Propaganda zinashinda vita kwenye uwanja wa medani, case ya vita ya Russia Ukraine

Propaganda zinashinda vita kwenye uwanja wa medani, case ya vita ya Russia Ukraine

Nkerebhuke

JF-Expert Member
Joined
Nov 1, 2021
Posts
796
Reaction score
2,026
Vita ni tamu kusimulia kutokana na matendo yake ya kishujaa lakini pia vita ni chungu kuiona kutokana na matukio ya mstari wa mbele yaani kumwaga damu kikatili na kupatwa kwa ugonjwa wa post traumatic stress kwa participants wote wa vita.

Leo nataka niwafahamishe vijana wadogo wajue kuwa vita inapigana sana kwa propaganda kupitia vyombo vya habari kisha uwanja wa medani. Uvumizi wa Russia dhidi ya jirani yake imeprove nguvu ya propaganda kwani hata hapa kwetu Tanzania kuna makundi mawili yanayounga mkono upande mmoja unaoshiriki hii vita. Propaganda ni njia ya kupika taarifa kwa lengo la kupata uharali wa kufanya Jambo flani kama uvumizi wa kijeshi, kupata umaarufu wa kisiasa au kupata ushawishi. Kama ilivyokuwa US kutunga uongo wa kuivamia Iraqi kisa anamiliki silaha za maangamizi ndivyo Putin alivyoivamia Ukraine kwa madai ya kuwa kitisho cha usalama wa nchi yake.

Propaganda ni mtaji muhimu sana kwenye aina yoyote ya vita yaani jeshi kubwa linaweza kuwa embarrassed na jeshi dogo kama likipata uungwaji mkono wa watu wake hili limeonesha na jishi jeshi la urusi lilivyokwaa kisiki ndani ya ardhi ya Ukraine. Hali hii inachagizwa na vyombo vya habari vya magharibi ambavyo sympathetically vinapika propaganda kuonesha kuwa Russia anafanya jinai kutekeleza operation ya kijeshi ndani ya Ukraine.

Kama ilivyokawaida kwa unafiki wa mabeberu ikiongozwa na big fish US wanabainisha kuwa hawaungi mkono Ukraine kuishambulia Urusi lakini vita inaenda kuchukua Sura mpya baada ya Russia kuanza kushumbuliwa kuhujumu vyanzo vyake vya uchumi.

Kwa upande mwingine Russia anapika na kuoneza propaganda kuwa kuwa Ukraine amekuwa rats root ya mabeberu ya kumnyemelea na kuhujumu usalama wake. Kwa hali hii atakaewini propaganda ndio atakaeshinda vita. Muhanga mkubwa kwenye uwanja vita ni ukweli unapaswa kuwa na analytical mind kuweza kujua nani mkweli vinginevyo utabaki kwenye illusion ya ushabiki wa ubeberu wa mabwenyenye au usoshalisti wa Russia and it's allies.
 
uzi wako ulivyoka sijui ni maoni, mtazamo au?? nashindwa nichangie vipi!!! anyway mi naikubali sana Urusi.... ni mkombozi wa dunia zidi ya mabeberu ya Magharibi!!

URUSI TAIFA TEULE
 
uzi wako ulivyoka sijui ni maoni, mtazamo au?? nashindwa nichangie vipi!!! anyway mi naikubali sana Urusi.... ni mkombozi wa dunia zidi ya mabeberu ya Magharibi!!

URUSI TAIFA TEULE
Sio dhambi kuwa na upande maana propaganda in its operation sense lazima kuna kundi litashawishika na upande kupitia sera zake wakija wa upande wa pili watakuja na maoni ya upande wao. Lakini wapo ambao hawana upande wao Amani na maridhiano ndio Imani yao.
 
Sio dhambi kuwa na upande maana propaganda in its operation sense lazima kuna kundi litashawishika na upande kupitia sera zake wakija wa upande wa pili watakuja na maoni ya upande wao. Lakini wapo ambao hawana upande wao Amani na maridhiano ndio Imani yao.
Mkuu Nkerebhuke muda mrefu umepotea. Nakumbuka mwanzo kabisa wa vita hii tulikuwa kwenye ule uzi wa updates kinachojiri ukraine pamoja na mkuu Nyamizi
 
Huwa nashangaa sana watu wanapo mtuhumu Mrusi kwa Propaganda, sisemi kwamba hafanyi propaganda ila hana Vyombo vya habari wala network yoyote Dunia nzima kueneza Hizo propaganda,

At same Time Ukraine na washirika wake wana Vyombo kwa maelfu kueneza propaganda na uongo. Imefika stage wanaongea uongo hadi wanasahau kama jana tu wamedanganya.
 
Back
Top Bottom