QUEEN MONICA: Story yenye mambo ya kijasusi ndani yake

Dah monica arudi bongo tuu tushammisi kwanza kashagawa KOJOLEO huko daah imeumaa
 
Amepata tatizo kidogo, yupo kwenye harakati za kurekebisha, akifanikisha tu anashusha mambo. Tuwe na subira.
 
Laptop yake imeleta shida kidogo, ndio anarekebisha, ikikaa poa anashusha ma-episode ya kutosha. Keep your eyes open!!
mambo yamekaa sawamkuu now ngoja nijitahidi kutupia za kulalia maana kesho mchaka mchaka unaanza tunaweza tukapoteana
 
SEHEMU YA 91


wengine sita wakaelekea meza kuu.Kabla
ya kikao kuanza yakafanyika maombi
halafu wimbo wa maalum wa kumtukuza
Alberto mkuu ukaimbwa huku ubani
ukifukizwa na baada ya hapo kikao
kikaanza.
“ Ndugu wajumbe ,tumekutana hapa
kwa dharura ili tujadili kile ambacho
kimetokea leo.Kilichotokea leo ni anguko
kubwa ambalo halijawahi kutokea tangu
Alberto mkuu wa kwanza .Mtu ambaye
tulimuamini
kwamba
angeweza
kutuvusha hapa Tanzania ,ametugeuka na
kufanya jambo ambalo hakuna
aliyetarajia.Nafikiri nyote mnafahamu
ugumu tulioupata kuingia hapa
Tanzania.Toka historia ya kuanzishwa
jumuia hii ya Alberto’s hakujawahi kuwa
na nchi ngumu kuingia kama Tanzania.Hii
inatokana na waasisi wa taifa hili kujenga
misingi imara na thabiti na hivyo
kulifanya taifa hili kutopenyeka
kirahisi.Ilitulazimu kutumia nguvu nyingi
na muda mrefu kupenya na kuotesha
mizizi hapa Tanzania.Mizizi imeota na
mmea umechipua na mti umemea na
kutoa maua yenye harufu nzuri lakini
wakati unakaribia kuanza kutoa matunda
ametokea
mwenzetu
mmoja
akaukata.Tulimuamini sana Ernest Mkasa
tukamuweka katika nafasi ya juu kabisa
lakini baada ya kufanikisha yale
aliyokuwa anayahitaji amechagua
kutusaliti.Ndugu zangu kufutwa kwa
muswada huu na kuvunjwa kwa baraza la
mawaziri ni pigo kubwa kwetu.Muswada
huu ulikuwa ni mwanzo wa kuipeleka
Tanzania kule tunakotaka na kufutwa
kwake kumetufanya turudi nyuma hatua
ishirini zaidi.Hili ni anguko kubwa ndugu
zangu na si suala la kupuuzia.Ofisi ya rais
ndiyo mzizi wetu mkuu kwa hiyo kama
tukiikosa ofisi ile hata sisi hatutakuwa na
nguvu tena na mambo yetu
yatakwama.Kwingineko kote duniani
ambako Jumuiya ya Alberto imeweka
mizizi yake marais wa nchi ndio wenyeviti
wa kamati kuu za Alberto za kila nchi
lakini hapa Tanzania ilikuwa tofauti
kidogo ,tulimpa urais mtu ambaye si
Alberto’s japokuwa ni kwa makubaliano
maalum lakini nataka nikiri kuwa
tulifanya kosa kubwa.tulitakiwa kuchagua
rais kutoka miongoni mwetu.Kosa
tulilolifaya sasa linatugharimu.Kwa hiyo
ndugu zangu tumekutana hapa kwa ajili ya
kulijadili suala hili.Nakaribisha sasa
maoni yenu lakini kabla ya yote napenda
kwanza nimpe nafasi ya kwanza
mwenzetu waziri mkuu mstaafu”akasema
Obi.Waziri mkuu aliyevuliwa madaraka
akasimama
“ Ndugu zangu sidhani kama kuna
haja ya kuendelea kulijadili suala hili
wakati kinachotakiwa kifanyike kiko
wazi.Ernest mkasa ametusaliti na kwa
mujibu wa sheria zetu yeyote
anayetusaliti au kushindwa kutimiza
wajibu wake na kuhatarisha maslahi ya
jumuia adhabu yake ni kifo.Rais
Ferdinand alikufa kwa kukataa
kushirikiana nasi na hivyo ndivyo
tunatakiwa kufanya kwa Ernest Mkasa.He
must die.Kama alivyosema mwenyekiti
kwamba ofisi ya rais ndiyo mzizi wetu
mkuu na hatutakiwi kuikosa basi
tumuondoe Ernest haraka ,tunaye Mr
Muhsini ambaye ni makamu wa rais
atashika usukani kwa muda na mambo
yetu yataendelea kama kawaida.Baadae
utafanyika uchaguzi na mtu wetu
 
