RAI - Nguvu ya Hoja?


Pundamilia07,

Asante sana.

Hakimu kunijua mimi kuwa ni mwizi hakumfanyi asisikilize ushahidi na utetezi. Kujua kuwa Rostam na Freeman wana fedha ya kutosha na wamiliki wa magazeti hakunifanyi mimi niache kusahau na kujadili matatizo ya mtanzania.

Asante tena
 

Sijakupata vizuri mkuu, hebu fafanua.
 
Sijakupata vizuri mkuu, hebu fafanua.

Kaka,

Tuwe Objective, tusitafute excuse za matatizo yetu au hali fulani ya mtu isikudrive kuamua tofauti na nia yako. Kumbuka tupo kwenye JF, JUKWAA SIASA NA SIO VINGINEVYO. Sidhani kama pesa ya Lowassa, Manji, Rostam, Ndesa, Freeman, Pundamilia, Dr. Slaa, Kichwangumu ni tatizo la mtanzania.

Labda tuangalie ni jinsi gani alizipata. ni halali au? Hapa ndio tunapigania kufuta ufisadi kwa njia yeyote kama walitumia kodi yetu na sie kama mtaji.

Kama wana common interest katika biashara hilo sio tatizo kuungana. Common interest is needed in this battle not individuals kama unavyotaka niamini. Kama pesa yake na biashara zake zinasaidia wafamilia yake sina tatizo na sio kusaidia au kukopesha CCM na CHADEMA based on personal interest. Huu ni utumwa mwingine tunatengeneza wa kushindwa kujitawala hata kimawazo kama akina Bibile

Hope umenipata
 

Hebu labda nijaribu kuuliza swali la moja kwa moja huenda tunaweza kuwa sawa na kwenda pamoja.

Je, unafahamu kuwa Freeman ndiye mmiliki wa Tanzania Daima?
 
Mkamap,

Hata Mengi alishasema kuwa wao wanatoa tu policy kwenye Kulikoni na Thisday na sio kuandika.

Kwi kwi kwi yaani wewe katika watu mashuhuri unaowaamini wakiongea Mengi ni mmojawapo? Mbona hakuna gazeti lake hata moja ambalo huwa linaandika skendo zake (Chukua mfano ile ya Mdogo wake na Waingereza)? Mbona thisday na kulikoni ndiyo yaliyoshikia bango issue ya Manji wakati ule wana ugomvi na Mengi? (hapa sina maana kwamba wasifichue ufisadi lakini ni kwanini washikie bango wale wagomvi wa Mengi tu?).

Ni ukweli usio kificho kuwa Media ya Tanzania inawatumikia hao mabwana zao (wamiliki wao). Nakwambia ukisoma gazeti kama kuna skendo ina mhusu RA, basi unasoma T/Daima kwanza halafu unaangalia Mtanzania/Rai wanamtetea vipi. Unaweza ukakuta kimya. Au wanaweza wakatoa mazuri peke yake. Hivyo hivyo kama kuna skendo ya Mbowe unaikuta kwenye Mtanzania/Rai, basi unaangalia T/Daima ili kuona wanamtetea vipi au wameandika mazuri gani. Hivyo media Tanzania haiko balanced kabisa. Ukisikia kuna skendo inamhusu mtu hasa hawa matajiri basi unaweza kabisa kubuni ni gazeti litakuwa limeandika hiyo story.

Kwa hiyo kujifanya kushangaa Rai wanapowashambulia T/Daima ni unafiki wa sisi wenyewe. Maana huo ndiyo umekuwa mtindo wa magazeti yetu au media zetu. Yaani inakera sana kwa sisi wasomaji au watazamaji. Unaona kabisa vyombo vya habari vimekuwa midomo ya wafanyabiashara/wanasiasa/wenye madaraka serikalini.
 

Mkodoleaji,

Hakika umekodoa hasa na kama Kichwangumu hajaelewa, basi aendelee kuuliza ili tumtoe gizani au asiendelee kusumbuka tena. What you narrated in your last posting is the hard fact.
 
mhariri wa TZ daima na balile wote ni makanjanja tu!Balile anawatumikia kina RA na kikosi chake na wa TZ daima anawatumikia kina Mbowe na kikosi chake!1+1=1
Wote wale wale!

Kwa Wakuu wote JF!

kinachonifurahisha mimi ni kuwa wote tunaelewa kusoma nyakati. hatupati shida kugundua ukweli wa mambo hata kama umefichwa.

big up wote wenye moyo wa dhati wa kulifikisha taifa hili teule la TZ ktk nchi ya "ahadi" tuliyoahidiwa na Mwalimu yenye maziwa na asali
 
Habari zinazoingia sasa hivi zinadokeza kuwa Mhariri wa gazeti la RAI Bw. Balile ameondolewa wadhifa wake huo. More to come!
 
Balile ni mtu wa ajabu sana alikuwa anakula pesa za membe at the same time HADEMA nako alikuwa anakula

says alot about the mans character

huyu ndiye balile:



nami nikamjibu balile hivi:


I really missed him kwa muda kwani hakurudi tena
 
Hii nayo ni "breaking news" kiaje?

Wanasema anaweza kurudishwa mara RA atakapojulishwa, wanasema huo ni uamuzi wa ndani ambao hauna baraka za RA. Wanasema hajang'olewa bali amewekwa pembeni kwa muda kabla ya kurudishwa.

Pamoja na hayo kama ndani ya jumba wanaweza kumuasi mwenye mali basi wajue zao zimekwisha na kwamba wakati wowote watakosa wa kuwafuata. Hii ni kama hadithi nyingi ambazo tunasimuliwa za HIMAYA INAYOANGUKA, maana hata ndani ya Jumba la Mfalme wataasi na ataangalia na kukosa pa kushika moto wa mapinduzi utakaposhika kasi.

MUNGU ENDELEA KUWALAANI NA KUWAANGAMIZA MAFISADI
 
Nilipokuwa napiga makelele juu ya hatma ya Balile na roho yake ya usaliti mlisema Lunyungu umezidi na majungu .Now here we are .Balile hana pa kwenda na mwisho umefika .Haya nilimtabiria long time ago hakuwa anaelewa nina kisema
 
vyanzo vya upande mwingine vinaonesha RA ametoa baraka zake; ila yawezekana tumeivujisha mapema wanaweza wakabadili maamuzi. Ile editorial yake ya juzi nadhani haikumfurahisha mtu yeyote ndani ya ofisi yake.

Tuangalie
 
Hizi ni issue za waandishi wa habari wenyewe, pelekeni kwenye jukwaa la wahariri mkajadili kwa mapana huko!!!
 

Bado sijaelewa umuhimu wa huyo Balile, na kwa nini kung'olewa kwake huko Rai kupewe uzito kiasi cha kuitwa "breaking news". I mean who is he to me and most of us? Isn't he just one of the many folks who get sacked for a variety of reasons, I mean why should this bother us? He got sacked, so what? Hii nayo ni breaking news?
 
Kithuku kuwa mtulivu na soma kwa makini mabandiko juu ya Balile hapa jamvini .Kwa nini ni habari then uje ujadili vinginevyo tulia mkuu wacha tufuatilie .
 
ukisikia kuset the agenda ndio huku

JF ina break the news halafu hao wengine wanafuaa
 
Wacha nimpigie Balile nisikie anasemaje .Sijui kama atakumbuka utabiri wangu .
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…