Rais awapiga kijembe TANROADS awatuhumu kuwa WABAGUZI!

Rais awapiga kijembe TANROADS awatuhumu kuwa WABAGUZI!

I regret to say wewe ndio mbumbu!!! Highway nyingi zina Matuta Tanzania... pamoja na Mandela Road... sidhani kuna high way Tanzania kama hiyo... lakini ndio hivyo tena vijana wetu wa chuo kikuu wamekuwa huenda wanagongwa!!!

I hear you Kasheshe I read you .Nikisema unasema Oh Lunyungu vile .Kweli JK anaweza kusema kitu kama kile useme anapnyeza ujumbe? Ana ogopa nini wakati anapaswa kuhakikisha Nchi na kila kitu kiko salama kwa kadiri awezavyo mengine tunamwachia Mungu ? Kama kupeleka ujumbe ndiyo kule basi tuna shida kubwa na ndugu Rais wetu .

Lakini mtoa mchango kauliza kama JK akiwa nje ya Nchi huwa anatumia barabara ama huwa anaishia hotel ?

Nakumbuka once akiwa Waziri wa Nje alikodishiwa Limo toka London hadi Gatwick na Mhindi mmoja wakawa wanafanya biashata humo nadhani alipata nafasi kuchungulia nje ama hata ku feel kwamba LIMO ilipanda tuta ama hapana .

Tuwaache wataalam wafanya mambo ya kitaalam yeye ahangaike na watu wake wa EPA yao waliyo iba wote huko akiwemo yeye .
 
Moran na wengine,
Ngoja nianzie alipoishia Moran. Naona tatizo lipo au linaanzia kwa kile alichosema Moran kuwa hizi inategemea nchi gani wanajenga. Kila nchi wana definition yao ya highway (The first road of this type was opened on September 21, 1924, in Italy, and connected Milan with Como and Lake Como; it was 42.6 km long. Now it is officially designed as Autostrada A9 Milano-Laghi.
Highway designs vary widely. They can include some characteristics of grade separations, multiple lanes of traffic, a median between lanes of opposing traffic, and access control (ramps and grade separation). Highways can also be as simple as a two-lane, shoulderless road.).
Sasa wengine ukiwaambia HIGHWAY unataka kuweka matuta, inakuwa kituko. Nchi kama Ugeruman ukiwa highway unaona hadi wameweka UZIO na speed wewe ni nguvu yako yaani kama una Ferrari au Bugatti Veyron, Lamboghin nk. unaweza kutumia HP zote za gari lako. Matuta katika hii barabara kwa kweli haitakuwa TUTA ila MACHINJIONI.
Naungana na MORAN kuwa Tanzania tuwe na STANDARD yetu kuhusu mgawanyiko wa barabara na wakija wageni tuwaambie tunataka barabara GRADE HII na Grade hii kwa Tanzania iko hivi. Ingawa kwa haraka haraka ningelipenda HIGHWAY ziwe ni zile barabara zilizogawanyika katikati na UZIO, ambazo kwa Tz kwa sasa hatuna. Au hilo tuliache na MIAKA hiyo Watukuu wakija jenga HIGHWAY kweli basi watumie jina la KIITALIANO yaani AUTOSTRAD. All in all, kusema HIGHWAY iwekwe matuta, ni sawa na Malikia Elizabeth kuvaa kama RAYC. Hapo ndipo umuhimu wa alama za barabarani kuwa ukikaribia kijiji au mji unaweka kibao kuwa HIGHWAY imeisha na sasa unakaribia MJI. Ukikaribia tuta unaweka nyingine na ukimaliza unaweka kuwa highway inaanza. Hii inamaaa kuwa ile sehemu iliyopo kijijini na matuta SI HIGHWAY.
 
Duh wahandisi wameingiliwa.............mara matuta.....................mara ajali barabarani...............mara maghorofa kuporomoka
 
Rais wetu naye ni Kilaza sana; sijui kama kweli anapata washauri katika mambo kama haya.

