Artifact Collector
JF-Expert Member
- Mar 7, 2019
- 6,617
- 10,205
Kama ni automatic, basi Lissu asinge dai posho zake wakati alijua hakuwepo bungeni! Vitu vingine don't just assume.
Lisu akulilia posho acha uongo, alikua anadai haki zake za matibabu Kama mbungeKama ni automatic, basi Lissu asinge dai posho zake wakati alijua hakuwepo bungeni! Vitu vingine don't just assume.
Kwani lazima kila kitu uchangie hata kama huna hoja?Chadema wamevunja sheria za bunge, wapo hatarini kukosa sifa za kugombea
Wananchi yeye na mumewe, Rais kwa mujibu wa katiba ndiye mkuu wa nchi, na kama mkuu wa nchi yuko na mamlaka ya kifalme ikiwemo kuagiza kitu chochote kifanyike au kisifanyike, tuko na mkuu wa nchi mmoja tu, Rais kama mkuu wa serikali (head of government) hawezi ingilia muhimili mwingine, hampendi badilisheni katiba.Ulipokosea ninkusema tunachojiuliza wananch .sema nachojiuliza mm ? Japo nakuunga mkono 85 %
Nimekwambia kuwa kwa nchi yoyote inayojidai kuwa ina utawala bora, ni lazima pawepo na "separation of power" katika mihimili 3 mikuu, katika kile kinachoitwa "check and balance"Rais sio Mbunge lakini ni sehemu ya Bunge.
Head of State and Government.
Mpaka hapo inatosha.
Ns posho piaLisu akulilia posho acha uongo, alikua anadai haki zake za matibabu Kama mbunge
Umenena vizuri sana .hujapanic kabisa.katiba ndo inaruhusu afanye hivo yeye na mumewe ni maoni ya wawili nice to meet themWananchi yeye na mumewe, Rais kwa mujibu wa katiba ndiye mkuu wa nchi, na kama mkuu wa nchi yuko na mamlaka ya kifalme ikiwemo kuagiza kitu chochote kifanyike au kisifanyike, tuko na mkuu wa nchi mmoja tu, Rais kama mkuu wa serikali (head of government) hawezi ingilia muhimili mwingine, hampendi badilisheni katiba.
Sent using Jamii Forums mobile app
Jiwe kanasa mwenyewe kwenye mtego wa Chadema. Yaani Serikali kuingilia kwenye Mihimili mingine. Sasa ni wazi kwa kila mmoja kulitambua hilo.Kwani posho ni nin mkuu? Me nazani chadema walijua kabisa kujiisolet watakosa posho na wamekubaliana na hilo, nachojua unalipwa posho baada ya kusaini mahudhilio pindi uingiapo bungeni sio otherwise. Jiwe anatafuta kiki tu za.kishamba kwenye hilii.
Mbona povu jingi Mkuu??
demokrasia si njia sahihi ya kuiondoa CCM madarakani.Tumemsikia wenyewe hivi Leo, wakati akimwapisha waziri mpya wa sheria na Katiba, Mwigulu Nchemba, katika mengineyo aliyoongolea Rais, ni kuhusu hatua iliyochukuliwa na wabunge wa Chadema, ambao wameamua kujifanyia "self isolation" kwa ajili ya kile walichokiita wenyewe kuwa ni hofu ya usalama wao na wa wenzao wa CCM, kutokana na ugonjwa wa corona, unaotingisha dunia hivi sasa na kuwa siyo busara kuendelea na vikao hivyo, wakati wabunge wote wakiwa hawajapimwa afya zao kubaini wale walioambukizwa ugonjwa huo na hivyo wafanyiwe katantini.
Jambo lililonistua ni pale nilipomsikia Mheshimiwa Rais akieleza kuwa amemwagiza Spika wa Bunge, ili asiwalipe.posho hizo wabunge wote wa Chadema, kwa siku zote ambazo hawatukuwepo Bungeni!
Ndipo hapo nikaanza kujiuliza, hivi mhimili wa Bunge si unaendeshwa kwa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na hivyo uko huru kufanya maamuzi yake?
Kwa utawala bora unaojali "power separation" hilo jambo haliwezi kujitokeza hata kidogo
Ndani ya Katiba ya Jamhuri ya Tanzania, kuna mihimili 3, ambayo ni serikali, inayoongozwa na yeye Rais, mhimili wa Bunge, ambao unaongozwa na Spika na mhimili wa mahakama, ambao unaongozwa na Jaji Mkuu.
Ndani ya Katiba hiyo hiyo, inaitaka mihimili hiyo mitatu, ifanye kazi kwa Uhuru, katika kile kinachoitwa "check and balance" ambapo haitakiwi mhimili mmoja uingilie shughuli za mhimili mwingine.
