Rais akikosea aambiwe ukweli hadi aelewe

Rais akikosea aambiwe ukweli hadi aelewe

The Boss

JF-Expert Member
Joined
Aug 18, 2009
Posts
49,282
Reaction score
117,244
Wakati wa Magufuli niliwahi andika hapa kama Magufuli anao watu wa kumwambia ukweli na akawasikiliza, nilitoa mfano wa Fidel Castro alivyokuwa anaogopwa na watu wengi sana lakini walikuwepo watu wawili walikuwa wana uwezo wa kumwambia ukweli Raul Castro mdogo wake na Comrade Che Guevara. Hawa wawili walikuwa na uwezo wa kumwambia ukweli na makosa yake bila kupepesa macho na akawasikiliza.

Juzi Rais Samia kasema madini yachimbwe kwenye mbuga, cha muhimu hela. Hii kauli si sahihi kabisa tena sio sahihi kutoka kwa Rais wa nchi.

Rais alipaswa kwanza kupata elimu ya kutosha kuhusu uchimbaji wa madini na athari za mazingira, lakini la muhimu zaidi alipaswa kuniuliza kwanini Viongozi kabla yake wote walisita au kukataa kutoa vibali vya kuchimba Mbugani?

Je hata kama tukikubaliana na Rais cha muhimu hela, kwani Rais hajui utalii ndo unaingiza hela Tanzania kupita madini?

Rais hajui au hana ushauri wa kumwambia kuwa athari za kimazingira huko Mbugani zinaweza moja Kwa moja kuathiri utalii na kupunguza mapato kuliko hata kuongeza hayo mapato?

Rais hajui kuwa hayo makampuni ya madini huwa yanaahidi sana mambo mengi mazuri lakini mwisho hushindwa kutekeleza kuanzia Kodi hadi taratibu za kulinda hayo mazingira? Kampuni ya madini inaweza sababisha sumu kwenye vyanzo vya maji ya wanyama hadi binadamu, na hili sio nadharia imewahi tokea na ushahidi upo.

Madini yanaweza chimbwa yakaisha na mapato ya maana yasipatikane, imeshatokea..na haitakuwa la ajabu ikitokea tena.

Mbuga za Wanyama zilzopo Tanzania haipatikani tena kwingine duniani, ni urithi wa dunia. Mbuga kama Serengeti ina Wanyama Wengi kupitia Mbuga yeyote duniani, hii Peke yake ni dhahabu kuliko dhahabu yenyewe.

Mbuga kama Selous ukubwa wa Ardhi tu ni zaidi ya nchi ya Belgium, halafu leo tunaanza tena kuruhusu uharibifu wa mazingira Mbugani mradi ipatikane hela? tuharibu kuku anaetotoa mayai ya dhahabu ili tukatafute mayai mengine tumboni?

Rais akikosea aambiwe hadi aelewe.
 
Tunakoelekea ni kubaya zaidi jamani. Viongozi waliotangulia wangekuwa wanapambana kuuza kila kitu yeye angekuta nini? Hizo hela wanazopokea baada ya mauzo zinafanya nini zaidi ya kuliwa na wajanja wachache?

Kwani ni lazima rasilimali zote ziuzwe in her regime? Yani napata ile feeling ya mzazi kutaka kuuza mali zake sababu amezeeka ili atumbue kabla hajafa bila kujali kizazi cha wajukuu zake kitakuja kuanza kuhangaika upya.
 
28% ya ardhi Tanzania imehifadhiwa, mbona kama nyingi?

utalii na madini havitofautiani kivile, mwaka jana utalii uliingiza $3.52b, madini $3.06b

na hapo ni baada ya utalii kuweka rekodi ambayo haijawahi tokea tangu uhuru

shida ninayoona labda ni kwamba serikali ikifanya kitu haiwaambii wananchi kwanini, haishawishi....

lakini nyie wananchi wengi mna 'siasa za hisia' mmeamua kumchukia mama basi kila anachofanya mnachukia
 
Tunakoelekea ni kubaya zaidi jamani. Viongozi waliotangulia wangekuwa wanapambana kuuza kila kitu yeye angekuta nini? Hizo hela wanazopokea baada ya mauzo zinafanya nini zaidi ya kuliwa na wajanja wachache?

Kwani ni lazima rasilimali zote ziuzwe in her regime? Yani napata ile feeling ya mzazi kutaka kuuza mali zake sababu amezeeka ili atumbue kabla hajafa bila kujali kizazi cha wajukuu zake kitakuja kuanza kuhangaika upya.
Mm na blame wananchi ambao hawaamki despite ya kudanyiwa haya yote, they are not waking up, ndio kwanza wanajipendekeza?

Unakiokoaje kizazi kinachojioendekeza kwa watesi wao?
 
Hili jambo ni sawasawa na Wakoloni. Hana uchungu na Mali za Tanganyika Si tulisema yeye ni Mzanzibar hana lolote la kupoteza Tanganyika mkabisha sasa ndo anawaonesha rangi yake.

Lakini pia tujifunze kuna sehemu ngapi za wazi zenye madini kwanini wang'ang'anie kwenye hifadhi za mbuga
Bandari imeenda, Sehemu ya Bahari nayo poa imeenda Ngorongoro nayo ilishaenda na sasa Mbuga ya Serengeti yote itaenda Wananchi tunaangalia tu akati fedha zenyewe hatunufaiki nazo hata
 
Labda madini yamegundulika hivi karibuni, waliomtangulia hawakuyagundua.

28% ya ardhi Tanzania imehifadhiwa, mbona kama nyingi?

utalii na madini havitofautiani kivile, mwaka jana utalii uliingiza $3.52b, madini $3.06b

na hapo ni baada ya utalii kuweka rekodi ambayo haijawahi tokea tangu uhuru

shida ninayoona labda ni kwamba serikali ikifanya kitu haiwaambii wananchi kwanini, haishawishi....

lakini nyie wananchi wengi mna 'siasa za hisia' mmeamua kumchukia mama basi kila anachofanya mnachukia
Hizo za madini zote zimeingia serikalini?au za makampuni ya nje serikali imeambulia mrabaha na kodi?..utalii ukiingiza hela unaingiza zaidi kuliko madini
 
Back
Top Bottom