Matuta ya barabarani husababisha barabara kupata shock loads ambazo hufupisha maisha yake. Watu wa Dar wanakumbukua kuwa barabara zote zilizowekewa matuta zimekuwa zinaanza kuharibikwa kwenye matuta haya haya. Kwenye nchi za wenzetu, matuta barabarani ni hadimu sana na yakiwepo huwa yamejengwa kwa staili fulani ambayo hupunguza makali ya shock loads, na vile vile matuta hayo huwekwa katika residential roads tu ambako magari makubwa hayapiti. Na zaidi ya yote matuta hayo huwa ni kwa ajili ya kuwatahadharisha madereva badala ya kuwaadhibu, kwa kawaida huwa yamepakwa rangi inayoonekana kutka mbali wakati wote (usiku na mchana) na kunakuwa na alama mbalimbali kutahadharisha madereva kuwa huko mbele kuna matuta.

Kupunguza ajali kwenye highway zetu inabidi tuache ufisadi ili tujenge barabara za njia mbili mbili; zaidi ya hapo tutakuwa tunatwanga maji kwenye kinu tu.
 
...........Kupunguza ajali kwenye highway zetu inabidi tuache ufisadi ili tujenge barabara za njia mbili mbili; zaidi ya hapo tutakuwa tunatwanga maji kwenye kinu tu.

Prof. Kichuguu......maneno mazito sana hayo.........mwenye masikio na asikie na aliye na macho aone.......na aliye na utashi atekeleze.

1.kuweka matuta ktk highway ni ku-defeat the purpose ya highway
2.Ndugu Rais.......kama jambo lilifanywa kimakosa haku-justify kosa kuendelea/kuendelezwa...............kuwekwa kwa matuta ktk barabara ulizozitaja haina maana makosa hayo yaendelee...............utakumbuka waziri Magufuli alikuwa ameshaanza kuyaondoa hayo matuta.......kwa kufuata ushauri wa wataalamu
3.kuepusha ajali kwa namna moja (kuweka matuta) kunaweza kuleta ajali kwa namna nyingine.........

4.JK......Kumbuka kuna kitu kinaitwa EEE i.e Engineering, Education and Enforcement.......these must go together to achieve the purpose of many designs...............KINACHOTUSHINDA SIYE ni ENFORCEMENT!........ndio maana unashuhudia maghorofa yanaporomoka na ajali zisizoisha barabarani
 
JK ni mbumbu sana, lini highway ikawekwa matuta, huyu jamaa si kila leo anasafili.... Siyo kwenye highway, cha kushangaza huyo waziri ana PhD ya Construction engineering kwa nini ............

Mkuu Kokolo nadhani hapo kidogo naomba nitofautiane nawe maradufu kwa kumuita Mkuu wa Kaya ni MBUMBU.... Angalia kwenye posts zangu zilzopita na utaona kuna logic which may not be what you will like lakini ni facts of life. Pili ukiweza nenda kwenye google au other search engine uangalia maneno [B]"HIGHWAY"[/B] na "FREEWAY" kisha usome tena post yako!!!


I regret to say wewe ndio mbumbu!!! Highway nyingi zina Matuta Tanzania... pamoja na Mandela Road... sidhani kuna high way Tanzania kama hiyo... lakini ndio hivyo tena vijana wetu wa chuo kikuu wamekuwa huenda wanagongwa!!!

Mkuu tupo pamoja lakini Mandela ya Jijini sio Highway.... Sana sana ni Major Urban arterial (au ring road) being the major road going around the city!! Zaidi ya hilo tupo pamoja Mkuu!!


kama rais.......haya matuta highway yameua sana, .......sehemu zenye matuta hakuna vibao, na kama ni mgeni wa barabara lazma ulivae, pia hayo matuta hayana reflecting color ambayo inasaidia kuliona hata ukiwa mbali.matuta yenyewe hayana proper dimensions, unakuta tuta kuuubwwa na haliko smooth kabisa na barabara.wangeyatoa tu kwenye highways.

Mkuu tupo pamoja lakini ukiangalia design speed ya barabara zetu zote Tanzania ni 120kmph lakini we restrict them to 80kmph considering the situation.... Issue ya ajali sababu ya tuta mostly ni uzembe wa madereva (pamoja na kwamba matuta hayana reflection & signs - zimeibiwa) kama dereva alikuwa anenda at 80kmph sioni kwa nini gari ipinduke kwenye matuta......!! Hilo la kuyatoa Mkuu ni kitu ambayo haipo, tutapoteza watu wengi sana na uharibifu wa mali kutokana na madereva wanaoendesha mwendo wa kasi, so THE MATUTAS ARE HERE TO STAY!!

