Qalibaf: Mataifa ya Kiislamu yasimamishe mashambulizi ya Wazayuni

Qalibaf: Mataifa ya Kiislamu yasimamishe mashambulizi ya Wazayuni

Malaria 2

JF-Expert Member
Joined
Oct 17, 2023
Posts
6,846
Reaction score
10,288

Nov 08, 2023 03:33 UTC

  • Qalibaf: Mataifa ya Kiislamu yasimamishe mashambulizi ya Wazayuni
Spika wa Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu (Bunge la Iran) amelaani vikali mashambulizi ya kinyama utawala wa Kizayuni huko Gaza na kusisitiza kuwa, mataifa ya Kiislamu yana wajibu wa kusimamisha dhulma na hujuma hizo za kikatili za Wazayuni dhidi ya Wapalestina wa Ukanda wa Gaza.

Muhammad Bagheri Qalibaf, Spika wa Bunge la Iran alisema hayo jana katika mazungumzo yake ya simu na mwenzake wa Algeria, Ibrahim Boughali, ambapo wamejadiliana kuhusu matukio yanayoendelea Gaza.
Qalibaf amebainisha kuwa, nchi za Kiislamu zinapasa kuchukua hatua za dharura za kukomesha jinai za kutisha zinazoendelea kufanywa na utawala wa Kizayuni dhidi ya Wapalestina wasio na hatia wa Gaza.

Amesema wahanga wakuu wa mashambulizi ya kinyama ya utawala wa Kizayuni katika eneo hilo lililozingirwa huko Palestina inayokaliwa kwa mabavu ni watoto wadogo na wanawake.

Spika wa Bunge la Iran ameashiria nafasi ya makundi ya muqawama katika kukabiliana na chokochoko za Wazayuni na kueleza kwa: Nguvu ya harakati ya muqawama imeulazimisha utawala huo kutoa majibu ya woga.

Amesema utawala wa Kizayuni umegeuka na kuwa chombo cha mauaji kisichodhibitiwa na kilichopindukia kwa kufanya uhalifu kupitia kupuuza na kukiuka sheria zote za kimataifa.
 
tarumbeta na vinubi vinazidi kupigwa pale kati kati mwa gazaa....ishara kuwa lile eneo linatawazwaa...
FB_IMG_1699422655405.jpg
 
Kwa hiyo sheria za kimataifa zinahalalisha magaidi kuwaua waisraeli na waisrael hawapaswi kufanya chochote.....!?!?! Israel wana haki ya kujibu ugaidi unaofanywa na kikundi cha kigaidi cha Hamas dhidi yao.
 
Back
Top Bottom