#COVID19 Rais Hussein Mwinyi waombe radhi waliochanjwa Zanzibar, umewakosea sana

#COVID19 Rais Hussein Mwinyi waombe radhi waliochanjwa Zanzibar, umewakosea sana

Hija bado hadi mwakani.
Labda ziara ya Umrah ambayo sio lazima kwenda.
 
Ngumu kumeza.Ati chanjo haitambuliki na Saudi Arabia? This is nonsense.kwa maana hiyo wanaamini haifanyi kazi au si salama.Mbona sasa Gwajima anatiwa hatiani bure? Ina maana chanjo haijawa approved na WHO??
Hatari sn
 
Hakuna Hijja ya mtu kuifanyia nyumbani kwake katika Sharia ya Uislam.
Afya kwanza maana ndio mtaji #1. Kuna haja gani ukimbilie kuchanjwa ksbb ya hijja?. Ukikosa mwaka mmoja hijja,ukaifanyia nyumbani tu huku ukisikilizia chanjo nzuri kuna ubaya gani?. Ona sasa madudu mliyopigwa nayo.

Watu wangu wanaangamia kwa kukosa maarifa
 
Tutulie. Je kuna uthibitisho kwamba wakati Zanzibar iliagiza ile Sinovac, Saudia walitangaza tayari chanjo maalumu? Kama wakati ule Saudia hawakutaja aina za chanjo wanazokubali, sioni kosa lolote.
Menginevyo hakuna ubaya maana Sinovac haina hasara.
Ni chanjo dhaifu lakini hata hivyo afadhali kuliko kukosa chanjo; kufuatana na majaribio %51 walikingwa dhidi maambukizi, na %100 walikingwa dhidi ya dalili nzito, hakuna aliyepaswa kuingia hospitalini.

(Chanzo: The Sinovac COVID-19 vaccine: What you need to know)
 
Wanasiasa siyo watu wa kuwaamini hata kidogo, wanatanguliza maslai yao kwanza. Hata hii J&J tunayo aminishwa Salama ipo Siku tu itakataliwa.
Mchina atalipiza kisasi anasoma mchezo. Maana yake Chanjo ya china inakosa wanunuzi na soko inawezekana ikawa Chanjo yenye ufanisi mkubwa kiutendaji mwilini.
 
Hakuna Hijja ya mtu kuifanyia nyumbani kwake katika Sharia ya Uislam.
Nipe maana hijja. Kufupisha ukiniambia ni maombi,basi nyumbani sehemu yenye utulivu MUNGU anakusikia zaidi kuliko sehemu ingine.
 
Mimi binafsi siipendi CCM kabisa, Ila kuna baadhi ya viongozi kidogo naona wana afadhali mmojawapo ni Hussein Mwinyi.

Raisi Mwinyi ni kiongozi mzuri sana, lakini hii haifanyi yeye kutotenda makosa. Raisi Mwinyi wakati wa kuagiza chanjo ya corona aliwahakikishia Wazanzibar kuwa chanjo wanayoleta ni salama sana hivyo wasiwe na wasiwasi wowote.

Akaenda mbali na kusema wameamua kuagiza chanjo kwa kuwa kuna watu wanahitaji kwenda "hijja", hivyo ni lazima walete chanjo watu wachanje waende hijja.

Alisisitiza sana kuwa kwenda hijja kuna vikwazo kwa wasiochanjwa hivyo chanjo hizi zitafanya Wazanzibar kwenda hijja bila kikwazo. Leo serikali hii hii imetoa taarifa kuwa waliopata chanjo wanapaswa tena kuchanja kwa kuwa chanjo waliochanja mwanzo haitambuliki huko Saudi Arabia.

Haya ni masihara kabisa kwenye afya za watu, ilipaswa kabla ya kuagiza chanjo ilipaswa Serikali ijiridhishe. Leo unawaambia watu warudie kuchanjwa chanjo nyingine tofauti na Sinovac, ikiwa mwanzo ulitumia kigezo cha hijja ili wakubali kupata chanjo.

Haya ni makosa makubwa ambayo Rais umeyafanya, inapaswa uwaombe radhi wote waliopata chanjo.

Kwa kuwa kama chanjo waliyopata haitambuliki sehemu takatifu Kama Makka, je usalama wa hiyo chanjo upo wapi?
Mungu anazidi kuwaaibisha.
 
La misumu wamechomwa na hayatambuliki kwingine?
Aliyeleta hakulijua Hilo?
Na yeye kuchomwa hiyo au ilikuwa zuga tu na water for injection?
 
Sasa si wanajiboost na johnson and johnson.....uliambiwa chanjo ni moja tu? jiandae kuishi kwenye ncha ya sindano.
 
wanataka za Wamarekani? maana hyo cinovac ni ya wachina
 
Back
Top Bottom