Radio Free Afrika watakiwa kujieleza kwanini wasiadhibiwe kwa kurusha kipindi cha 'Amka na BBC' bila mizania

Radio Free Afrika watakiwa kujieleza kwanini wasiadhibiwe kwa kurusha kipindi cha 'Amka na BBC' bila mizania

1597057821544.png

1597057847281.png

1597057865966.png
 
Mkumbuke tu, vyombo vya habari hasa vya nje ya nchi ndio huwa chanzo cha machafuko na kutoweka kwa amani katika mataifa mengi duniani hasa Africa, hii ni hatua nzuri kudhibiti mitafaruku inayotarajiwa kutokea...

Na tunaomba serikali ifungie na mitandao ya kijamii hasa Facebook na Twitter.
 
Wapinzani fungueni online tv nje ya nchi. Waambie watu wa subscribe na kushare link. Kisha rusheni matangazo mubashara. Nunueni video camera, blackmagic atem hd na live U solo. Mfanye haraka kabla ya kampeni. Hakuna chombo chochote cha habari kitakacho waonesha.

Rekodini hotuba zenu kwa video na audio kisha tumeni nchi zima watu watapeana kwa memory card na bluetooth. Tcra hawawezi kupiga faini bluetooth na memory card.

Nisaidieni kushare na kuforward ujumbe huu kwa wahusika. Hata kwenye magroup ya whatsapp ya wahusika.
Wazo: Kutumia njia mbadala kufikisha ujumbe kwa wananchi

Zitto


Wapinzani muwe serious katika hili. Kulalamika mitandaoni hakutasaidia kitu chochote.
 
Hizi sheria alie zitunga Yesu amsamehe tu

Hilo ni fundisho la wanahabari, wakiwa darasani wanafundishwa jambo la mizania, lakini wakiwa mtaani wanaishi wapendavyo sasa bora kutumia sheria kuwafundisha hawa waandishi, viango vyao vya habali ahvitakuwa kimataifa.

Sidhani kama walishindwa kupata mawasiliano ya msemaji wa serikali.
 
Wapinzani fungueni online tv nje ya nchi. Waambie watu wa subscribe na kushare link. Kisha rusheni matangazo mubashara. Nunueni video camera, blackmagic atem hd na live U solo. Mfanye haraka kabla ya kampeni. Hakuna chombo chochote cha habari kitakacho waonesha.

Rekodini hotuba zenu kwa video na audio kisha tumeni nchi zima watu watapeana kwa memory card na bluetooth. Tcra hawawezi kupiga faini bluetooth na memory card.




Wapinzani muwe serious katika hili. Kulalamika mitandaoni hakutasaidia kitu chochote.
Wanayo pesa?
Utakuta hapo wanasubili beberu litume pesa za kampeni
Alafu wewe unaleta mambo ya tv?
Mwaka huu bila beberu mtakuwa tepe kama uji.
 
The Ofcom Broadcasting Code (with the Cross-promotion Code and the On Demand Programme Service Rules)

Watanzania watakwambia media zinaonewa wapitie hizo kanuni za regulator wa mabeberu ☝sheria zetu zina afadhali. Upuuzi BBC unaofanya africa awawezi thubutu kuufanyia kwao.

We ukimsikiliza mzungu kwenye kila kitu utaingia chaka huko kwao UK kwenye muungano wao wame devolve mambo kibao isipokuwa vitu vitano tu vya msingi moja kati ya ivyo ni BBC kwanini wanajua ni namna gani media inaweza tumiwa vibaya kuaribu nchi yao kwa iyo kama chombo cha propaganda za serikali kiko kwenye control ya central government.

Huku kwetu wanataka kila aina ya ujinga na upuuzi wananchi wasomeshwe na wasikilizishwe bila ya kujali midhani ya habari, mtu akitaka kusema uongo sawa na upuuzi wowote; serikali yoyote makini duniani aiwezi acha huo upuuzi ata wanaojiita liberal democracies media ni sehemu moja wasiyochekea mambo hatari yanayoweza wagawanya au hata kuwa sehemu ya kuchochea ujinga ndani ya jamii.
 
TCRA imekituhumu kituo cha utangazaji cha RFA kukiuka kanuni na maadili ya utangazaji kupitia kipindi cha 'amka na BBC' kwa kurusha maudhui bila kuzingatia mizania ya habari walipokuwa wanamuhoji Makamu mwenyekiti wa CHADEMA, Tundu Lissu juu ya viongozi wa chama hicho kutoshiriki kutoa heshima za mwisho kwenye msiba wa hayati Benjamin Mkapa.

TCRA imesema mtangazaji wa kipindi aliruhusu kurushwa habari iliyoegemea upande mmoja kwa Lissu kutoa tuhuma na kulalamika kuwa serikali ilimnyima nafasi ya kutoa heshima za mwisho bila kumtafuta msemaji wa serikali ili aweze kutolea ufafanuzi tuhuma hizo.

RFA wanatuhumiwa kukiuka kanuni Na. 15(2)(b) na (c) na 16 za mawasiliano ya kielektroniki na Posta(Maudhui ya Utangazaji na Televisheni) 2018.
Delete ccm Oct 28
 
Wanayo pesa?
Utakuta hapo wanasubili beberu litume pesa za kampeni
Alafu wewe unaleta mambo ya tv?
Mwaka huu bila beberu mtakuwa tepe kama uji.
Najua upo kazini. Lakini najua pia njaa haina chama. Kwa hiyo nina uhakika uchaguzi huwapi kura CCM. Ila usiwe na wasiwasi naogopa nisijekukuharibia kazi yako.

Nakutakia kazi njema ya kusifia.
Njaa haina chama.
 
Back
Top Bottom