QUEEN MONICA: Story yenye mambo ya kijasusi ndani yake

QUEEN MONICA: Story yenye mambo ya kijasusi ndani yake

SEHEMU YA 62



DAR ES SALAAM – TANZANIA
Zaidi ya dakika nne sasa rais wa
jamhuri ya muungano wa Tanzania Ernest
Mkasa alikuwa amesimama katika dirisha
la chumba chake akitazama nje.Agatha
mke wake akamfuata taratibu
“ Ernest darling” akasema na
kumshika kiunoni.
“ Kuna jambo gani linakusumbua?
Nimekuona kwa siku mbili tatu
umebadilika sana na ninakufahamu vizuri
lazima kuna kitu kinakisumbua akili
yako.Niambie tafadhali kama kuna kitu
kinakuumiza kichwa .”
Ernest akageuka na kumtazama
mkewe akamshika mabegani na kusema
“ hakuna tatizo lolote Agatha,niko
kawaida.Kwa leo nina kikao cha dharura
cha baraza la mawaziri,kuna jambo la
dharura la kujadili ndiyo maana unaniona
katika hali hii.Kikao hakitakuwa chepesi”
akasema Ernest na mke wake akaonekana
kustuka
“ Kuna mambo gani ya dharura
mnakwenda kujadili katika kikao hicho?
Akauliza Agatha
“ Siwezi kukueleza kwa sasa hadi
hapo baadae” akasema Ernest na mke
wake akamtazama kwa macho
makali.Hakuonyesha kufurahishwa na
jibu lile
“ Ernest toka lini umeanza kunificha
mambo? Kila kinachoendelea katika ofisi
yako umekuwa unanitaarifu na kuniomba
ushauri lakini nashangazwa leo umeamua
kunificha mambo hayo ya dharura
mnayokwenda kuyajadili.Au umepata
mshauri mwingine unayemuamini zaidi
yangu? Akauliza Agatha
“
Agatha
si
hivyo
unavyodhani.Nitaongea nawe baadae kwa
kirefu lakini kwa sasa ngoja niwahi
ofisini” akasema Ernest na kuchukua
mkoba wake akatoka na kumuacha mke
wake akishangaa
“ This is strange!!.Whats going on?
Haijawahi kutokea hata mara moja Ernest
akagoma kunieleza jambo.Kabla ya kikao
chochote anachokwenda lazima mimi na
yeye tukae tujadili lakini leo amegoma
kabisa .Kuna kitu kinaendelea ambacho
nahitaji kukifahamu” akawaza Agatha na
kuchukua simu yake akazitafuta namba za
makamu wa rais akampigia.
“ hallo Madam first lady” akasema
Muhsin
“ Muhsin ,hukunipa mrejesho
wowote kuhusu lile jambo nililokuomba
ulifuatilie jana” akasema Agatha
“ Agatha sikuona sababu ya kukupa
mrejesho kwa sababu vijana niliowatuma
hawakuweza
kugundua
jambo
lolote.Katika ule muda uliosema kuna
makabidhiano yatafanyika,kuna gari
Waoo
 
Back
Top Bottom