Moran na wengine,
Ngoja nianzie.....

Highway designs vary widely.......

Mkuu nice definition lakini naomba uangalie zaidi kwenye Basic definition ya HIGHWAY in conjuction with FREEWAY (ambapo tunapata Autobahns etc

Rais wetu naye ni Kilaza sana; sijui kama kweli an.......

Matuta ya barabarani husababisha barabara kupata shock loads ambazo hufupisha maisha yake. Watu wa Dar wanakumbukua kuwa barabara zote zilizowekewa matuta zimekuwa zinaanza kuharibikwa kwenye matuta haya haya. Kwenye nchi za wenzetu, matuta barabarani ni hadimu sana na yakiwepo huwa yamejengwa kwa staili fulani ambayo hupunguza makali ya shock loads, na vile vile matuta hayo huwekwa katika residential roads tu ambako magari makubwa hayapiti. Na zaidi ya yote matuta hayo huwa ni kwa ajili ya kuwatahadharisha madereva badala ya kuwaadhibu, kwa kawaida huwa yamepakwa rangi inayoonekana kutka mbali wakati wote (usiku na mchana) na kunakuwa na alama mbalimbali kutahadharisha madereva kuwa huko mbele kuna matuta.

Kupunguza ajali kwenye highway zetu inabidi tuache ufisadi ili tujenge barabara za njia mbili mbili; zaidi ya hapo tutakuwa tunatwanga maji kwenye kinu tu.

Mkuu Kichuguu hilo la Raisi kuwa kilaza kidogo naomba tutofautiane sana.... Raisi ni kama mkuu wa idara, yey anategemea kupokea maelekezo kutoka kwa washauri wake.... Sasa leo JK anatakiwa awe injinia (when tatizo ni roads), daktari (kwenye afya), mwanasheria nk... hiwezekani.... Huwezi kumuita Mkuu wa kitengo (for this case, nchi) kilaza eti sababuw ashauri wake wamechemsha!!

Asante kwa kukubali kuwa hata nchi za wenzetu matuta yapo tena zaidi kwenye residential areas... Mkuu nilisema huko mbele katika highways zetu zote matuta hayapo porini eti, yapo kwenye maeneo ya miji/vijiji (ukumbuke hii ni Bongo ambapo hatuna bypasses around towns/settlements).... Kuhusu shock loads mkuu hapo hebu rudi kwenye types of loadings expected from multiple axles, we consider that one too.... Nakubaliana nawe kuwa kuna tatizo la design za matuta yetu (standardization nilishaongelea kwenye posts huko nyuma). Swala la alama tumegundua kwamba rangi zinapauka na kufutika with time nasi ni wavivu wa kufanya periodic maintenance, pia kwenye signs kama kawa watu wanaiba.... Solution ilikuwa kuweka what we call "Rumble strips" ambazo zinamfanya dereva achukue tahadghari once anazikanyaga na hivyo kupunguza mwendo!! Hilo la eti kwenye makazi ya watu huko kwa wenzetu inakuwa ngumu kulikubali kama "valid argument" kwani tunajua kuna ujenzi unaweza kutokea, kuna watu wanahama na kuhamia, kuna service trucks nk nina uhakika zinapita hayo maeneo pia - au nimekosea Mkuu!!

Barabara za njia mbili?? Wow, Mkuu kwa sasa tunajitahidi kuweka lami kwenye barabara zetu hilo la kuweka njia mbili nadhani ni a long throw lakini tutafika (long term solution), in the mean time MATUTA lazima yaendelee tu Mkuu!!

Prof. Kichuguu......maneno mazito sana hayo.........mwenye masikio na asikie na aliye na macho aone.......na aliye na utashi atekeleze.

1.kuweka matuta ktk highway ni ku-defeat the purpose ya highway
2.Ndugu Rais.......kama jambo lilifanywa kimakosa haku-justify kosa kuendelea/kuendelezwa...............kuwekwa kwa matuta ktk barabara ulizozitaja haina maana makosa hayo yaendelee...............utakumbuka waziri Magufuli alikuwa ameshaanza kuyaondoa hayo matuta.......kwa kufuata ushauri wa wataalamu
3.kuepusha ajali kwa namna moja (kuweka matuta) kunaweza kuleta ajali kwa namna nyingine.........

