Anatakiwa kula chakula chochote kile.hakuna kinachozuia kula kwenye tatizo alilonalo.Uko mkoa gani ili watu wajue namna ya kukuelekeza?Nina mzee wangu ambaye ana tatizo la kibofu cha mkojo ni mzee miaka kama 63 hivi,ninampango wa kumpeleka Hospital akafanyiwe matibabu sahihi,wakati najiandaa kifedha naomba sana Mnisaidie nijue mgonjwa wangu huyu anatakiwa asile vyakula gani na ale vyakula gani wakati nasubiri kumpeleka hospitali.
Pia naomba mwenye mawasiliano na daktari mtaalam wa ugonjwa huu anipe namba zake
Nawasilisha.
Anatakiwa kula chakula chochote kile.hakuna kinachozuia kula kwenye tatizo alilonalo.Uko mkoa gani ili watu wajue namna ya kukuelekeza?
Ni kweli hajapimwa na kudhibitika kuwa ana Prostate cancer lakini mimi nimeita hivyo baada kuona ana matatizo ya kukojoa mara kwa mara na wakati mwingine anakojoa matonematone tu.Nashukuru kwa mawazo hayo inabidi kwanza akapimwe ili idhibitike ni Prostate cancer au ni matatizo mengine ya kukojoa.Matatizo ya kibofu cha mkojo sio lazima yawe kansa. Prostate cancer ni tofauti.
Unaweza kumuona dr asheesh wa agha khan akakupa ushauri. Ila kama umeshathibitishiwa na vipimo kuwa ni kansa, basi dr ngoma anakufaa. Ana clinic mwenge lakini pia unaweza kwenda ocean road cancer institute.
Pole sana.
Je, imethibitishwa kwamba ana kansa ya prostate? kama bado haijathibitishwa, ni vizuri akapelekwa bugando ili afanyiwe vipimo.Mimi niko wilaya ya kahama shinyanga,nashukuru kwa maelezo hayo maana kuna mtu alishanishauri kuwa asitumie vyakula vyenye sukari na asile nyama kwa wingi.
Je, imethibitishwa kwamba ana kansa ya prostate? kama bado haijathibitishwa, ni vizuri akapelekwa bugando ili afanyiwe vipimo.
Tatizo la bugando, ni kwamba kuna Urologist mmoja tu, anaitwa Dr.Igenge.na hii ni baada ya daktari bingwa mzoefu wa siku nyingi kustaafu.
Sasa hospitali hii inahudumia wagonjwa kutoka kanda ya ziwa na kanda ya magharibi.Kumpata daktari huyu lazima umuone kwenye PRIVATE APPOINTMENT hapo hapo bugando.kwa kuwa clinic ya kawaida imejaa wagonjwa kibao, na madaktari waliopo sio madaktari bingwa, watapiga siasa na kumcheleweshea ndugu yako matibabu.