Putin hana budi kuchochea vita ili anusurike

Putin hana budi kuchochea vita ili anusurike

Mrengwa wa kulia

JF-Expert Member
Joined
Mar 21, 2022
Posts
1,091
Reaction score
3,695
Uhamasishaji wa kijeshi Urusi na kura za haraka za maoni katika maeneo yanayokaliwa mashariki mwa Ukraine ni ishara za udhaifu.

Putin amekosea; gharama wanalipa maelfu ya Warusi kwa maisha yao.

Rais Putin hawezi kurudi tena nyuma: Na ikiwa atashindwa katika vita vyake vya uvamizi dhidi ya Ukraine, itamgharimu madaraka yake, na yumkini zaidi ya hayo. Hali iatkuwa hivyo kwa wawakilishi wa bunge la Duma, ambao hatma yao hivi imeunganishwa na ile ya mkuu huyo wa Kremlin.

Wote wako katika hali ya taharuki kufuatia mafanikio ya karibuni ya vikosi vya jeshi la Ukraine katika kurejsha maeneo ya nchi yao yaliokaliwa.

Hali inaitishia Moscow kushindwa kijeshi, jambo ambalo hakuna alielitarajia mjini Moscow. Kutokana na hofu hiyo, Putin ameamuru kuwekwa tayari wanajeshi laki tatu wa akiba kwa ajili ya kwenda uwanja wa vita.
Jukumu la wanajeshi hao litakuwa kuzuwia kasi ya vikosi vya Ukraine kusonga mbele zaidi.

Putin Amedhoofika na alietengwa.
Uturuki, India na hata China ziliweka wazi kwamba zinapinga vita vya Putin, zinaunga mkono uhuru wa mipaka ya Ukraine. Na zilikuwa sababu za msingi:

Vita hivyo ni mzigo kwa uchumi wa dunia na vivyo hivyo kwa mamlaka ya wanasiasa hao, ambao Putin alitumai kupata uungwaji wao mkono kwa ajili ya vita vyake.

Mabadiliko ya mwelekeo katika Kremlin
Kwa mtazamo wa Kremlin, mambo hayangeweza kuendela hivi. Hivyo mjini Moscow, Putin anaharakisha kubadili mwelekeo na hivyo ukusanyaji huo wa wanajeshi kwa sehemu ni kukiri juu ya udhaifu wa kijeshi mashariki mwa Ukraine.

Kwa matangazo ya kuitisha kura ndani ya siku chache katika maeneo yaliotekwa kuhusu kujiunga na shirikisho la Urusi, ni wazi kwamba wa Ukraine hawataki kujiunga na Urusi. Kwa sababu kura inayofanyika mbele ya mtutu wa bunduki, kura ya maoni katika magofu, hakuna yeyote duniani anaweza kuichukulia kwa uzito.

Putin anataka kupata mali zilizoporwa. Maeneo yaliotekwa yatakuwa sehemu ya shirikisho la Urusi. Kisha Putin anaweza kutoa wito wa kutetea taifa kwa kutumia nguvu za kijeshi. Kile kinachoitwa operesheni maalumu ya kijeshi, ambayo ina mipaka ya muda na nafasi na ambayo haikuhusika kwa vyovyote na maisha ya kila siku ya Warusi walio wengi, inageuka kihistoria utetezi wa ardhi ya Urusi kwa njia zote, ikiwemo silaha za nyuklia.

Mtu haitaji kuwa nabii mkuu kutabiri mwisho unaokaribia wa neno operesheni maalumu. Propaganda ya Kremlin italizika neno hilo. Badala yake, kutakuwa uongo zaidi na zaidi wa kipumbavu na kuchanganya, uzushi, vitisho ambavyo vituo vya televisheni vinavyodhibitiwa na serikali vitatumia kuwarubuni Warusi.

Hata sasa inadaiwa kuwa Urusi haifanyi vita dhidi ya Ukraine, lakini inanjitetea nchini Ukraine dhidi ya Marekani na Uingereza. Hilo wanaliamini wanaotaka kuamini.