4.JK......Kumbuka kuna kitu kinaitwa EEE i.e Engineering, Education and Enforcement.......these must go together to achieve the purpose of many designs...............KINACHOTUSHINDA SIYE ni ENFORCEMENT!........ndio maana unashuhudia maghorofa yanaporomoka na ajali zisizoisha barabarani


To sum up wakuu ni hizi definition kama nilivyosema:

1. A freeway — also known as a highway, superhighway, autoroute, autobahn, autopista, autovía, autostrada, dual carriageway, expressway, or motorway — is a type of road designed for safer high-speed operation of motor vehicles through the elimination of at-grade intersections.

2. Highway is a term commonly used to designate major roads intended for travel by the public between important destinations, such as cities.

Wakuu tusisahau kuwa Engineering ni ku translate zile basic principles za nature into a tool to solve our problems.... Tatizo hapa sio kwamba kwa nini barabara zetu hazlingani na za wenzetu bali ni tunafanya/tumefanya nini kutumia maendeleo ya wenzetu katika kutatua matatizo yetu!! Kwa upande wangu ni kama nilivyosema huko mwanzo, wahusika tumezemba kuangalia chanzo cha ajali na hivyo kupelekea wananchi kupeleka malalamiko yao kwa wale wanaowasikiliza (wanasiasa, akiwemo Raisi). Kwa upande wangu badala ya kusema hatutaki matuta tulitakiwa kukaa chini na kuyaBORESHA matuta yetu ili yaweze kuwa kwenye standard ambayo yatatimiza wajibu husika ambao ni kupunguza spidi za magari kwenye maeneo/makazi ya watu; na kwa wakati huohuo kupunguza uharibifu wa magari, barabara na hata kupunguza kero kwa madereva na hata kupunguza vifo vya so called "Madereva wazembe"

Kunradhi kwa mlolongo mrefu sana lakini imebidi!!!

Naomba kuwakilisha!!
 
Naona turudia tena tabia yetu ya kukimbilia kutibu symptoms badala ya ugonjwa wenyewe. Kwa kukimbilia matuta ni kukiri kuwa tumeshindwa kusimamia na kurekebisha tabia ya watumiaji wa barabara zetu. Kwa nini tunasisitiza kusema kuwa ni VIGUMU kuhakikisha sheria za usalama barabarani zinafuatwa? Wenye jukumu la kuzisimamia si wapo! kwa nini wasiwajibishwe? kwa mfano, ikitokea ajali mbaya ya basi, mwenye basi anasimamishiwa biashara ( anawajibika kuhakikisha kuwa dereva wake ni qualified na gari lake ni salama) na kamanda wa traffic wa eneo husika nae anakuwa suspended wakati uchunguzi unafanyika. Ikionekana kuwa ajali ilisababishwa na mwendo mkali, mwenye basi anaonywa na kuwajibishwa kama ni mara ya kwanza na kama ni mara ya tatu anafungiwa biashara ya kuchukua abiria. Kamanda wa traffic anashushwa cheo na ikitokea katika uangalizi wake zaidi ya mara tatu, anastaafishwa. Naamini tukifanya hivi (au hatua zifananazo) tutapunguza ajali maana hakuna anayetaka kukosa ajira au kipato. Madereva wananyang'anywa leseni kwa muda mrefu ( k.m. miaka mitano) na akirudia permamently.

Haya ya matuta yanafanana na wazo la kujenga hospitali kubwa Tumbi ati kwa vile ajali nyingi zinatokea Kibaha!
 
matuta na highway wapi na wapi ....vituko vitupu!
 
Wizara ya MIUNDOMBINU( Kiswahili kinakua!) iko busy "kutuharibia" Wanasiasa wetu tu; UMAKINI katika kazi haupo.
 
Hivi Rais wa hiyo nchi ilipo Tanroad si akutane na ya Rais Jakaya Kikwete ili JK amuombe waweke alama na humps anazotaka??

Au waombe Umoja wa mataifa wawakutanishe kama JK ambaye ni mwenyekiti wa AU imeshindikana.

Mambo mengine bwana.................................. kweli hii nchi itaendelea kudumaa kama kweli yamesemwa hayo.