Tunachojiuliza wananchi, hivi kama tumemsikia wenyewe wakati akilihutubia Taifa, akiuingilia mhimili wa Bunge, tutajuaje kama hauingilii pia katika utendaji wake, mhimili wa mahakama?
Ndipo hapo ninapojiuliza, hivi Rais Magufuli amepata wapi mamlaka, hadi kumpa kiburi cha kuongea hadharani kuwa atauagiza mhimili wa Bunge, upige STOP malipo yoyote ya posho, ambayo wabunge wa Chadema walistahili kupewa_ wakati akijua fika kuwa mamlaka hayo anayo Spika wa Bunge la Jamhuri ya Tanzania?
Ninawakaribisha wachangiaji wa aina yoyote ile, ili tuidadavue mada hii muhimu mno kwa mustakabali wa Taifa letu
Ni vigumu sana kwani tamko lile limetolewa na M/K wa chama chake.Ingependeza kama speaker wa bunge amjibu rais kama alivyofanya speaker wa Uganda juzi kwa rais Museven ili kuonesha nguvu ya bunge kama mhimili unaojitegemea na wenye maamuzi yake so rais auheshimu.
Unashindwa kutofautisha posho na allowance, lisu alikua anataka allowance zake Kama mbunge ambazo sipo kisheria, posho ni Ile umeingia kwenye kikao unapewa hujaingia upewiNs posho pia
Plan B ipi Mkuu?demokrasia si njia sahihi ya kuiondoa CCM madarakani.
itafutwe plan B!
Kwa mawazo yako kwa kuwa nyinyi mna buku 7, mnadhani na Chadema nao wako hivyo hivyo?
Mimi nasukumwa na uzalendo wa nchi hii, hata ukiwauliza viongozi wa Chadema, mimi hawanijui kabisa!
Rais wa Tanzania kwa mujibu wa katiba ni mkuu wa nchi na kiongozi mkuu wa serikali pia hivyo Spika na Jaji mkuu wako chini yake.
Rais anapotoa maagizo ni vizuri tukaelewa anayatoa katika capacity gani na siyo kuibuka na kuanza kumpinga bila uelewa.
Kwa mfano Rais kama mkuu wa nchi anaweza kulivunja bunge wakati wowote anaporidhika kuna sababu za kufanya hivyo kadhalika anaweza kutoa miongozo fulani kwa Spika au Jaji mkuu.
Tunaposema mihimili ya Serikali, Bunge na Mahakama ni sawa hatumaanishi kwamba viongozi wake wako sawa, la hasha ndio maana mahakama iko chini ya wizara ya katiba na sheria na bunge liko chini ya ofisi ya Waziri mkuu kiutawala.
Mafungu ya fedha za bunge yapitishwa kupitia ofisi ya Waziri mkuu na matumizi yake ni lazima yawe kwa mujibu wa utaratibu wa mlipaji mkuu wa serikali.
Hivyo ni sahihi kabisa Rais Magufuli " kumkumbusha" Spika kwamba fedha ya serikali ina utaratibu wake hivyo wabunge wa Chadema wasiohudhuria vikao wasilipwe posho.
Endapo Spika atapuuza basi taratibu za kisheria zitachukuliwa dhidi yake.
Niko tayari kusahihishwa.
Nawatakia Dominica yenye baraka!
Kama yeye ndiye anayelipa wote, why not? Kama yeye na chama chake wanaamua nani awe speaker nashangaa nini?Katiba inamruhusu? Kwa Ibara ipi ya Katiba. Wengine tunapenda kujifunza!!
Sasa unasemaje Mimi nimiosea kwa kijumlisha wananchi, wakati huo wewe pia ukiniunga mkono kwa mawazo yangu??Ulipokosea ninkusema tunachojiuliza wananch .sema nachojiuliza mm ? Japo nakuunga mkono 85 %
mbn mnazunguka sana wazee? toen jibu tu ikiwa ni sawa raisi kumuagiza spika afanye maamuzi flani na km ni sawa je pia naweza kuiagIza mahakama ifanye maamuzi flani maana nao ni mhimili km bungeRais sio Mbunge lakini ni sehemu ya Bunge.
Head of State and Government.
Mpaka hapo inatosha.
@namkumenenankumene said:mbn mnazunguka sana wazee? toen jibu tu ikiwa ni sawa raisi kumuagiza spika afanye maamuzi flani na km ni sawa je pia naweza kuiagIza mahakama ifanye maamuzi flani maana nao ni mhimili km bunge