Kama ndoa ya kiislamu ipo, aliyeifungisha anatakiwa awe na kibali cha registrar of marriage kinachomtambua kufanya kazi hiyo, kama ni sheikh, na hupewa mamlaka ya kutoa cheti cha ndoa kwa wahusika, ndoa hii haivunjwi kienyeji tu kwa maamuzi ya mtu mmoja kuamua kuachana, lazima ipite katika bodi ya usuluhishi ya ndoa, possibly !BAKWATA, suluhu ikikosekana, bodi ya usuluhishi hutoa cheti kinachoonyesha kwamba suluhu imeshindikana, then suala hupelekwa mahakamani.Itambulike kwamba ni mahakama pekee ndio yenye mamlaka ya kutoa talaka, haya mambo ya talaka rejea au talaka tatu kwenye sheria sijayaona. Kwa upande wa talaka, kabla haijatolewa, mahakama lazima ijiridhishe kwamba ndoa hairekebishiki(irreparably broken down). Na katika kutoa talaka mahakama imeweka vigezo mbalimbali kama uzinzi, ukatili, kutelekezwa e.t.c, kama nilvyosema awali ndugu hapo juu hajatenda kosa litakaloleta talaka, bali ni mke ndie katenda, bwana anaweza kudai fidia kutokana na uzinzi au kuomba talaka. I beg to end here