Hivi huyu jamaa yuko serious kweli, anaongea nini, yuko dunia gani? hahaha, au anatania tu hapa. hivi kweli wewe haujui Tanrods ni nini? hadi ufikirie kuwa ni nchi?hahahahaha. yaani jamaa kanichekesha kishenzi...hahahaha, kwiwkiwkiwkilll
 
Mkuu nice definition lakini naomba uangalie zaidi kwenye Basic definition ya HIGHWAY in conjuction with FREEWAY (ambapo tunapata Autobahns etc

1. A freeway — also known as a highway, superhighway, autoroute, autobahn, autopista, autovía, autostrada, dual carriageway, expressway, or motorway — is a type of road designed for safer high-speed operation of motor vehicles through the elimination of at-grade intersections.

2. Highway is a term commonly used to designate major roads intended for travel by the public between important destinations, such as cities.
Naomba kuwakilisha!!
Moran,
Ndiyo maana nikaandika kuwa hizo definiion zinategemea na nchi uliyopo. Kwa hapa nilipo, ukisema AUTOSTRAD yaani Highway inamaana zile tu zenye minimum 2 lanes na hazi-cross direct na barabara nyingine. Chini yake kuna Express road in-cross kwa shida. Inafuata General road, nk nk. Kwao wao hapa ni kuwa Tanzania HATUNA HIGHWAY. Ukienda USA utagundua kuwa Tanzaniatuna HIGHWAY. Ndiyo maana nikasema kuwa naungana na wewe ili Tanzania tuwe na definition yetu. By the way hiyo hapo juu umendika ni ya nchi gani?
Juu ya aliyeandika eti tujenge barabara zenye lane mbili mbili, sijui kama anajua anachokisema. Hiyo ya lane moja moja yenyewe haina magari, sasa ukijenga ya lane mbili si unakuwa DUBAI au Kazakhstan wanaojenga majengo na yanakaa wazi maana hamna wapangaji na wakati huo kwa sisi Tanzania pale Dar kwa barabara pamechoka!! Kuna haja ya kujenga (IKIWEZEKANA) express roads kama RINGS kuzunguka Dar kama ilivyo Mandela Road. Ila tu iwekewe KONOKONO ili magari yasiwe yanasimama kwenye crossing
Moran, jaribuni pia kutumia ule mchezo mwingine wa kupunguza speed yaani au kupindisha barabara kila baada ya muda fulani au kuweka kila baada ya distance fulani ROUGH finishing. Hii huwa inawaamsha madereva na pia kuwakumbusha wawe waangalifu. Pia matuta jamani yasiwe makubwa sana ya kutisha kiasi kwamba ukisahau au usipoliona basi gari linavunja spring zote.
 
Sikonge, right on point.... Unajua tatizo letu ni kwa kweli matuta mengine yamejengwa kama kukomoa madereva (bila standard yoyote). Najua ni a bit primitive solution (matuta) lakini kwa kweli kwa uelewa wangu na kutokana na kazi yangu nimepita mikoa mingi sana hapa nyumbani matuta ndio njia pekee ya kutufanya kuwa na control ya mwendo kwa madereva wetu....

Mkuu FM, nakubaliana nawe kwamba tutatue tatizo, bahati mbaya hayo yote umyaweka hapo tumejaribu lakini mwendo ni uleule watu wanatesa na mwendo na ajali ndio kabisaa... Sasa kwa vile mimi (kama walivyo wenzangu wachache hapa nyumbani) tumejaribu kuangalia na kuona solution ni kuweka matuta (lakini hayapendelewi saana) tungeomba ushauri mbadala kwa tatizo hili angalau tupunguze ajali na kuondoa matuta (considering our economy and timely implementation)?

Tukumbuke kuwa hata kama sisi ni wahandisi/kandarasi/mchundo wote tumefundishwa shuleni lakini kuna maswala ambayo yanatokana pia na experience/exposure/logic na offcourse utundu, tusaidiane jamani kuliko kukaa na kusema hatutaki matuta, THEN WHAT!!!

Naomba kuwakilisha!!
 
Mkuu Sikonge, kwa swali lako hizo definition nimetoa "WIKIPEDIA"................. Zipo nyingi kwa kweli lakini hizi za Wiki... nimeona kidogo zimeonyesha nchi nyingi (mabara tofauti) na hivyo kunifanya niziweke....