SEHEMU YA 92



mwingine ashike nafasi hiyo ili mipango
yetu iendelee.Hatutaweza kufanya
chochote bila kuwa na mtu wetu ambaye
ni rais wa nchi.Kwa hiyo ndugu wajumbe
pendekezo langu mimi ni kwamba hakuna
chochote tunachoweza kukifanya kama
hatutaitwaa tena ofisi ya rais.Tusipoteze
muda mwingi kujadili jambo hili wakati
suluhu ya jambo hili ni moja tu” akasema
waziri mkuu aliyevuliwa wadhifa.Kabla
mjumbe mwingine hajasimama Agatha
mke wa Ernest Mkasa akasimama
“ Ndugu mwenyekiti naungana na
mjumbe aliyetangulia kwamba sheria zetu
zinasema hivyo lakini suala hili si dogo
kama tunavyodhani.Ernest ni mume
wangu na ninamfahamu vizuri ,lazima
kuna watu waliompa nguvu ya kuweza
kufanya haya aliyoyafanya.Peke yake
naamini hawezi kuyafanya haya.Kwa hiyo
basi tusiwe na haraka ya kutaka
kumuua,tufanye kwanza uchunguzi wa
kina tufahamu anashirikiana na akina
nani .Kwa kulipanua zaidi suala hili ni
kwamba kwa siku za hivi karibuni
niligundua mabadiliko Fulani kwa Ernest
.Niliamini lazima kuna jambo
linalomsumbua.Siku ya jana asubuhi
alipigiwa simu na mtu wakazungumza
kuhusu
kufanyika
kwa
makabidhiano.Nilimchunguza
mtu
aliyeongea naye na kugundua ni balozi wa
China hapa nchini.Niliwasiliana na
makamu wa rais nikamtaka achunguze
nini kinaendelea kati ya Ernest na balozi
wa China lakini hakuweza kupata
chochote.Ninaamini kabisa kuna jambo
linaloendelea kati yao na ndiyo maana
nikasema kwamba tufanye uchunguzi wa
kina kwani endapo tutamuondoa Ernest
peke yake na kuwaacha watu
anaoshirikiana nao bado hatutakuwa
tumefanya kitu .Hatufahamu watu
anaoshirikiana nao wanatufahamu kiasi
gani kwa hiyo tulipe suala hili uzito
unaostahili.Inawezekana
tayari
wanaufahamu mtandao wetu kiundani na
ndiyo maana Ernest amekuwa na nguvu
kubwa na haogopi.Tunapaswa kuwa
waangalifu sana.Kwa ushauri kuna mtu
mmoja ni msaidzi wa karibu sana wa rais
anaitwa Mukasha huyu ndiye ambaye
amekuwa akimshirikisha katika mambo
yake mengi .Tuanze kwa kumchunguza
kwanza huyu kuna kitu atakuwa
anakifahamu.Huyu ndiye aliyebeba siri
zote za Ernest” akasema Agatha
“ Agatha wazo lako ni zuri na hata
mimi nakubaliana nalo lakini tunapaswa
kutafuta njia ya haraka ya kuhakikisha
tunaurejesha bungeni muswada ule
muhimu.Nahitaji mawazo zaidi” akasema
Obi mwenyekiti wa kikao kile
“ Mimi kwa maoni yangu endapo
suala la kumuua Ernest litakuwa gumu
basi
tuwatumie
wabunge
kumuondoa.Asilimia karibu sabini ya
wabunge ni watu wetu.Tumegharamia
kampeni zao wakashinda na kila mwezi
wanapokea fedha nyingi kutoka kwetu
kwa hiyo tuwatumie hawa kuanzisha
mchakato wa kura ya kutokuwa na imani
na rais.Kwa kuwa tuna idadi kubwa ya
wabunge walio wafuasi wetu basi
itakapigwa hiyo kura lazima tutaibuka na
ushindi.Kwa kutumia njia hiyo tunaweza
kumuondoa rais madarakani kwa haraka
wakati tukiendelea kufanya uchunguzi
kuwabaini watu anaoshirikiana nao huku
mambo yetu yakienda kama kawaida”
akasema mmoja wa wajumbe
Hilo nalo ni wazo zuri mno.Nitakaa
na kamati ya uongozi tutalijadili hilo pia
na kwa kuwa tunao mabingwa wa sheria
tutawashirikisha na watatushauri nini cha
kufanya kwani jambo hili ni la kisheria
zaidi” akasema mwenyekiti
Kilikuwa ni kikao kirefu ,mawazo
mengi yakatolewa na kujadiliwa na hadi
mwisho wakaafikia mambo kadhaa
wanayotakiwa kuyafanya na kikao
kikafungwa
 
