Raia atakayetoa taarifa ya mhalifu Dar kulipwa Mil. 2

Raia atakayetoa taarifa ya mhalifu Dar kulipwa Mil. 2

Polisi kwanza wawakamete askari wote wa Trafic wala rushwa ndio nitawaamini
 
Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, limetangaza donge nono la kiasi cha shilingi milioni mbili kwa mtu yeyote atakayetoa taarifa za kweli na kwa usiri mkubwa kwa jeshi hilo kuhusu mtu anayefanya uhalifu wa kutumia silaha, lengo likiwa ni kuhakikisha mkoa huo unabaki kuwa shwari.

MULIROOO%20WEB.jpg

Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam Muliro Jumanne

Kauli hiyo imetolewa leo Juni 23, 2021, na Kamanda wa kanda hiyo Muliro Jumanne, wakati akizungumza kwenye kipindi cha Capital Radio, na kwamba siri ya mtoa taarifa itatunzwa na pesa hizo atapatiwa kwa siri bila kuzungushwa.

"Tumeamua kutangaza donge nono la zawadi ambazo tutawapatia kwa siri watakaotuletea taarifa za kweli zilizosahihi za kuwakamata katika mazingira yoyote watu wanaojihusisha na vitendo vya unyang'anyi wa kutumia silaha, na wakikamatwa pamoja na silaha zao, tutatoa milioni 2 palepale mchezo ukikamilika anapewa pesa yake hakuna mzunguko na hili ni zoezi endelevu," amesema Kamanda Muliro.

Aidha, Kamanda Muliro amewataka wahalifu Jijini Dar es Salaam kuchagua mambo mawili kuendelea kuingia kwenye msuguano na jeshi la polisi ama kuwa raia wema.

Chanzo: EATV
Mbona hamjaandika kama ameua tena huyu jamaa? Tangia amehamia dar keshaua raia 6 akiwatoa kafara ili aonekane anafanya kazi, nitumie jukwaa hili kumpelekea ujumbe kwamba kila anayeua haishi muda mrefu ajikumbushe bwana shana yuko wapi aliyekuwa anaua watoto wa watu kisha anashangiria.

Muriro atambue kwamba polisi mwenye weledi haui watu anakamata baada ya kupeleleza na kwa kufanya hivyo anamaliza mtandao mzima was wezi/ majambazi.

Swali kwake ni je Mambosasa ambaye ameua mwishoni mwishoni kabla hajahamishwa hakuwa anayaona haya majambazi? Je rais Samiah anatamani kusikia mnaua raia wake kwa kutowapa nafasi ya kusema ukweli jinsi mlivyo na majambazi ndani yenu na wanawanufaisha?
ACHA MARA MOJA KUUA WATANZANIA!!
 
Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, limetangaza donge nono la kiasi cha shilingi milioni mbili kwa mtu yeyote atakayetoa taarifa za kweli na kwa usiri mkubwa kwa jeshi hilo kuhusu mtu anayefanya uhalifu wa kutumia silaha, lengo likiwa ni kuhakikisha mkoa huo unabaki kuwa shwari.

MULIROOO%20WEB.jpg

Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam Muliro Jumanne

Kauli hiyo imetolewa leo Juni 23, 2021, na Kamanda wa kanda hiyo Muliro Jumanne, wakati akizungumza kwenye kipindi cha Capital Radio, na kwamba siri ya mtoa taarifa itatunzwa na pesa hizo atapatiwa kwa siri bila kuzungushwa.

"Tumeamua kutangaza donge nono la zawadi ambazo tutawapatia kwa siri watakaotuletea taarifa za kweli zilizosahihi za kuwakamata katika mazingira yoyote watu wanaojihusisha na vitendo vya unyang'anyi wa kutumia silaha, na wakikamatwa pamoja na silaha zao, tutatoa milioni 2 palepale mchezo ukikamilika anapewa pesa yake hakuna mzunguko na hili ni zoezi endelevu," amesema Kamanda Muliro.

Aidha, Kamanda Muliro amewataka wahalifu Jijini Dar es Salaam kuchagua mambo mawili kuendelea kuingia kwenye msuguano na jeshi la polisi ama kuwa raia wema.

Chanzo: EATV
Mshahara wa constable tu haufiki million 2
 
Ila huyu RPC mpya inaonesha hatanii mtu
Ni RPC poa sana. Sisi wa Mwanza tumehuzunika sana kwa kuhama,lakini ndio sifa ya mwajiriwa. Ila kwenye hili la kutoa m. 2 eti kwa mtoa taarifa, HAPANA! Au nasema uongo ndugu zangu!!!???
 
Polisi wanazingua, kazi 8mewashinda wanataka kutumia pesa ya kodi zetu hovyo. Mbona miezi michache tu iliyopita hakukuwa na ahadi hizi za hela na ujambazi waliudhibiti kama sio kuukomesha? Imekuwaje sasa, au wameishiwa mbinu?


Vv
 
Back
Top Bottom