DOKEZO Rais hili la mbolea umenikuna sana. Nakuomba ifanyieni uchunguzi Benki ya Kilimo, kuna jambo halipo sawa

DOKEZO Rais hili la mbolea umenikuna sana. Nakuomba ifanyieni uchunguzi Benki ya Kilimo, kuna jambo halipo sawa

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'

Mganguzi

JF-Expert Member
Joined
Aug 3, 2022
Posts
1,604
Reaction score
3,715
Jana ilikuwa siku njema sana kwangu hii ni baada ya kusikia tamko la serikali kuhusu bei elekezi ya mbolea. Nasema nimekunwa sana Kwa sababu hili lilikuwa aibu kubwa mwaka Jana . Mimi ni mkulima wa mahindi mashamba yapo mkoani Rukwa.

Mwaka Jana nimeshindwa kumudu kabisa bei ya mbolea hekari moja nimekunwa napata hata Tani 3au mbili na nusu lakini kulingana na kushindwa kumudu gharama za mbolea nimejikuta mwaka huu ekari Moja napata Tani Moja tu!

Nasema Asante sana kwako rais na wizara ya kilimo, ombi langu ni kuhusu hii benki ya kilimo inavyoonesha ,Kuna aina ya wakulima wanaopata mikopo kupitia benki hii .na ninahisi Kuna mabwanyenye wanapewa pesa hata mashamba hawana.

Benki ya kilimo ipo kwenye majiji makubwa lakini sio vijijini ambako ndio Kuna walengwa haswaa. Lakini pia Kuna urasimu mkubwa na masharti magumu sana ambayo mkulima wa kawaida hawezi kumudu ,naiomba serikali iwe inafuatilia hao wanaokopeshwa kama kweli ni wakulima.

Nahisi sio wakulima kwa sababu hakuna mkulima anaeenda kuomba mkopo kutoka vijijini na akapewa, wanapeana wenyewe Kwa kujuana ,niombe pia benki hii ifungue matawi vijijini
 
Narudia tena utaratibu wa kuppata mbolea ya ruzuku ueleweke. Msije kuwa walimu mkaanza kutukana kwa kutokuelewa kwa 23.3

Wakulima wanapaswa kusajiliwa, usajili wao ndio utawafanya wapate mbolea ya ruzuku. Na sio kila duka la pembejeo utaenda utakuta hiyo bei ya ruzuku.

Wakulima mnapaswa kuuelewa utaratibu kabla ya nyinyi kuanza kuilamu serikali
 
Dap 70000,urea 70000, npk aina zote 70000,sa 50000
Hii sio kwamba ukienda tu dukani utaikuta. Mnaapaswa kuelewa utaratibu uliowekwa ili kupata hii bei, wakulima ni lazima wasajiliwe kwanza na huo usajili ndio utawafanya wapate hizo mbolea za ruzuku na sio kila muuzaji atakua na hizo mbolea za ruzuku.

Ninaona kabisa mtakuja kuanza kuitukana serikali Kama walimu walivyoshindwa kuelewa 23.3
 
Huo ndiyo ukweli...wengi wanaopewa mikopo hata shamba hawalijui

Ova
Raisi ana kazi kubwa sana, watu wengi akili hawana kabisa. Walimu walishindwa kueilewa 23.3 ni kwa kina nani.

Naona kabisa wakulima nao wanaandaa lawama bila kuelewa utaratibu utaotumika kupata hiyo mbolea ya ruzuku. Si kila duka la pembejeo litakua na mbolea ya ruzuku. Na Kuna masharti lazima mkulima ayafuate ili kupata hiyo mbolea ya ruzuku.
 
Narudia tena utaratibu wa kuppata mbolea ya ruzuku ueleweke. Msije kuwa walimu mkaanza kutukana kwa kutokuelewa kwa 23.3

Wakulima wanapaswa kusajiliwa, usajili wao ndio utawafanya wapate mbolea ya ruzuku. Na sio kila duka la pembejeo utaenda utakuta hiyo bei ya ruzuku.

Wakulima mnapaswa kuuelewa utaratibu kabla ya nyinyi kuanza kuilamu serikali
Nendeni mkawasajili wakulima kupata mbolea yenye ruzuku wakiwa na kadi zao za Chama tawala kama mlivyofanya ktk zoezi la SENSA.

Bt mwisho wenu umewadia.
 
Nendeni mkawasajili wakulima kupata mbolea yenye ruzuku wakiwa na kadi zao za Chama tawala kama mlivyofanya ktk zoezi la SENSA.

Bt mwisho wenu umewadia.
Nimemsaidia kumuelewesha huyo kuwa asifikirie akienda tu dukani atakutana na hizo bei. Kuna utaratibu wake na haupo sehemu zote.

Mengine kaa nayo
 
Back
Top Bottom