Psychedelic Drugs & Consciousness

😂😂😂😂🤣🤣🤣😂😂😂🤣
 
🤨🤨🤔🤔🤔🤔
 
Naam uzi murua kabisa.

Mchango wangu kuhusu bhangi

Inakufanya utambue ujinga wa kurudia vimizunguko vya viujinga vilevile kila siku mfano unalala unaamka tena unalala tena na kuamka! au unakula unakunya unakula tena unajisaidia tena na tena! au unaenda kaziini unarudi unaenda tena kazini unarudi ni kama ujinga fulani. Au mnapiga kura anakuja raisi mnapiga tena kura ni kama kila siku tunapiga kura japo wao kuweka miaka mitano tunaona kama ni proceeeeeees kumbe tunarudiaga viujinga vilevile kila mara. Vipo vingi tu, unakunywa maji unakojoa tena unakunywa maji unakojoa tena😏. Unatafuta hela unapata unatumia tena unatafuta yaani unaona kama ni mchakato kumbe ni ujingaujinga na marudio ya viujinga ukitafakari.

Nisiendelee sana msije kuwaza nipo high mazee

Nahisi kutambua kinamna hiyo kunasababisha baadhi ya wavutaji kukosa mwamko wa kutafuta baadhi ya vitu -Amotivation Syndrome

Mfano mtu anakaa anawaza; nifanye bidii nijinyime kula vizuri sasa hivi ili ninunue gari halafu linifanye nisitembee sana afya yangu izorote nitakiwe tena kwenda gym/au jogging mazoezi ya kutembea[sasa nakimbia nn kama nimerudi tena kutembea?] na bado nikatazwe sasa kula vizuri tena safari hii kwa lazima. - Ukiangalia haka ni ka mzunguko ka viujinga tu unakuwa amotivated being living in the now.

Lakini faida labda itakuja pale mtu akishatambua hayo yote na akaondokana na ule uoga wa kulazimishwa kufanya mambo fulani fulani/ out of neccesity or fear.

Badala yake anakuwa mtu huru mwenye kufanya mambo kwa kupenda na kukua [Love, growth, service] na sio kwa ulazima au uoga fulani. Mtu huyu anayo furaha ya kweli katika mafanikio yake hapa duniani na zaidi.

Changamoto ni kwamba baadhi ya watu ukiwaondolea uoga na neccesity hawatataka kufanya kazi yoyote tena inakuwa ni hasara kwa jamii yetu. Kwa hiyo ni bora tu viendelee kupigwa marufuku.

Siku tukijiridhisha sasa kuwa watu wamejaa upendo na wapo motivated kukua na kuwa watumishi wa watu na kuacha alama nzuri duniani ndio madawa yaliyokatazwa yataacha kuwa hasara kwa jamii. Lakini kwa sasa wacha tu wayaangalie kwa makini [REGULATE].

Tutajuaje tumefika huko? Ni pale ambapo matendo ya kishujaa ndiyo yatashika headline za habari. Ni kama unavyoona muvi za kizungu wanavyopaisha heroism,love, service na legacy....... sasa hiyo ikiwa reality ndiyo tutakuwa tumepiga hatua. Contrast na muvi za kibongobongo ambapo dhima nyingi zinakuwa ni kuepuka mabaya fulani usaliti, uoga wa vifo laana na kukimbia umasikini.

Ushauri: Tusiwaige wazungu waliofikia hatua ya kutafuta matakwa wao hawana hasara mmoja akiacha kufanya kazi maana ni kweli ni kwa hasara yake[hatapata matakwa yake binafsi].....
..... ila kwetu bado tunatafuta mahitaji hivyo mmoja akiacha kufanya kazi ni hasara kwa jamii maana kama anaishi inamaana anatumia mahitaji - atanyonya nguvu za wengine.

Amotivation kwa bhangi imesingiziwa pakubwa [mda mwingine yenyewe ndio motivator mkuu kabisa]. Lakini kwa madawa mengine [hard drugs] ndiyo menyewe haswaa. So on second thought tunaweza kuruhusu bhangi ila sio madawa ya kulevya. Nawasilisha.
 
Niggas promoting drug abuse kwa kivuli eti ni mind opening, sio kwa Tz hii na hauez elewa mpaka uwe angalau ulishakaa MAT clinic ukahudumia watu wanaokumbwa na urahibu. hakuna ugonjwa mbaya kama uraibu wa madawa ya kulevya na siku Tz wakiruhusu bangi iwe legal basiii naamin tutapoteza nguvu kubwa sana ya taifa.
 
umesoma vizuri uzi wote?
binafsi sijaona anaye hamasisha kutumia madawa ya kulevya.
nb: hata pombe tunazokunywa ni madawa ya kulevya na wengi hawajui namna sahihi ya kutumia/kunywa.
 
Mkuu Mk54 vip na sisi wanafunzi tunaweza kutumia bangi kama tukiwa na purpose ya kusoma ili tuwe na kumbukumbu zaidi na sio for recreational na pleasure!!!
 
Mkuu Mk54 vip na sisi wanafunzi tunaweza kutumia bangi kama tukiwa na purpose ya kusoma ili tuwe na kumbukumbu zaidi na sio for recreational na pleasure!!!
Unaweza kutumia mara moja kwa miezi sita. Bangi siyo ya kutumia kila siku.
Bangi inakusaidia kuwa kwenye timeless moment ambayo ni "now". Itakusaidia usijidumbukize kwenye past na kuwaza vitu vilivyopita, kwa kifupi inakufanya uwe focused zaidi na inaongeza concentration.
Hivyo ikitumika kwa jinsi nilivyokueleza itakuamsha zaidi.
 
Hii marketing ya bangi na madawa ya kulevya iliyofanywa hapa imezidi kipimo kabisa.. Ni hatari mno. Huu uzi ufutwe haraka.
 
Wakuu poleni na majukumu, naomba kuuliza kama kuna mtu anaufahamu huu mmea. Kuna Boss wangu (Indian old man) amekuwa akitumia kila asubuh kwa kuweka kwenye maji yake ya kunywa.
Kama kuna ambaye yupo familiar na huu mmea ningeomba kujua yafuatayo...
1. Unaitwaje?
2. Unasaidia nini/faida zake ukiutumia?
3. Madhara yake?

Naomba kuwasilisha. Ahsante
 
Huu unapatikana kanda ya ziwa unaitwa kashagara ....kama nimepatia ni dawa inayotibu magonjwa mengi sana
 
Unaitwa kashwagala
Ni dawa ya magonjwa mengi Kuanzia tumbo ( la Aina yoyote ) na mengine mengi.
Mdiku Jafaar wenye Makao Arusha Tiba asilia wanautumia Sana.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…