Huyu mtu, hata Mi nilihisi anahusika kwa kiasi fulani, ingawa wengine walimtaja mpaka Suge Knight, na nafikiri ndio maana Mase alikaa naye mbali kwa kujitoa kidogo kwenye music, ili asije akapatwa na matatizo hata ya kuuawa kwa kuongozana na mtu wa aina hii, miaka ya 2000's mwanzoni, rapper Shyne kutoka Bad Boys alifungwa jela miaka 10, baada ya kupiga risasi, ili kumtetea P.Diddy asiuawe, nafikiri tukio hili lilitokea muda mfupi baada ya Snoop Dogg, kunusurika kuuawa, P.Diddy na Snoop Dogg walishanusurika kuuawa baada ya kila mmoja kumtumia mwenzie wauaji but now P.Diddy, Snoop Dogg na East Coast, Bad Boys na West Coast kwa ujumla, walishasameheana na wana maelewano mazuri, ndio maana kuna muziki mmoja wa P.Diddy, watu wa West Coast kama Snoop Dogg na Mike Tyson walionekana. Mike Tyson ni mshikaji mkubwa sana wa West Coast, West Side, na 2pac, Tupac, alipigwa risasi muda mfupi baada ya kutoka kwenye pambano la Tyson na Bruno la 96, inasemekana ilikuwa ni dakika 45 baada ya pambano, gari aliponda iliposimama kwenye mataa, siku hiyo hakuwa amevaa bullet proof, shuhuda mmoja aliyekuwa karibu sana na eneo, aliuawa baada ya siku 3, wakati 2pac alifariki baada ya siku 9, akiwa hajitambui kabisa na akipumulia mashine, 2pac na Big walikuwa marafiki but kutokuaminiana na wivu, kuliwafanya wachukiane, kutokuaminiana, wivu, majivuno, chuki, unafiki, makundi, kuliwacost uhai wao.