Naomba radhi kwa kutokuonyesha source yangu kwenye original posting!!!
 
Unapokwenda kwenye event halafu ukawa huna cha kuongea, sio lazima uongee! Silence is golden. Sikutegemea rais akaongelee masuala ya matuta ya barabarani hadharani.

Mbona kuna mambo mengi sana ya msingi ya kufanya jamani!!!!
 
Tukumbuke kuwa hata kama sisi ni wahandisi/kandarasi/mchundo wote tumefundishwa shuleni lakini kuna maswala ambayo yanatokana pia na experience/exposure/logic na offcourse utundu, tusaidiane jamani kuliko kukaa na kusema hatutaki matuta, THEN WHAT!!!

Mhandisi Morani! Tatizo tumeanzia hapo ulipoishia, then what! Kwa nini tusiangalie kwanza kuwapenalize wale wote wanaohusika katika hizi ajali (kuanzia mhandisi aliye'design' barabara chini ya kiwango, mhandisi asiyesimamia matengenezo ya barabara, mkuu wa idara/kitengo husika na hiyo barabara, madereva wabovu, wamiliki wa vyombo vibovu na wanao ajiri madereva wabovu, mapolisi wanaoangalia tu magari mabovu, yaliyojaza kupita kiasi na yaendayo kasi, sisi abiria tunaoshangilia madereva wanao kiuka taratibu n.k.). Tuanze huko badala ya kukimbilia huku kwenye matuta. Matatizo ya matuta ni kwamba tukishayaweka tunasahau mengine. Tatizo ni kubwa zaidi!
 
Mhandisi Morani! Tatizo tumeanzia hapo ulipoishia, then what! Kwa nini tusiangalie kwanza kuwapenalize wale wote wanaohusika katika hizi ajali (kuanzia mhandisi aliye'design' barabara chini ya kiwango, mhandisi asiyesimamia matengenezo ya barabara, mkuu wa idara/kitengo husika na hiyo barabara, madereva wabovu, wamiliki wa vyombo vibovu na wanao ajiri madereva wabovu, mapolisi wanaoangalia tu magari mabovu, yaliyojaza kupita kiasi na yaendayo kasi, sisi abiria tunaoshangilia madereva wanao kiuka taratibu n.k.). Tuanze huko badala ya kukimbilia huku kwenye matuta. Matatizo ya matuta ni kwamba tukishayaweka tunasahau mengine. Tatizo ni kubwa zaidi!

swala la elimu kwa mtumiaji wa barabara linapaswa kufanya na chama cha watumiaji barabra au tanzia roads users asscoiation, wakishirikiana na sumatra,

hata hivo hatuwezi kuona wananchi wakiteketea kwa kigezo cha kutoa elimu, matuta yaendelee kujengwa, mpaka hapo hiyo elimu itakapokolea kwa madereva na watumiaji wa bara2
 
Hivi huyu jamaa yuko serious kweli, anaongea nini, yuko dunia gani? hahaha, au anatania tu hapa. hivi kweli wewe haujui Tanrods ni nini? hadi ufikirie kuwa ni nchi?hahahahaha. yaani jamaa kanichekesha kishenzi...hahahaha, kwiwkiwkiwkilll


Kijana/dada/bibi/mzee/kaka, read between the lines...... ....

Usikurupuke kuandika/ku comment kama huelewi tumia muda kidogo kufikiri.

Ngoja nikupe namna ya kufikiri. Rais wa nchi analalamikia idara iliyopo chini yake, kana kwamba hawezi kufanya kitu. Sasa kama yeye aanalalamika sisi wananchi tufanyeje?, It is as if analalamikia NCHI flani.....

Angalia usije ukawa unachekesha wewe.
 
Tuko pamoja Pundit, kwa kweli tumejaribu sana swala la speed control ikiwemo kuweka "LUKU" kwenye mabasi lakini kama kawaida yetu rushwa na nini mambo yakawa palepale..... Unajua tumekuwa tunaangalia ajali zikiendelea kutokea siku hadi siku na kupoteza maisha ya nguvu kazi yetu muhimu sana kwa nchi yetu... Ukiangalia kwa haraka inaonekana swala zima la "Traffic Safety" limeachwa kwa Polisi.... Kwa mtazamo wangu ni kwamba Polisi sio watunga sheria za barabara bali ni wafuatiliaji wa utekelezaji (mahakama pia inaingia hapa).... Ukijiuliza, TANROADS/MoW wana jukumu/nafasi gani katika hili?? Sisi tunaishia kuangalia ujenzi wa mabarabara bila kuangalia effect ya barabara mpya, ongezeko la magari vinatoa mchango gani katika kuongezeka kwa ajali....

