikwa kuwa ni sahihi kudai katiba mpya. Mzee Mwinyi akipenda anaweza akamrithisha tu Dr Hussein Tanzania Bara hata Visiwani lakini kwenye katiba ya nchi akampitie to Makamba, Salmin Amur, Mzee Butiku na Mzee Mzindakaya ili wakahudhurie tu kama wajumbe wengine KWA URAIA wao na wala si VYEO VYAO.

Hivyo, kama kuna mtu aliingia MIKATABA YA AJABU AJABU na mataifa mengine kwa maslahi binafsi basi imekula kwako. Wenye mali wamedhamiria kujiandikia upya KATIBA yao full stop!!
 

huyu nae keshajizeekea asubiri kufa tuu atuachie nchi vijana..yeye katiba mpya inamuhusu nini wakati atakufa soon hata 2015 hafiki..? mwacheni aseme anayoyasema..nenda mzee!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…