Capt Tamar, MUNGU (NIPO AMBAYE NIPO) wala hajashindwa maana yeye ni MUNGU wa kutimiza ahadi (COVENANT GOD), duniani ni himaya ya shetani aliyetupwa na MUNGU mwenyewe kwa kumkosea ndiyo maana hayo yote uliyoyaorodhesha yanafanyika duniani. Pia kumbuka MUNGU ni mwazilishi wa demokrasia, amekuwekea dhamira moyoni umchague YEYE au shetani.
Kwa hiyo kuwa fisadi, muuaji, mbinafsi ni chaguo la mtu kutoka moyoni mwake. MUNGU hajashindwa ila yale yaliyonenwa yanaachwa yatimie. Kama angeshindwa basi watu wote duniani tungekuwa tumeshakufa maana jukumu kuu la shetani ni kuangamiza.
Tena MUNGU aalivyokuwa wa huruma amekusikia ulichosema ila amekusamehe na unaendelea Kutumia jua lake, hewa yake na kuna siku utakiri MUNGU HAJASHINDWA.