Uchochezi mpya wa Putin utachuliwa kwa uzito na viongozi wa dunia wanaokutana hivi sasa katika hadhira kuu ya Umoja wa Mataifa mjini new York. Lakini sera yao kuelekea Moscow haitabadilika pakubwa. Kiev itaendelea kupokea silaha, jeshi lake litadelea kupambana. Na wanajeshi 300,000 wa akiba wa Urusi? Hawajawahi kuwa vitani, hawana zana za kutosha. Ni watu wenye familia, wanaume wanaotenganishwa na maisha ya kila siku dhidi ya matakwa yao.

Source: DW
 
Kuna atakayepona kwenye iyo vita ya nuclear.maana itakuwa piga nikupige.kikubwa ni kuomba Mungu wakae meza moja
Hilo jeshi la akiba la watu 300,000 litafyekwa lote ndani ya wiki mbili kisha Putin atatishia kutumia silaha za nuclear na hapo ndipo usa anapopasubiri kwa hamu ili aingie mzigoni rasmi
 
Yani hata kama wewe ni mwanajeshi wa Ukraine alafu unasikia adui anaongeza zaidi ya wanajeshi laki 3,uwezi ukawa na furaha maana unajua kabisa mpaka hao mia 3 waishe sizani kama utakuwa bado duniani
Hilo jeshi la akiba la watu 300,000 litafyekwa lote ndani ya wiki mbili kisha Putin atatishia kutumia silaha za nuclear na hapo ndipo usa anapopasubiri kwa hamu ili aingie mzigoni rasmi
 
Andikeni hata nyuzi 600 per day, andikeni nyuzi ndefu zenye kuwafurahisha ila ukweli Ukraine amepoteza tena majimbo mengine kama ilivyo cremea. Kama kweli Ukraine na west ni wababe basi wayarudishe hayo majimbo, au waingie urusi kuchukua maeneo kama urusi anavyofanya. Hapa JF tutadanganyana mpaka mwisho.
 
Andikeni hata nyuzi 600 per day, andikeni nyuzi ndefu zenye kuwafurahisha ila ukweli Ukraine amepoteza tena majimbo mengine kama ilivyo cremea. Kama kweli Ukraine na west ni wababe basi wayarudishe hayo majimbo, au waingie urusi kuchukua maeneo kama urusi anavyofanya. Hapa JF tutadanganyana mpaka mwisho.
Wanabweka bweka ovyo kama mbwa
 
Andikeni hata nyuzi 600 per day, andikeni nyuzi ndefu zenye kuwafurahisha ila ukweli Ukraine amepoteza tena majimbo mengine kama ilivyo cremea. Kama kweli Ukraine na west ni wababe basi wayarudishe hayo majimbo, au waingie urusi kuchukua maeneo kama urusi anavyofanya. Hapa JF tutadanganyana mpaka mwisho.
Sasa west wayachukue majibo ya urusi ili iweje[emoji16]
 
Yani hata kama wewe ni mwanajeshi wa Ukraine alafu unasikia adui anaongeza zaidi ya wanajeshi laki 3,uwezi ukawa na furaha maana unajua kabisa mpaka hao mia 3 waishe sizani kama utakuwa bado duniani
Wanajeshi wa Ukraine walikabiliana na majeshi ya Urusi tena wale wenye mafunzo kamili na uzoefu wa vita wakiwa na vifaa tele vya kijeshi tena wakiwa wameingia Kiev na wakawashinda tena kwa kishindo halaf ndo eti sasa wawaogope hao wa reserve ambao wengi wao sio full trained na hawana uzoef wa kutosha yaan jeshi la ukraine liogope jeshi la akiba? na mpaka urusi inatumia reserve ni kumaanisha urusi ana hali tete kwenye uwanja wa vita.
 