mambo yamekaa sawamkuu now ngoja nijitahidi kutupia za kulalia maana kesho mchaka mchaka unaanza tunaweza tukapoteana
Aseeeee mi zangu nakuvizia tuuu
Tatizo unaahidi saa hizi unaleta saa nane[emoji134] [emoji134]
 
SEHEMU YA 93



yari ni saa tisa za usiku kwa saa za
Dubai ambayo ni sawa na saa nane kwa
saa za afrika mashariki ,katika chumba
kimoja ndani ya hoteli kubwa ya kifahari
msichana mmoja mrembo Maria alikuwa
amejilaza kitandani akiwa na kompyuta
yake ndogo.Mawazo mengi yalimsumbua
“ Ni usiku mwingi sasa ,Austin
hajapiga simu na mtandaoni
hapatikani.What happened ? Kwa nini
hajanipigia simu? Hii si kawaida
yake.Hawezi kupitisha siku bila ya
kuwasiliana nami.Amepatwa na tatizo
gani? Au ni janja yake ya kutotaka
mawasiliano nami kwa vile nilimwambia
nataka kwenda Dar es salaam? Ninahisi
bado hataki niende Tanzania kwa sababu
hakuonyesha kupendezwa na wazo
hilo.Kuna kitu gani anakificha? Ana
mwanamke mwingine Dar es salaam na
hataki nijue? Akajiuliza Maria akainuka na
kuketi.
“ Sitaki kuwaza mambo hayo ya
Austin kuwa na mwanamke mwingine
kwani sijui nini kitatokea kwa namna
ninavyompenda .Sijawashi kumpenda
mwanaume
kama
nimpendavyo
Austin.Niliapa kufanya jambo lolote kwa
ajili yake kwa hiyo lazima niende Dar
.Lazima
nijue
maendeleo
yake.Sintomweleza kama ninakwenda
lakini atashangaa niko Dar es
salaam.Anasema kuna hatari , mimi
siogopi hatari yoyote.Ngoja niwasiliane
kwanza na baba nimtaarifu kuwa kesho
ninakwenda Dar es salaam na yeye ndiye
atakayenipa maelekezo ya mahala
ninakoweza kumpata Austin” akawaza
Maria akazitafuta namba za simu za hoteli
aliyofikia baba yake akapiga.
“ hallow “ ikasema sauti ya upande
wa pili ambayo Maria akaitambua ilikuwa
ya baba yake.
“ Hallow baba.It’s me Maria”
“Hello Maria hujalala bado? Najua ni
usiku mwingi hapo Dubai “
“ Ndiyo baba ni saa tisa za usiku hapa
Dubai.Nimekosa kabisa usingizi”
“ Oh my princess pole sana”
“ Ahsante baba” akasema Winnie
halafu ukimya mfupi ukapita
“ Baba nimekupigia kukutaarifu
kuwa baada ya kumaliza majukumu yangu
hapa Dubai kesho ninakwenda Dar es
salaam.Nataka unielekeze mahala
nitakapomuona Austin”
“Unakwenda Dar es salaam?
Akauliza Boaz
“Ndiyo baba nakwenda Dar es
salaam kesho kuonana na Austin”
“Austin
anafahamu
kuwa
unakwenda huko ?
“Ndiyo anafahamu ila sijamueleza
lini ninakwenda.I want to surprise him”
akasema Maria.Boaz akafikiri kidogo na
kusema
“Maria mimi pia nimepata dharura
nahitajika Dar es salaam mara moja kwa
hiyo kesho nitaondoka hapa Comoro
kuelekea huko.Tutakutana Dar es salaam
na halafu tutaonana na Austin “
“Ahsante baba tutaonana hiyo
kesho” akasema Maria na kukata simu
“Huu ndio wakati niliopanga Austin
aanze kunifanyia kazi zangu.Nilimuokoa
toka mikono ya Alshabaab nikamtunza na
kwa kujua thamani yake na nilijua iko siku
atanisaidia na wakati wenyewe ni sasa
 
