PSSSF yazindua Baraza la Wafanyakazi Kidijitali Lengo ni kupunguza gharama

PSSSF yazindua Baraza la Wafanyakazi Kidijitali Lengo ni kupunguza gharama

Mliogwa

Member
Joined
Jun 6, 2024
Posts
37
Reaction score
37
WhatsApp Image 2025-02-07 at 07.57.53_816b24d9.jpg

IMG-20250207-WA0006.jpg
Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) umezindua Baraza la Wafanyakazi linaloendeshwa kidijitali kwa lengo la kupunguza gharama za uendeshaji na kusaidia jitihada za kulinda mazingira.

Uzinduzi huo uliofanyika jana Februari 06, 2025 Mkoani Singida, uliongozwa na Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini wa PSSSF, Bi. Joyce Mapunjo, ambaye aliipongeza Menejimenti kwa hatua hiyo muhimu katika kuongeza ufanisi wa baraza.
IMG-20250207-WA0004.jpg

IMG-20250207-WA0002.jpg
Sambamba na uzinduzi huo, Bi. Mapunjo alifungua kikao cha Baraza la Wafanyakazi wa PSSSF kilichoanza Februari 6 na kinatarajiwa kukamilika Februari 7, 2025.

Mwenyekiti huyo amewataka Watumishi wa PSSSF kutimiza wajibu wao wa kutoa huduma bora kwa Wanachama ili kuhakikisha malengo ya Serikali inayoongozwa na Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, yanafikiwa.

Amesisitiza umuhimu wa kila mfanyakazi kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi ili kusaidia Serikali kufikia malengo yake ya kuwahudumia wananchi, wakiwemo wastaafu wa PSSSF.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Baraza la Wafanyakazi la PSSSF ambaye pia ni Mkurugenzi Mkuu wa PSSSF, Abdul-Razak Badru, alisema kuwa kila kinachofanywa na PSSSF kina lenga kutafsiri ndoto kubwa ya Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kujenga Taifa imara kiuchumi.

Akizungumzia Baraza hilo kuendeshwa kidijitali, Badru alisema, "Lengo kubwa ni kuendana na jinsi tunavyowahudumia wanachama wetu, kwani hivi sasa tunawahudumia kidijitali na sisi tunapaswa kwenda vivyo hivyo.

"Pia najua Baraza ni chombo muhimu katika kutoa maamuzi, Baraza la PSSSF linashirikishwa katika mambo yote muhimu ya uendeshaji na linaleta tija katika utendaji wa Mfuko."
IMG-20250207-WA0008.jpg
Naye Mjumbe wa Baraza la PSSF kutoka TUICO Makao makuu Bw. Peles Jonathan-Hageza, aliipongeza PSSSF kwa jinsi inavyoshirikiana na Baraza hilo katika masuala mbalimbali muhimu ya kiuendeshaji.

Baraza la Wafanyakazi la PSSSF la sasa ni baraza la pili tangu kuanzishwa kwa PSSSF mwaka 2018.
 
Badru, alisema kuwa kila kinachofanywa na PSSSF kina lenga kutafsiri ndoto kubwa ya Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kujenga Taifa imara kiuchumi.
Aache uongo huyo mzee mtu mzima. Mbona hataki kulipa wanufaika haki zao kwani hayo ndio maelekezo ya Dk. Samia?
Wanamtajataja mama wa watu ili kumtoa kwenye reli asiwashtukie
 
Pamejaa wezi hapo PSSSF HQ usipime!

Nina mzee hapa ana RB toka 2021 alitapeliwa na hao jamaa baada ya kuwasiliana na kitengo cha huduma kwa wateja HQ.

Ukipiga hiyo namba rasmi ya ofisi utasikilizwa then utaambiwa tutakupigia baadae ngoja tulifanyie kazi.

Hiyo baadae utapigiwa na namba isiyo ya ofisi na mtu yuleyule wa PSSSF akiwa na taarifa zako zote na atakupotosha akihitaji utume pesa.

Jeshi letu la polisi linahitaji watu wenye weledi hasa kitengo cha cyber au PPP ya Kafulila.

Namba za simu zilizotumika zinapatikana hadi kesho na control namba iliyotumwa na huyo tapeli ipo na majina yake matatu ila mpelelezi sound kibao akisingizia TCRA HQ ndiyo mchawi.
 
Back
Top Bottom