Wang Shu
JF-Expert Member
- Feb 1, 2014
- 2,562
- 3,715
Watu wa pwani hii kitu tunapendaga sana mapishi pia hutofautiana leo nenda fresh food nunua pweza alafu pika kama hivi hutojutia..
MAHITAJI
Pweza - 1 Kilo
Mafuta - ½ kikombe
Chumvi - 1 kijiko cha chai
Tangawizi mbichi iliyosagwa - 1 kijiko cha chai
Kitunguu saumu (thomu/galic) iliyosagwa - 1 kijiko cha chai
Masala ukipenda - 1 kijiko cha supu
Namna ya kutayarisha na kupika
Kidokezo: Unaweza kumwagia masala kiasi baada ya kukaanga kama picha inavyo onyesha.
MAHITAJI
Pweza - 1 Kilo
Mafuta - ½ kikombe
Chumvi - 1 kijiko cha chai
Tangawizi mbichi iliyosagwa - 1 kijiko cha chai
Kitunguu saumu (thomu/galic) iliyosagwa - 1 kijiko cha chai
Masala ukipenda - 1 kijiko cha supu
Namna ya kutayarisha na kupika
- Osha pweza kisha mkatekate
- Mtie viungo vyote ulotayarisha na chumvi
- Muache nusu saaa akolee viungo
- Mtie ndani ya sufuria bila maji mfunike kisha weka jikoni, atatumbuka maji mwenyewe kwa moto wa kiasi paka awe rangi ya damu yam zee (maroon)
- Akishawiva kwa rangi hiyo basi sasa mwaga maji yote,chukua pweza pekee weka kwenye bakuli au sahani
- Weka karai au kikaango (frying pan) motoni tia mafuta acha kwa muda wa dakika tano hivi mafuta yapate moto.
- Mimina pweza kwenye karai aacha wakaangike paka wabadilike ukiwageuza geuza kila baada ya muda wa dakika kumi hivi. Pweza tayari kwa kuliwa kwa ugali au muhogo