Pweza wa kukaanga

Pweza wa kukaanga

Wang Shu

JF-Expert Member
Joined
Feb 1, 2014
Posts
2,562
Reaction score
3,715
Watu wa pwani hii kitu tunapendaga sana mapishi pia hutofautiana leo nenda fresh food nunua pweza alafu pika kama hivi hutojutia..

MAHITAJI

Pweza - 1 Kilo

Mafuta - ½ kikombe

Chumvi - 1 kijiko cha chai

Tangawizi mbichi iliyosagwa - 1 kijiko cha chai

Kitunguu saumu (thomu/galic) iliyosagwa - 1 kijiko cha chai

Masala ukipenda - 1 kijiko cha supu

Namna ya kutayarisha na kupika
  1. Osha pweza kisha mkatekate
  2. Mtie viungo vyote ulotayarisha na chumvi
  3. Muache nusu saaa akolee viungo
  4. Mtie ndani ya sufuria bila maji mfunike kisha weka jikoni, atatumbuka maji mwenyewe kwa moto wa kiasi paka awe rangi ya damu yam zee (maroon)
  5. Akishawiva kwa rangi hiyo basi sasa mwaga maji yote,chukua pweza pekee weka kwenye bakuli au sahani
  6. Weka karai au kikaango (frying pan) motoni tia mafuta acha kwa muda wa dakika tano hivi mafuta yapate moto.
  7. Mimina pweza kwenye karai aacha wakaangike paka wabadilike ukiwageuza geuza kila baada ya muda wa dakika kumi hivi. Pweza tayari kwa kuliwa kwa ugali au muhogo
Pweza Wa Kukaanga.jpg
Kidokezo: Unaweza kumwagia masala kiasi baada ya kukaanga kama picha inavyo onyesha.
 
Ahsanteee, napenda sana Pweza,
Ila naona wale wa mtaani watamu zaidi wa kuchoma kwa vijiti, lol

(Kuna jamaa yangu mitaa ya Mwenge pale sijui bado yupo pweza wa vijiti na kachori, [emoji39])
 
Ahsanteee, napenda sana Pweza,
Ila naona wale wa mtaani watamu zaidi wa kuchoma kwa vijiti, lol

(Kuna jamaa yangu mitaa ya Mwenge pale sijui bado yupo pweza wa vijiti na kachori, [emoji39])
Ni kweli mkuu wale wa mtaani ni watamu sana inabidi niwachunguze nijue wanawaanda namna gani
 
Back
Top Bottom