SEHEMU YA 94


gatha aliwasili katika makazi yao
akitokea katika kikao na kuelekea moja
kwa moja chumbani .Tayari Ernest Mkasa
alikwisha rejea muda mrefu alikuwa
kitandani amejilaza akitafakari.Hakuwa
na usingizi kutokana na mawazo
mengi.Mara tu mke wake alipoingia
chumbani
akainuka
na
kukaa,wakatazamana kwa sekunde
kadhaa halafu Ernest akasema
“ Leo ni siku ya mwisho kurejea hapa
nyumbani mida kama hiyo.Nitatoa amri
ukichelewa kurudi zaidi ya saa tatu usiku
usiruhusiwe kuingia na urudi ulikotoka”
akasema Ernest kwa ukali
“ Usinitishe Ernest ,si wewe au mtu
yeyote anayeweza kunizuia nisiingie
humu ndani muda wowote nitakao”
akasema Agatha naye kwa ukali
“ Tambo hizo zilikuwa zamani na
kuanzia sasa utafuata amri zangu na kama
utashindwa kufuata kile ninachokiamuru
basi mlango uko wazi unaweza kuondoka
zako lakini kama unataka kuendelea
kuishi humu ndani utafuata sheria na
taratibu na kwa hapa ikulu mimi ndiye
mwenye kauli ya mwisho ninachokiamuru
lazima kitekelezwe!!!
Agatha akamtazama mumewe kwa
hasira na kusema
“ You are doing a very big mistake
Ernest.You don’t know what you’ve done”
akasema Agatha
“ I know what I’m doing tena
ninajilaumu kwani haya niliyoyafanya
nimechelewa sana.Sikutakiwa kuwaacha
wewe na hao wenzako mkaitawala nchi
hii.Hilo ni kosa ambalo nitalijutia katika
maisha yangu yote hadi siku naingia
kaburini”
“ I trusted you Ernest.Sikutegemea
kama siku moja ungeweza kutusaliti kiasi
hiki.Uliaminiwa ukapewa nafasi ya urais
lakini umechagua kutugeuka .Kwa hiki
ulichokifanya umetengeneza uadui
mkubwa kati yetu nawe na unafahamu
utaratibu wetu kwa wale wanaotusaliti”
“ Naomba kwanza nikuweke wazi
kwamba sikuwahi kufikiria wala sikutaka
kuwa rais.Mlinilazimisha nishike nafasi hii
kwa maslahi yenu.Ulikubali kuwatoa
kafara
wanao
wa
kuwazaa
mwenyewe.Jambo hilo linaniuma sana na
leo nataka nikuweke wazi kwamba
ninajua kukutana na mwanamke kama
wewe.Kila usiku ninasikia sauti za
wanangu uliowatoa kwa huyo shetani
wako unayemuabudu.I swear I’ll never
forgive you for that.Wewe na wenzako
mliwaua wanangu ili kunishinikiza
nikubali kuwa rais.Nilikubali wakati ule
kwa kuwa nilikuwa na woga wa kufa lakini
 
