Rais Chama cha Walimu Tanzania(CWT) atolewa kikaoni kwa nguvu

Rais Chama cha Walimu Tanzania(CWT) atolewa kikaoni kwa nguvu

peno hasegawa

JF-Expert Member
Joined
Feb 24, 2016
Posts
14,255
Reaction score
23,949
Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Chama cha Walimu Tanzania (CWT) wamemuondoa kwa nguvu Kaimu Rais wa chama hicho, Dinah Mathaman na kumchagua mjumbe mwingine kuongoza kikao.
---

Rais CWT atolewa kikaoni kwa nguvu

Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Chama cha Walimu Tanzania (CWT) wamemuondoa kwa nguvu Kaimu Rais wa chama hicho, Dinah Mathaman na kumchagua mjumbe mwingine kuongoza kikao kinachoendelea jijini Dodoma leo Ijumaa Desemba 16, 2022.

Mathaman ametolewa kwa nguvu akisukumwa na wajumbe kisha kumzonga hadi nje ya ukumbi huku wakipiga kelele za kutomtaka kwenye chama hicho.

Hata hivyo, Mwananchi linafahamu kuwa sababu kubwa iliyomfanya kiongozi huyo kutolewa nje kwa nguvu ni uamuzi wake kulazimisha ajenda namba tatu ijadiliwa kama namba saba badala ya kufuata mtiririko.

Chanzo: Mwananchi
 

Ijumaa, Desemba 16, 2022


Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Chama cha Walimu Tanzania (CWT) wamemuondoa kwa nguvu Kaimu Rais wa chama hicho, Dinah Mathaman na kumchagua mjumbe mwingine kuongoza kikao kinachoendelea jijini Dodoma leo Ijumaa Desemba 16, 2022.

Mathaman ametolewa kwa nguvu akisukumwa na wajumbe kisha kumzonga hadi nje ya ukumbi huku wakipiga kelele za kutomtaka kwenye chama hicho.

Wajumbe wanadai kutokuwa na imani na viongozi wao kwa kushirikiana na Katibu wa TUCTA na Msajili wa vyama vya Wafanyakazi kugandamiza haki za Walimu na maslahi yao.
 
Kuwa Mwl. Bongo ni noma aisee!

Watu wenyewe kipato cha ngama halafu bado makato chungu nzima na matozo na kuibiwa tena jamani?!

Mnawatafuta nini Wlm nyie?!
 
Wangempiga kabisa. Amekula sana pesa zetu walimu hadi tumemchoka.
Watoto Wadogo waliowafundisha wanawasumbua, they want to divide teachers so can be ruled easily kisa dola iko nyuma yao..wamjue adui yao kwanza wasiishie kufukuzana tu.
 
Waalimu waondokane kuwa na chama chao cha CWT kufanywa jumuiya mojawapo chini ya CCM kama UVCCM, UWT, WAZAZI, USHIRIKA n.k

16 December 2022
Dodoma, Tanzania

VURUGU ZAIBUKA MKUTANO WA CHAMA CHA WALIMU, WAMTIMUA KAIMU RAIS



Mkutano huo wa CWT unafanyika katika ukumbi unaomilikiwa na CCM wa Jakaya Kikwete mjini Dodoma
 
15 December 2022
Dodoma, Tanzania

Vurumai CWT, Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha CCM Bara Mndeme awalipua "Msikubali kutumika na wenye nia mbaya"



Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha CCM Bara, Christina Mdeme amewataka walimu kutokubali mtu kuwaingilia na kuwavunjia umoja walionao.

Kada na kiongozi huyo wa juu wa CCM Christine Mdeme ameyasema hayo leo Desemba 14, 2022 wakati akizungumza katika mkutano mkuu wa Chama cha Walimu (CWT) unaoendelea jijini Dodoma.

“Mwalimu ni mzalendo namba moja, walimu tuendelee kusimamia uzalendo kwa manufaa ya Taifa, tusikubali mtu akatuchonganisha na tusikubali mtu akatuingilia na kutuondolea umoja wetu,”amesema Mdeme na kuibua shangwe kutoka kwa walimu hao.
 
Kuwa Mwl. Bongo ni noma aisee!

Watu wenyewe kipato cha ngama halafu bado makato chungu nzima na matozo na kuibiwa tena jamani?!

Mnawatafuta nini Wlm nyie?!
kwenye utumishi wa umma walimu wanalipwa sawa na wengine tu isipokuwa madaktari na manesi. Tatizo wao wanalalamika zaidi na kwasauti kubwa
 
Back
Top Bottom