PSPTB Ivunjwe??!

Larusai Mux

JF-Expert Member
Joined
Oct 24, 2012
Posts
979
Reaction score
277
Wakuu wanajf,
huu ni mwezi unakaribia wa nne sasa toka wanabod wa Ugavi Na Ununuzi au Procurement & Supplies wafanye mitihan lakin hadi sasa matokeo hayajatoka!
Nakumbuka mitihani ya PSPTB Ilifanyika wiki moja baada ya mitihani ya CPA kuanza!,ila cha kushangaza matokeo ya CPA yametoka yapata miezi 2 sasa!,hakuna taarifa maalum iliyotolewa na PSPTB kwa ucheweleshaji wa matokeo haya.

My take; Hii bod ivunjwe iundwe upya?!
 

Tatizo la hii bodi ni huyu punguwan Tesha. Huyu jamaa ni kiazi sana, anairudisha sana nyuma hii bodi, lakini bado anaangaliwa tu. Kuna watu makini kama kina Songoro wapewe kazi hii wataifanya vizuri...
 
Tatizo la hii bodi ni huyu punguwan Tesha. Huyu jamaa ni kiazi sana, anairudisha sana nyuma hii bodi, lakini bado anaangaliwa tu. Kuna watu makini kama kina Songoro wapewe kazi hii wataifanya vizuri...

ni kweli kabisa mkuu,tena huyu Tesha si ana kashfa na kesi mahakaman!!,sijui imeishia wapi,
 
Miezi minne! Je mlifanya wanafunzi wangapi? Je kozi (mtihani mmoja), kwa wastani, mtu anatumia scripts ngapi?
Hii ni hatari, ikiwa kama NECTA waliendesha mtihani wa watahiniwa zaidi ya laki nne, na wametoa matokeo. Labda hiyo bodi itakuwa imempa tenda mtuu mmoja ili asahihishe.
 
hivi taarifa rasmi zinasemaji tujisajili tu na tunajisajili kwa matokeo gani..? maana nilienda pale bddi mwezi huu mwanzoni ila wakawa hawana taarifa za kueleweka eti wananiambia niendele kusubiri matokeo
mwenyewe taarifa zaidi anaijuze
 
hivi taarifa rasmi zinasemaji tujisajili tu na tunajisajili kwa matokeo gani..? maana nilienda pale bddi mwezi huu mwanzoni ila wakawa hawana taarifa za kueleweka eti wananiambia niendele kusubiri matokeo
mwenyewe taarifa zaidi anaijuze

Kuna jamaa kaniambia kuwa kasikia kwamba tunaruhusiwa kufanya pepa, vimeo vyote vitafanyika mwezi november
 
isije kuwa labda waliweka usimamizi mkali na matokeo yake 70% wamefeli hivyo wanatafuta jinsi ya kuelezea, yaani kama yale ya Form IV wakuu
 
isije kuwa labda waliweka usimamizi mkali na matokeo yake 70% wamefeli hivyo wanatafuta jinsi ya kuelezea, yaani kama yale ya Form IV wakuu

Kwani usimamizi ukiwa mkali ndiyo watahiniwa wanafeli?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…