Memento
JF-Expert Member
- Jun 13, 2021
- 4,423
- 9,986
Mimi binafsi siipendi CCM kabisa, Ila kuna baadhi ya viongozi kidogo naona wana afadhali mmojawapo ni Hussein Mwinyi.
Raisi Mwinyi ni kiongozi mzuri sana, lakini hii haifanyi yeye kutotenda makosa. Raisi Mwinyi wakati wa kuagiza chanjo ya corona aliwahakikishia Wazanzibar kuwa chanjo wanayoleta ni salama sana hivyo wasiwe na wasiwasi wowote.
Akaenda mbali na kusema wameamua kuagiza chanjo kwa kuwa kuna watu wanahitaji kwenda "hijja", hivyo ni lazima walete chanjo watu wachanje waende hijja.
Alisisitiza sana kuwa kwenda hijja kuna vikwazo kwa wasiochanjwa hivyo chanjo hizi zitafanya Wazanzibar kwenda hijja bila kikwazo. Leo serikali hii hii imetoa taarifa kuwa waliopata chanjo wanapaswa tena kuchanja kwa kuwa chanjo waliochanja mwanzo haitambuliki huko Saudi Arabia.
Haya ni masihara kabisa kwenye afya za watu, ilipaswa kabla ya kuagiza chanjo ilipaswa Serikali ijiridhishe. Leo unawaambia watu warudie kuchanjwa chanjo nyingine tofauti na Sinovac, ikiwa mwanzo ulitumia kigezo cha hijja ili wakubali kupata chanjo.
Haya ni makosa makubwa ambayo Rais umeyafanya, inapaswa uwaombe radhi wote waliopata chanjo.
Kwa kuwa kama chanjo waliyopata haitambuliki sehemu takatifu Kama Makka, je usalama wa hiyo chanjo upo wapi?
Raisi Mwinyi ni kiongozi mzuri sana, lakini hii haifanyi yeye kutotenda makosa. Raisi Mwinyi wakati wa kuagiza chanjo ya corona aliwahakikishia Wazanzibar kuwa chanjo wanayoleta ni salama sana hivyo wasiwe na wasiwasi wowote.
Akaenda mbali na kusema wameamua kuagiza chanjo kwa kuwa kuna watu wanahitaji kwenda "hijja", hivyo ni lazima walete chanjo watu wachanje waende hijja.
Alisisitiza sana kuwa kwenda hijja kuna vikwazo kwa wasiochanjwa hivyo chanjo hizi zitafanya Wazanzibar kwenda hijja bila kikwazo. Leo serikali hii hii imetoa taarifa kuwa waliopata chanjo wanapaswa tena kuchanja kwa kuwa chanjo waliochanja mwanzo haitambuliki huko Saudi Arabia.
Haya ni masihara kabisa kwenye afya za watu, ilipaswa kabla ya kuagiza chanjo ilipaswa Serikali ijiridhishe. Leo unawaambia watu warudie kuchanjwa chanjo nyingine tofauti na Sinovac, ikiwa mwanzo ulitumia kigezo cha hijja ili wakubali kupata chanjo.
Haya ni makosa makubwa ambayo Rais umeyafanya, inapaswa uwaombe radhi wote waliopata chanjo.
Kwa kuwa kama chanjo waliyopata haitambuliki sehemu takatifu Kama Makka, je usalama wa hiyo chanjo upo wapi?