Rais anazunguka mbuyu, badala ya kushughulikia kiini Cha tatizo

Rais anazunguka mbuyu, badala ya kushughulikia kiini Cha tatizo

econonist

JF-Expert Member
Joined
Jul 11, 2015
Posts
20,189
Reaction score
29,663
Rais kanikatisha tamaa Sana. Kwenye hotuba yake ya leo hajatoa suluhisho la kudumu kuhusu utekaji. Yeye kajikita kwenye kuwatisha mabalozi na chama Cha CHADEMA kwamba anawafuatilia kila kikao wanachofanya .

Kwa kifupi Rais hajashughulika na kiini Cha tatizo Bali amejikita kwenye matokeo. Yani anazunguka mbuyu baadala ya kuukata. Yeye hasira zake na muda wake amemalizia kuwakemea mabalozi na kuwatisha CHADEMA.

Pia ameonesha dharau kwenye tukio la juzi kwa kusema kifo Cha Ally Kibao ni Cha kawaida Kama vifo vingine. Ni kama anajaribu kutetea jinsi mauaji yalivyo fanyika. Maana jinsi alivyotekwa na kuuawa ile haikuwa kawaida.

Nilitegemea Rais kwenye hotuba yake Leo afanye yafuatayo:

1. Akemee matukio ya kutekana na kuuana.

2. Kuliwajibisha jeshi la Polisi kwa kushinda kulinda Raia.

3. Kuwasihi CHADEMA watulie wasubirie matokeo ya kamati ya uchunguzi kuhusu mauaji ya Ally Kibao.

4. Kuagiza mara moja walihusika na unyama ule wakamatwe.

5. Kuunda Tume Maalum kuchunguza mienendo ya Polisi kwenye kuteka na kuua raia.

6. Kuweka wazi taarifa za kiintelijensia kuhusu wanaofanya utekaji na lengo lao

Soma Pia: Rais Dkt. Samia: Nina taarifa ya kikao chao cha Arusha, wanapanga uhalifu, Serikali ya Tanzania haiondoshwi hivyo
 
Kuna marais walikuwa na mapolisi wa kuwapeleka hadi chooni kunya, lakini siku ya mwisho wao hawakuamini kwamba wao ndio wanakimbizwa hadi na vitoto vidogo. Gadaffi ni mmoja wao lakini mpaka siku ya mwisho wa kifo chake hakuamini nguvu ya wananchi wanyonge.
 
Samia kaamua kama mbwai na iwe mbali. Kaona akicheka na nyani ataondoka ikulu kweli.
 
Kisomo Cha Tanga chaivuruga Ufipa st 😂😂

Ustaadh Yasin: Kisomo kinaanziaga mbali 😂🔥
 

Zaburi 109​

Lalamiko la mtu taabuni
(Kwa Mwimbishaji. Wimbo wa Daudi)
1Usinyamaze, ee Mungu ninayekusifu!
2Watu waovu na wadanganyifu wanishambulia,
wanasema uongo dhidi yangu.
3Wanasema maovu juu yangu,
na kunishambulia bila kisa.
4Ingawa niliwapenda, walinishtaki,
hata hivyo niliwaombea dua.
5Wananilipa uovu kwa wema wangu,
na chuki kwa mapendo yangu.
6Umweke hakimu mbaya dhidi ya adui yangu;
na mshtaki wake ampeleke mahakamani.
7Anapohukumiwa apatikane na hatia;
lalamiko lake lihesabiwe kuwa kosa jingine.
8 Siku za maisha yake ziwe chache,
mtu mwingine na achukue kazi yake!
9Watoto wake wawe yatima,
na mke wake awe mjane!
10Watoto wake watangetange na kuombaomba;
wafukuzwe katika magofu ya nyumba zao!
11Anayemdai kitu amnyanganye mali yake yote;
na wageni wanyakue mapato ya jasho lake!
12Pasiwe na mtu wa kumwonea huruma,
au Kuwatunza watoto wake yatima!
13Wazawa wake wote wafe;
jina lake lisahauliwe katika kizazi kijacho!
14Mwenyezi-Mungu aukumbuke uovu wa wazee wake,
dhambi za mama yake zisifutwe kamwe!
15Mwenyezi-Mungu azikumbuke dhambi zao daima;
lakini wao wenyewe wasahauliwe duniani.
 
Back
Top Bottom