Andikeni hata nyuzi 600 per day, andikeni nyuzi ndefu zenye kuwafurahisha ila ukweli Ukraine amepoteza tena majimbo mengine kama ilivyo cremea. Kama kweli Ukraine na west ni wababe basi wayarudishe hayo majimbo, au waingie urusi kuchukua maeneo kama urusi anavyofanya. Hapa JF tutadanganyana mpaka mwisho.
Hii ni forum hujakatazwa kuandika nyuzi kinakuuma nin wenzako wakiandika nyuzi acha ujinga na uzwazwa
 
wanajeshi wa Ukraine walikabiliana na majeshi ya Urusi tena wale wenye mafunzo kamili na uzoefu wa vita wakiwa na vifaa tele vya kijeshi tena wakiwa wameingia Kiev na wakawashinda tena kwa kishindo halaf ndo eti sasa wawaogope hao wa reserve ambao wengi wao sio full trained na hawana uzoef wa kutosha yaan jeshi la ukraine liogope jeshi la akiba? na mpaka urusi inatumia reserve ni kumaanisha urusi ana hali tete kwenye uwanja wa vita
Nchi hii inawajinga wengi watu walikabiliana na makimandoo wenye moral waje wawaogope hao ambao wanamda mrefu walikua sio active
 
Kuhusu Turkey, China na India Dw imeandika kichekesho😆 na huo uchambuzi wote umeonekana wa hovyo.
 
Nchi hii inawajinga wengi watu walikabiliana na makimandoo wenye moral waje wawaogope hao ambao wanamda mrefu walikua sio active
kwa hiyo ina maana Mauripol, Luhansk, Donesk na Kherson mmezirudisha ukraine au ni kwamba mnajitekenya wenyewe
 
Wanajeshi wa Ukraine walikabiliana na majeshi ya Urusi tena wale wenye mafunzo kamili na uzoefu wa vita wakiwa na vifaa tele vya kijeshi tena wakiwa wameingia Kiev na wakawashinda tena kwa kishindo halaf ndo eti sasa wawaogope hao wa reserve ambao wengi wao sio full trained na hawana uzoef wa kutosha yaan jeshi la ukraine liogope jeshi la akiba? na mpaka urusi inatumia reserve ni kumaanisha urusi ana hali tete kwenye uwanja wa vita.
kwa hiyo ina maana Mauripol, Luhansk, Donesk na Kherson mmezirudisha ukraine au ni kwamba mnajitekenya wenyewe
 
Wanajeshi wa Ukraine walikabiliana na majeshi ya Urusi tena wale wenye mafunzo kamili na uzoefu wa vita wakiwa na vifaa tele vya kijeshi tena wakiwa wameingia Kiev na wakawashinda tena kwa kishindo halaf ndo eti sasa wawaogope hao wa reserve ambao wengi wao sio full trained na hawana uzoef wa kutosha yaan jeshi la ukraine liogope jeshi la akiba? na mpaka urusi inatumia reserve ni kumaanisha urusi ana hali tete kwenye uwanja wa vita.
Haha wenye.mafunzo kamili sio wafungwa tena?? Mbona jamaa zenu wanalia mrusi kutumia wafungwa na majeshi ya kukodi
.....taarifa zenu wenyewe mnajipiga OG
 
Nchi hii inawajinga wengi watu walikabiliana na makimandoo wenye moral waje wawaogope hao ambao wanamda mrefu walikua sio active
Labda mori za kimasai.....jimbo lipi limerudi zaidi ya hivyo vijiji mrusi alivyoona hana haja ya kupigania sana,,,rudisheni hicho kipande kinachomegwa
 
Yani hata kama wewe ni mwanajeshi wa Ukraine alafu unasikia adui anaongeza zaidi ya wanajeshi laki 3,uwezi ukawa na furaha maana unajua kabisa mpaka hao mia 3 waishe sizani kama utakuwa bado duniani
Wa Ukraine wameamua iwe kwa kifo ama uhai watailinda na kukomboa ardhi yao, Warusi hawa cause of war ni tamaa ya mlafi Vlad imewafikisha hapo.
 
Wa Ukraine wameamua iwe kwa kifo ama uhai watailinda na kukomboa ardhi yao, Warusi hawa cause of war ni tamaa ya mlafi Vlad imewafikisha hapo.
Lazima watu waheshimiane enzi za ubabe wa kiboya wa ma LGBT upo mwishoni
 
Labda mori za kimasai.....jimbo lipi limerudi zaidi ya hivyo vijiji mrusi alivyoona hana haja ya kupigania sana,,,rudisheni hicho kipande kinachomegwa
Kharkiv ni Jiji la pili kwa ukubwa baada ya Kiev na Ukraine wamelikomboa kutoka Russia nakushangaa sana unaposema ni kijiji
 
Back
Top Bottom