Radio free afrika inatumia maneno visivyo

Radio free afrika inatumia maneno visivyo

mzeelapa

JF-Expert Member
Joined
Jul 14, 2010
Posts
1,118
Reaction score
404
Nimekuwa nikisikiliza kipindi cha RFA kinachozungumzia magazeti kila siku saa 12.30 asubuhi. Nimegundua watangazaji wanatumia neno lakini visivyo hasa kwa kuunganisha taarifa zisizofanana au kuhusiana. Nijuavyo mimi neno hilo hutumika kwa kutoa kasoro au kuunganisha habari zilizo sambamba. Isitoshe neno hilo linatumika saana au kurudiwa rudiwa mpaka inakera. Kituo hakina wasanifu wa lugha au ndio watangazaji makanjanja wasiojua lugha wameshawaingilia?
 
Baadhi ya watangazaji wa RFA hutangaza Star Tv pia. Kiswahili wanachotumia ni ovyo sana na si hilo neno la 'lakini ' tu, ila maneno mengi wanayatumia vibaya. Mojawapo ni 'kuweza'. Utasikia wanasema: 'Ndege ya ATCL iliweza kukwama kwenye uwanja wa ndege wa Mwanza'

Pia si hayo maneno tu ila uchanganyaji wa herufu 'l' na 'r' kiasi cha kuharibu majina ya watu na vitu kama Elasto Mbwilo badala ya Erasto Mbwillo (Mkuu wa mkoa, Manyara) Saida Kalori badala ya Saida Karoli(Mwanamuziki wa nyimbo za jadi)au marelia badala ya malaria, roli badala ya lori nk.

Eti wamesomea uandishi wa habari! Uandishi wa habari bila lugha?Kichefuchefu kitupu!
 
Back
Top Bottom