Promota mnataka Mandonga afie ulingoni?

Mmhh hapa litakufa jitu😁😁
 
Ndiyo unamtisha Mandonga na hayo manyama uzembe? Minyama imelegea utadhani kuku la broiler
 

Hujaielewa falsafa yake wala hujamsikiliza mandonga akiongea.


Falsafa ya Mandonga ni akishinda au akishindwa ulingoni yote hayo ni ushindi kwake.

Hivi wewe hujaona kuwa mapambano mawili yaliyompatia umaarufu wa kujulikana mandonga alipigwa ulingoni?

Fatilia kidogo.

Mandonga yupo kivingine kabisa na kaelewa namna ya kuitumia hii fursa iliyopo kwenye media.


Wengi wetu mamndonga akishinda hatuna raha. Tunataka anyukwe tuone anavyopanguwa hoja nje ya ulingo.

Mandonga ndiyo mwanamichezo pekee anayeelewa kutumia fursa za kushindwa mchezoni.

Mandonga haingii ulingoni kuuwa wala haiingii kujiuwa, akiona unamzidi anajitupa anahesabiwa, ananyanyuka, kipato kishajiingizia, anapiga porojo nyingi, mnamtafuta kwa promo anaendelea kula pesa kuliko mshindi.

Mandonga akishinda au akishindwa ulingoni anabaki kuwa bingwa.

Katika miaka ya sitini huko, kuna Mkimbiaji wa Tanzania "John Stevens" alipata umaarufu mkubwa duniani siyo kwa kushinda bali kwa kushindwa, alikuwa wa mwisho kabisa kwenye Marathon. Mtafute kwenye mtandao utamuona ni vipi kushindwa kulimpa umaarufu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…