SEHEMU YA 95


kwa sasa siogopi tena.Hata leo mkitaka
kuniua fanyeni hivyo lakini mkae mkijua
kwamba wakati wenu umefika na hamna
nafasi tena ya kufanya ushenzi wenu hapa
Tanzania.Kuanzia sasa mimi na wewe ni
maadui na hautalala tena katika chumba
hiki.Tayari kuna chumba kingine
kimeandaliwa kwa ajili yako.Kwa ufupi tu
ni kwamba me and you we’re over.We’re
finished.Hakujawahi kuwa na mapenzi
kati yetu,its all lies.One more thing kwa
kukutunzia heshima yako nitakuacha
uendelee kuishi hapa ikulu lakini baada tu
ya kumaliza kipindi changu kila mmoja
ataenda kuishi maisha yake.Nadhani
umenielewa vizuri” akasema Ernest kwa
ukali
“ Ernest unajidanganya kwa
kujifanya malaika wakati we’re both
devils.Ulikunywa kikombe cha damu ya
mwanadamu na kwa kitendo kile
ulibatizwa kuwa mfuasi wetu kwa hiyo
basi usijidanganye kuwa unaweza
kupambana nasi.Wewe bado mdogo sana
na utapeperushwa kama tiara
inavyopeperushwa na upepo.Kufumba na
kufumbua utapotea kama matone ya mvua
yanavyopotea ardhini .Nakushauri Ernest
muda bado unao jirudi ,utubu na
utasamehewa.Bila kufanya hivyo
sintakuwa na namna nyingine ya
kukusadia.Mimi pekee ndiye mwokozi
wako.Kwa taarifa yako nimetoka katika
kikao cha kujadili hiki ulichokifanya na
wajumbe waliamua uuawe kama sheria
zinavyosema lakini mimi nikasimama na
kukutetetea kwa hiyo bado unao muda
Ernest jirudi”
“ You are Idiot!!! Akasema Ernest
“ Mwokozi wangu ni Yesu pekee
ambaye alitufia msalabani.Nakubali
nimemkosea sana lakini nimeamua
kujirudi kwake na kumkiri kuwa ndiye
bwana na mwokozi wa maisha yangu na
nitamtumikia yeye peke yake.Naomba
utoke chumbani kwangu haraka sana!!
Akafoka Ernest na kumshika Agatha
mkono akamtoa mle chumbani
akampeleka katika chumba kingine
“ Nani kambadilisha Ernest namna
hii? Katoa wapi ujasiri huu? Anajiamini na
haogopi chochote.” akawaza Agatha baada
ya
kuingia
katika
chumba
alimohamishiwa.Mara akakumbuka kitu
na kuinamisha kichwa
“ Ernest amenikubumbusha kuhusu
watoto wangu na kwa mara ya kwanza
baada ya miaka kupita ninahisi kuumizwa
na jambo nililolifanya” akafuta machozi
“ Lakini sipaswi kujilaumu kwa hiki
nilichokifanya .Nilifanya vile kwa ajili ya
nchi hii.Tanzania lazima ibadilike.kwa ajili
ya wanangu ambao ni mashujaa wa
mabadiliko
hayo
sintorudi
nyuma.Nitaendelea kupigania mabadiliko
hadi nihakikishe Tanzania imebadilika.”
Akawaza Agatha.
Agatha alipotoka mle chumbani
Ernest akapanda tena kitandani
“ Agatha ni adui yangu mkubwa.Yeye
ndiye aliyenifanya nikubaliane na
mashetani wenzake.Najua Alberto’s
watamtumia sana Agatha ili kukabiliana
nami lakini hawataweza kwani
nitahakikisha ninakuwa mbali naye na
njia pekee ya kujiweka mbali naye ni
kukata kabisa mawasiliano.Hakuna
kinachotuunganisha tena ,kilichobaki ni
ndoa iliyoko katika makaratasi.” Akawaza
Ernest akamkumbuka Monica na
kutabasamu
“Toka Janet aliponieleza kuwa
Monica ni mwanangu nimekuwa na hisia
kubwa kuwa jambo hili ni la kweli.Endapo
vipimo vitaonyesha kweli Monica ni
mwanangu nitatumia gharama zozote
kumlinda.” akawaza Ernest na kujilaza
kitandani
“ Siku ya kwanza ya mapambano
imekwisha ngoja nilale nisubiri siku ya
kesho.” Akawaza Ernest na kuanza
kuutafuta usingizi
 
