Radio Free Afrika watakiwa kujieleza kwanini wasiadhibiwe kwa kurusha kipindi cha 'Amka na BBC' bila mizania

Radio Free Afrika watakiwa kujieleza kwanini wasiadhibiwe kwa kurusha kipindi cha 'Amka na BBC' bila mizania

Replica

JF-Expert Member
Joined
Aug 28, 2017
Posts
1,681
Reaction score
8,887
TCRA imekituhumu kituo cha utangazaji cha RFA kukiuka kanuni na maadili ya utangazaji kupitia kipindi cha 'amka na BBC' kwa kurusha maudhui bila kuzingatia mizania ya habari walipokuwa wanamuhoji Makamu mwenyekiti wa CHADEMA, Tundu Lissu juu ya viongozi wa chama hicho kutoshiriki kutoa heshima za mwisho kwenye msiba wa hayati Benjamin Mkapa.

TCRA imesema mtangazaji wa kipindi aliruhusu kurushwa habari iliyoegemea upande mmoja kwa Lissu kutoa tuhuma na kulalamika kuwa serikali ilimnyima nafasi ya kutoa heshima za mwisho bila kumtafuta msemaji wa serikali ili aweze kutolea ufafanuzi tuhuma hizo.

RFA wanatuhumiwa kukiuka kanuni Na. 15(2)(b) na (c) na 16 za mawasiliano ya kielektroniki na Posta(Maudhui ya Utangazaji na Televisheni) 2018.

Saa 5 asubuhi ya tarehe 10 Agosti, 2020 itakuwa ukomo kwa uongozi wa RFA kufika ofisi za makao makuu ya TCRA zilizopo Dar es Salaam kutoa utetezi wao katika shauri dhidi yao wa kimaandishi na kufika mbele ya kamati kujieleza kwanini kituo chao kisichukuliwe hatua za kisheria kwa kukiuka kanuni za huduma ya utangazaji.

94F76062-E4FC-4298-9CA5-100D141A2318.jpeg

3F4B4B69-17DA-4945-8023-A04E43D24E34.jpeg

D2730A42-D96E-4A5D-B200-7018391A2325.jpeg



SHERIA INASEMAJE?

64C7AD56-20EE-4A44-BF1F-ACCC22AEB0CD.jpeg

3B455AC7-1D14-4797-AB2E-1CB6CCF9B163.jpeg
 
Awamu pekee ambayo watakaofurahia uongozi wake ni wale ambao wako karibu na mkulu/wateule kwa sababu na wao hawana namna zaidi ya kusifia, otherwise ni nchi inaendeshwa kipuuzi Sana sijapata kuona Tanzania.
 
Ina maana sasa hivi chombo chochote kikitaka kujiunga lazima waombe kibali hatari hii
 
Back
Top Bottom