Radio One Sterio, habari za Rais wa Zanzibar ni za Zanzibar

Radio One Sterio, habari za Rais wa Zanzibar ni za Zanzibar

Hismastersvoice

JF-Expert Member
Joined
Jan 26, 2013
Posts
21,741
Reaction score
26,735
Radio One Sterio mnapotusomea habari za rais wa Zanzibar haziwezi kuwa ni habari za kitaifa, hizo ni habari za taifa la Zanzibar lenye serikali yake na katiba yake.

Siku hizi kumezuka mtindo wa kuifanya serikali ya Zanzibar kuwa ni ya muungano! Na huu mtindo unafanywa na viongozi wa serikali ya muungano na kuifanya Zanzibar inaongozwa kwa pamoja na viongozi wa muungano, hii ni kinyume na katiba na wanafanya hivyo wakilenga uchaguzi mkuu. Kikatiba viongozi wa Zanzibar si viongozi wetu bara kwani hatujawachagua, hao ni wa wananchi wa Zanzibar na serikali yao ya Zanzibar, hivyo habari za serikali ya Zanzibar zitangazwe kuwa ni za Zanzibar na si za muungano.
 
Wana magazeti yao zanzibar leo na zanzibar mail, habari ni rais wa zanzibar tu kila siku ukurasa wa mbele mpaka inachosha kusoma habari za mwinyi tu, hata habari leo halifanyi hivyo kila siku front page ni samia tu kana kwamba hakuna habari nyingine ya kubeba gazeti
 
realMamy kuna ujumbe wako hu
Habari za Zanzibar ni za Kitaifa na Wala haziwezi kuwekwa kuwa za Kimataifa kwa sababu ukweli utabaki kuwa sisi tumeungana kuwa Taifa moja.

Tena ni habari kubwa kabisa kama inamhusu Rais wa Zanzibar.

Ikiwa ya kwanza ya Rais wa Jamhuri basi atafuata Rais wa Zanzibar ndipo habari nyingine zifuate.

Labda itokee vinginevyo.
 
Jana nilimsikia kiongozi wa juu bara akitoa maelekezo kuhusu shule za Zanzibar! Labda sheria za muungano imebadilishwa.
 
Habari za Zanzibar ni za Kitaifa na Wala haziwezi kuwekwa kuwa za Kimataifa kwa sababu ukweli utabaki kuwa sisi tumeungana kuwa Taifa moja.

Tena ni habari kubwa kabisa kama inamhusu Rais wa Zanzibar.

Ikiwa ya kwanza ya Rais wa Jamhuri basi atafuata Rais wa Zanzibar ndipo habari nyingine zifuate.

Labda itokee vinginevyo.
Siwezi kukukatalia, inawezekana uchaguzi mkuu wa jamuhuri ya muungano uliopita ulimpigia kura Mwinyi! Uchaguzi Tanzania lolote linawezekana.
 
Hata ITV na Azam huwa nawashangaa kuturushia hizo habari za Zanzibar
 
Back
Top Bottom