Kasomi
JF-Expert Member
- Sep 3, 2014
- 11,030
- 20,391
Aliyekuwa waziri mkuu nchini Kenya Raila Odinga ametangaza kwamba atagombea urais katika uchaguzi mkuu ujao nchini humo mwaka wa 2022.
Alitoa tangazo hilo katika kongamano la Azimio la Umoja siku ya Ijumaa. "Ninatangaza kwamba ninakubali kujiwasilisha kama mgombeaji urais," Raila alisema.
Alizindua vuguvugu la Azimio la Umoja, ambalo alisema litakuwa muungano. Kiongozi huyo wa chama cha ODM alisema hivi karibuni atatoa manifesto yake.
Raila alisema maafikiano yake na Rais Uhuru Kenyatta sio yenye nia ya kujitajirisha. Alisema kuwa hatawahi kuuliza chochote kutoka kwa mwafaka huo isipokuwa kwa nafasi ya kutumikia.
“Lazima niongeze hapa kwamba kwa maridhiano haya, siombi chochote na kamwe sitaomba chochote isipokuwa nafasi ya kutumikia,” alisema.
Waziri Mkuu huyo wa zamani alisema kuwa kuleta amani si biashara ya kujitajirisha, bali ni wito kutoka kwa Mungu.
==========
Kinara wa chama cha ODM Raila Odinga ametangaza rasmi kuwania kiti cha urais kwenye uchaguzi mkuu ujao nchini Kenya kwa tikiti ya Muungano wa Azimio la Umoja.
Basi la Azimio la umoja linaloongozwa na Raila Odinga, liling'oa nanga katika uwanja wa Kimataifa wa Kasarani, uliochorwa rangi mpya za samawati na nyeupe za chama cha ODM. Aidha kila pembe ya uwanja huo yenye viti elfu sitini kulikuwa na mabango ya herufi za R zenye rangi ya chungwa, kuashiria jina la kiongozi huyo mwenye sifa ya kupigania demokrasia ya vyama vingi nchini Kenya.
Kiongozi huyo ambaye alizuru taifa zima kabla ya kongamano la leo alibainisha hoja 10 ambazo ni mwarubaini kwa changamoto zinawakabili wakenya. Raila aliahidi kuwa serikali yake itatenga shilingi za Kenya bilioni mbili za kuwapa vijana kila mwaka. Kuhusu suala la afya,
Raila ameahidi kuwa kila Mkenya atakuwa na mpango wa bima ya afya, huku serikali yake ikiwalipia wale wasiojiweza. Huku Kenya ikiongoza kwa ukosefu wa nafasi za ajira Afrika Mashariki, Raila amesema kuwa, atahakikisha kuwa vijana wanapata kazi kwa kuboresha sekta ya jua kali. Hii itakuwa mara ya tano kwa Raila kuwania kiti cha urais.
"Nilipoongea na Wakenya nikawauliza niendelee au nisiendelee, nawajibu nitaendelea na tarehe nane tisa mwezi ujao, baba atakuwa kwenye kinyang'anyiro cha kuwania kiti cha urais.”, alisema Raila.
Alitoa tangazo hilo katika kongamano la Azimio la Umoja siku ya Ijumaa. "Ninatangaza kwamba ninakubali kujiwasilisha kama mgombeaji urais," Raila alisema.
Alizindua vuguvugu la Azimio la Umoja, ambalo alisema litakuwa muungano. Kiongozi huyo wa chama cha ODM alisema hivi karibuni atatoa manifesto yake.
Raila alisema maafikiano yake na Rais Uhuru Kenyatta sio yenye nia ya kujitajirisha. Alisema kuwa hatawahi kuuliza chochote kutoka kwa mwafaka huo isipokuwa kwa nafasi ya kutumikia.
“Lazima niongeze hapa kwamba kwa maridhiano haya, siombi chochote na kamwe sitaomba chochote isipokuwa nafasi ya kutumikia,” alisema.
Waziri Mkuu huyo wa zamani alisema kuwa kuleta amani si biashara ya kujitajirisha, bali ni wito kutoka kwa Mungu.
==========
Kinara wa chama cha ODM Raila Odinga ametangaza rasmi kuwania kiti cha urais kwenye uchaguzi mkuu ujao nchini Kenya kwa tikiti ya Muungano wa Azimio la Umoja.
Basi la Azimio la umoja linaloongozwa na Raila Odinga, liling'oa nanga katika uwanja wa Kimataifa wa Kasarani, uliochorwa rangi mpya za samawati na nyeupe za chama cha ODM. Aidha kila pembe ya uwanja huo yenye viti elfu sitini kulikuwa na mabango ya herufi za R zenye rangi ya chungwa, kuashiria jina la kiongozi huyo mwenye sifa ya kupigania demokrasia ya vyama vingi nchini Kenya.
Kiongozi huyo ambaye alizuru taifa zima kabla ya kongamano la leo alibainisha hoja 10 ambazo ni mwarubaini kwa changamoto zinawakabili wakenya. Raila aliahidi kuwa serikali yake itatenga shilingi za Kenya bilioni mbili za kuwapa vijana kila mwaka. Kuhusu suala la afya,
Raila ameahidi kuwa kila Mkenya atakuwa na mpango wa bima ya afya, huku serikali yake ikiwalipia wale wasiojiweza. Huku Kenya ikiongoza kwa ukosefu wa nafasi za ajira Afrika Mashariki, Raila amesema kuwa, atahakikisha kuwa vijana wanapata kazi kwa kuboresha sekta ya jua kali. Hii itakuwa mara ya tano kwa Raila kuwania kiti cha urais.
"Nilipoongea na Wakenya nikawauliza niendelee au nisiendelee, nawajibu nitaendelea na tarehe nane tisa mwezi ujao, baba atakuwa kwenye kinyang'anyiro cha kuwania kiti cha urais.”, alisema Raila.