Raia aliyeanza kuomba kabla ya uhuru

Raia aliyeanza kuomba kabla ya uhuru

jjackline

Senior Member
Joined
Jul 25, 2024
Posts
111
Reaction score
274
IMG_0253.jpeg

Unaweza kumwita kwa majina utakayo: rais wa ombaomba, nguli wa kuomba, mtoto wa mjini na mengineye.

Hata hivyo, unaweza kumwita mwamba aliyefikia hatua yakutunishiana misuli na mamlaka

unamkumbuka ombaomba huyu maarufu nchini? Alijulikana kwa jina moja la Matonya. Jina lake likawa kiwakilishi na msemo unawakilisha watu wanaoomba msaada wa fedha kwa jamaa, maratiki, au ndugu.

Ukiwa mtu wa kupenda 'kupiga mizinga' jina lililosadifu kwakolilikuwa matonya.

Matonya, ambaye jina lake halisi ni David Paulo, alizaliwa Kijiji cha Mpamatwa, wilayani Bahi, Mkoa wa Dodoma.

Safari yake ya maisha mjini ilianza mwaka 1961 alipohamia Dar es Salaam kwa mara ya kwanza kwa kazi ya kuomba.

Matonya pia aliingia katika vuta nikuvute na aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Yusuf Makamba, alipokataa kurudi kijijini kwao Bahi.
 
Mwamba Matonya Alipambana Na Senior Makamba Akiwa RC DSM
 
Namkumbuka sana enzi hizo nikiishi Dar alikuwa analala kando ya barabara mtaa wa Samora na kikombe ameshika mkononi watu waweke sadaka humo. Nadhani alishafariki kitambo.
 
Nadhani huyu ndiye aliyelifanya kabila la Gogo’s/Wagogo kuwa kama limelaaniwa,(mtanisamehe) lakini kwa sisi tunaoishi mijini siyo ajabu kukuta ombaomba kijana mdada au bibi akiomba omba.

Bahati mbaya sana hata watoto zao shule hawawapeleki utawakuta wanatembea nao ili kuongeza wingi wa familia kupata kipato kwa njia hiyo hiyo ya kuomba
 
enzi hizo! upinzani wa jadi BONGO! ulikua ni:-
*SIMBA vs. YANGA,
*CITY vs. MACHINGA,
*MATONYA vs. MAKAMBA.
 
Serikali imjengee Ghorofa liitwe Matonya Tower kama kumuenzi hapo DSM.
 
Kuna gazeti lilifanya naye mahojiano kipindi kile akasema kwamba ana nyumba na ng'ombe wengi kijijini kwao kwa kupitia kuomba.

Alielezea seasons nzuri za kuomba na maeneo
 
Tunategemea kuweka sanamu lake pale daraja la Shani kama muasisi wa ombaomba hilo eneo.
 
Back
Top Bottom