rafiki yangu anaomba msaada wa kisheria

wakuu ndoa ilikuepo ya kiislam tatizo ilikua mwanaume hajafika kwa wakwe na mahari alikua hajalipa
kama ndoa ilikuwepo ya kiislam, walii gani aliyemtoa huyo binti?
 
Kama ndoa ya kiislamu ipo, aliyeifungisha anatakiwa awe na kibali cha registrar of marriage kinachomtambua kufanya kazi hiyo, kama ni sheikh, na hupewa mamlaka ya kutoa cheti cha ndoa kwa wahusika, ndoa hii haivunjwi kienyeji tu kwa maamuzi ya mtu mmoja kuamua kuachana, lazima ipite katika bodi ya usuluhishi ya ndoa, possibly !BAKWATA, suluhu ikikosekana, bodi ya usuluhishi hutoa cheti kinachoonyesha kwamba suluhu imeshindikana, then suala hupelekwa mahakamani.Itambulike kwamba ni mahakama pekee ndio yenye mamlaka ya kutoa talaka, haya mambo ya talaka rejea au talaka tatu kwenye sheria sijayaona. Kwa upande wa talaka, kabla haijatolewa, mahakama lazima ijiridhishe kwamba ndoa hairekebishiki(irreparably broken down). Na katika kutoa talaka mahakama imeweka vigezo mbalimbali kama uzinzi, ukatili, kutelekezwa e.t.c, kama nilvyosema awali ndugu hapo juu hajatenda kosa litakaloleta talaka, bali ni mke ndie katenda, bwana anaweza kudai fidia kutokana na uzinzi au kuomba talaka. I beg to end here
 
Asante wakuu mumetupa mwanga mkubwa katika sakata hili kwaniaba ya rafiki yangu napenda nitumie nafasi hii kuwashukuru na kuwaombea kwa mungu awape heri zaidi na mudumu ili muendelee kusaidia wanaodhulumiwa
 

naona lushoto kuna fanya kaz yake well done!! upo mama kilikuu
 
unaongea bila uhakika, hakuna registration talaka inatolewa kutoka wapi sasa...
 
mind you, definition ya ndoa haiongelei vyeti wala sherehe, ndoa ni muungano wa watu wawili, wa hiari, mengine ni umaliziaji wa taratibu ambao si wa lazima kwa mfano katika ndoa za kimila
ndoa ni muungano wa watu wa wili kiroho lakini ukija kidunia lazima registration iwepo ndipo itatambulika na sheria, ama la kama registration haipo na kuna mtu anataka kudhulumiwa mfano katika kugawana mirathi au mali basi presumption of marriage imewekwa na sheria kumuokoa. kama hakuna wa kudhulumiwa usijifariki kama hujafunga ndoa kuwa upo kwenye ndoa. mwenzio anaweza siku yeyote akapata mwingine akaoana naye kwa ndoa na wewe ukawa huna la kumfanya.amekuwahi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…