SI KWELI Punyeto husababisha Kunyauka na Kusinyaa kwa ngozi

SI KWELI Punyeto husababisha Kunyauka na Kusinyaa kwa ngozi

Baada ya kuitathmini taarifa hii, tumebaini kuwa si ya kweli.
Hivi ni kweli kuwa punyeto iliyokithiri hupelekea tatizo la kukauka na kusinyaa kwa ngozi?

IMG_6663.jpeg
 
Tunachokijua
Punyeto ni tendo analofanya mtu, likihusisha kujisisimua sehemu zake za siri ili afikie utimilifu wa kihisia (Orgasm).

Takwimu
Tofauti na jinsi ambavyo watu wengi hudhani, tendo hili halijali jinsia ya mtu. Wanaume na wanawake wote hupiga punyeto.

Katika utafiti mmoja uliofanyika nchini Marekani ukihusisha vijana wa kike na kiume wenye umri kati ya miaka 14-17, 73.8% ya wavulana wote waliofanyiwa utafiti walikiri kupiga punyeto mara kadhaa, huku 48.1% ya wasichana wote waliofanyiwa utafiti wakikiri pia kufanya tendo hili.

Kwa watu wazima wenye umri kati ya miaka 57-64, 63% ya wanaume hupiga punyeto, huku wanawake wakiwa ni 32%.

Punyeto na kukauka kwa ngozi
JamiiForums imefuatilia jambo hili kwa kurejea machapisho mbalimbali pamoja na tafiti za afya. Tumebaini mambo yafuatayo;
  1. Punyeto haisababishi kukauka au kusinyaa kwa ngozi
  2. Madhara makubwa ya tendo hili ni kuleta uraibu, utegemezi, kuvimba na kuchubuka kwa sehemu za siri, kutokuridhika kirahisi, uchovu mkubwa pamoja na kudhoofisha mahusiano ya watu wa jinsia tofauti.
  3. Nadharia za ubaya wa jambo hili kwa kiwango kikubwa huwa na asili ya dini
Kwa upande mwingine, tendo hili linapofanyika kwa kiasi huwa na faida ya kupunguza stress, hupunguza maumivu ya mwili na huboresha usingizi.

Ni tendo zuri kwa watu waliotengwa na jamii, pia ni njia ya kujikinga na ujauzito usio tarajiwa pamoja na magonjwa ya zinaa.
Nyeto ni zoezi tosha la kuzuia kumwaga. Wakati wa sex unaweza zuia kufika mshindo hata mara 4 na utakapo amua kuliachia bao, huwa bao very strong in term of pleasure kiasi kwamba huna haja for second round.
 
Back
Top Bottom