Hawa wakuu wa TANROADS walitakiwa kufanya a concise study ya nchi nzima kisha kuamua kufanya improvements zikiwemo matuta, rumble strips, katika mabarabara yote ya Bongo... Lakini cha kushangaza hili halijanyika, pia lazima wafanye standardization ya matuta hayo (angalia yale ya Mikumi na yale ya kule Mazinde, utafikiri jamaa wanatoa contract ya kujenga matuta na standards ni up to the contractor regardless of the difference)

Hili la wanasiasa kuheshimu watendaji ni sawa kabisa lakini ndugu yangu tukubaliane kuwa swala la ajali ijijini na uwekaji wa matuta wa kwanza kujua ni wanasiasa.....sababu ni kwamba mikutano ya hadhara wanavijiji wanalalamika kwa wanasiasa manake hao watendaji (wahandisi) hawaendi/hawafiki kujua vifo vinavyotokea kwa ajali!!! So kwa hili sidahni kama tunaweza kuwa control wanasiasa unless us, watendaji/wajenzi tuamua kutimiza wajibu wetu - kulinda maisha na mali za watu wetu!!

Fundi, tupo pamoja Mkuu.... Hili swala kama nilivyosema, hapo mwanzoni (angalia quote yangu hapo juu) utaona kwamba tupo kwenye mlengo mmoja kuwa ajali sio polisi wa kuangaliwa pekee au mahakama kwa kutoa fine na adhabu nyinginezo. Lazima sisi kama wanafani tuangalia kwa mfano kwa nini ajali ni nyingi sana katika maeneo fulani (mfano rahisi ilikuwa pale Chalinze -Segera Rd kuna eneo ilikuwa kuna ajali nyingi sana tukafikia kufanya a complete re-allignment)..... Mkuu, sikatai kwamba tuna udhaifu wa kutokupenda kufanya tafiti, tatizo ni wakati mwingine hata hawa wakuu wa TANROADS, MoW, nk hawana hata accident data za barabara zilizo chini yao.... Sasa pamoja na uvivu pia wajibu wetu wa kuweka records pia unatushinda na hili sio la Raisi kuliangalia bali ni watendaji wake......
 
swala la elimu kwa mtumiaji wa barabara linapaswa kufanya na chama cha watumiaji barabra au tanzia roads users asscoiation, wakishirikiana na sumatra,

hata hivo hatuwezi kuona wananchi wakiteketea kwa kigezo cha kutoa elimu, matuta yaendelee kujengwa, mpaka hapo hiyo elimu itakapokolea kwa madereva na watumiaji wa bara2

Ninachozungumzia hapa ni uwajibikaji! Tunapenda mno simplistic solutions (matuta, speed governors n.k.) ambazo zinatuepusha kuangalia tatizo kwa undani. Nitatoa mfano. Hivi karibuni pametokea wimbi la majengo, cranes kuanguka katika jiji la New York. Pamoja na jitihada za idara ya majengo kujaribu kujisafisha, imebidi, Mkuu wake, the Buildings Commissioner ajiuzulu! Sisi wanakufa zaidi ya watu 40 kwenye ajali ya gari lakini tunaishia kuwakaripia madereva wazembe, kutoa salamu za rambirambi na kuunda tume ambazo ripoti zake hata siku moja hatuzisikii! Sheria zipo, wahusika wapo, kwa nini tusihakikishe zinasimamiwa kikamilifu na hao waliopewa hilo jukumu? Pakitokea tatizo watu wawajibike. Matuta yako kibao lakini watu bado anafariki. Ili haya matuta yawe effective inabidi yawe kila baada ya mita hamsini barabara nzima! Mapolisi wana rada guns, wana alcometres, sasa kwa nini wasiwajibishe akionekana dereva alikuwa anakimbiza huku amelewa ndani ya eneo lao?
 
Back
Top Bottom