SEHEMU YA 96



KINSHASA – DRC
Miale ya jua ilipenya dirishani na
kukifanya chumba kiwe na nuru ya
kuvutia asubuhi hii.Monica alifumbua
macho na kujikuta akitazamana na sura
yenye tabasamu ya David Zumo
“ Hallow malaika wangu” akasema
David huku akitabasamu
“ hallow David,umeamkaje?
“ Nimeamka salama malaika
wangu.Usiku wako ulikuaje?
“ Nilikuwa na usiku mzuri sana
David” akajibu Monica.Bado David Zumo
aliendelea kumtazama
“ Mbona unanitazama hivyo David?
Akauliza Monica huku naye akitabasamu
“ Monica nashindwa nikueleze nini
mpenzi wangu kwa namna ulivyoyafanya
maisha
yangu
yakawa
na
furaha.Nakupenda mno Monica.Tafadhali
naomba usibadilishe mawazo ya kuolewa
na mimi ” Monica akatabasamu na kusema
“ Usiogope David siwezi kubadilisha
mawazo.Tayari nimekwisha fanya
maamuzi na kukubali kuolewa nawe kwa
hiyo mimi ni wako daima” akasema
Monica.David akambusu akamtazama kwa
makini na kusema
“ Monica naomba nikuulize kwa
mara nyingine tena .Japokuwa umekubali
kuolewa nami lakini je ndani ya moyo
wako ninayo nafasi au nitakuwa na nafasi?
Monica huku akikichezea kifua cha
David akasema
“ kama nilivyokujibu uliponiuliza
mara ya kwanza kwamba tulipe nafasi
suala hili kwani tumefahamiana ndani ya
kipindi kifupi na ndani ya muda huo mfupi
mambo makubwa yamefanyika.Nimefanya
mapenzi kwa mara ya kwanza,nimekubali
kuolewa nawe .Hiyo ni ishara tosha kuwa
unayo nafasi kwangu kwani kama
usingekuwa na nafasi nisingekubali
kuyafanya
hayo
mambo
makubwa.Japokuwa bado nafasi yenyewe
ni ndogo lakini kadiri tutakavyoendelea
ndivyo utakavyozidi kujijenga ndani ya
moyo wangu kwa hiyo basi usiwe na wasi
wasi”
“ Ahsante Monica kwa kuwa
muwazi.U mwanamke wa pekee
sana.Nakuahidi nitajitahidi kuwa
mwanaume bora kwako na siku zote uso
wako hautakauka tabasamu”
Monica akatabasamu na kumbusu
David
“ Una maneno matamu sana.Ahsante
kwa maneno hayo mazuri ambayo
naamini yametoka moyoni.Halafu David
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…