Rais Kenyatta aruhusu Watanzania kuanza kufanya kazi na biashara Kenya bila kuwa na Work Permit wala Business visa

Rais Kenyatta aruhusu Watanzania kuanza kufanya kazi na biashara Kenya bila kuwa na Work Permit wala Business visa

Tuna mtihani mkubwa wa kujinasua na hii mentality ya unyonge tuliyojazwa na wanasiasa wetu. Yaani badala ya kuchangamkia opportunity na kuangalia fursa zilizopo kenya... automatically una conclude kwamba hamna kitu unachoweza kufanya kule na wao wana advantage huku? Naililia sana nchi yangu kwa hii mental slavery tuliyonayo
unakurupuka. nijuavyo mimi maisha ya tz kwa mtu wa kawaida ni bora kuliko ya kenya. nani mnyonge sasa hapa?
 
Mtego huu, anataka na Samia aseme hivyohivyo kwa wakenya

Nilifikiri ni mimi mwenyewe nimemstukia Uhuru.Kenya ni wajanja kweli kweli Mama Samia Suluhu asipokuwa kuwa makini anaweza kuchukiwa na WaTanganyika very soon.
 
Nilifikiri ni mimi mwenyewe nimemstukia Uhuru.Kenya ni wajanja kweli kweli Mama Samia Suluhu asipokuwa kuwa makini anaweza kuchukiwa na WaTanganyika very soon.
halafu samia hajasema hivyo wala nini, kaona mtego
 
Kigelegele kwa Kenyatta aruhusu watanzania kuanzia sasa ruksa kufanya kazi na biashara kenya bila kuwa na work permit wala Business visa

Kasema mida hii mkutano wa wafanya biashara
Mbona hakuruhusu wakati wa utawala wa Magufuli halafu nyie MATAGA mlikuwa mnamshangilia huyo mwendazake ,Duh,Mungu alifanya kazi nzuri mno kumchuka Magufuli.
 
Piga kelele kwa Kenyatta akee😁😁😁😁😁😁

Seriously, EA hatutakiwi kuwa na barrier zozote za kibiashara. Tuna custom union ya maneno tu lakini haifanyi kazi. Tunazuia na kubania biashara za Kenya huku tukijaza masoko kwa bidhaa za India na China. EA inatakiwa kufunguka, iwe kama nchi moja. Hapo ndiyo tunaweza fikia shirikisho la kisiasa
Usiwe one sided...hata huko Kenya huwezi kufanya biashara kiholela...ila nakubaliana na wewe kwamba custom Union ni maneno tu...nchi zote hazina political will...ziko very protective...
 
unakurupuka. nijuavyo mimi maisha ya tz kwa mtu wa kawaida ni bora kuliko ya kenya. nani mnyonge sasa hapa?
Hujanielewa. Ninasema tumedanganywa na viongozi wetu kwamba sisi ni wanyonge...sijui hatuna uzoefu..eti wakenya wako vizuri sana kwenye kazi na bishara na tukiwaruhusu kuja watachukua kazi na biashara zote. Sio kweli! Ni hofu tu ya kipumbavu
 
Dah....

Inafikirisha na kusikitisha sana...

labda sijaelewa unasikitika nn, lakn embu take moment mtu na hela zake mtanzania wa namanyele, ana details gani za aina ya biashra ya kufanya nchini kenya? hajui mtu kenya, na wala asitegemee support ya ubalozi wetu kule...

wao makejipanga. wao tayr wana information za kutosha kwa kila raia wao anayetaka kwnda kuwekeza au kufanya biashr tanzania. possibly atapewa mkopo wenye riba ndogo, atasemehewa kodi kwa upande wa kenya kwa kila bidhaa atakoyo itoa kenya kupeleka tanzania, kwa miaka fulani..

pengine, kwa mkenya atakaye kuja kuwekeza huku, moja ya mashrt ya kupata mkopo kwao, lazma aajir wakenya kiasi kadhaa katika top management, na mshahar usiwe less tha amount fulani..
sisi tumejipanga kwa hili ili tuseme ok njooni?
wao wana hakika hakuna mtanzania atakaye weza kushindana nao katika ardhi yao kibiashar labda mtanznia mwenye asili ya asia.

embu tufikirie nje ya box, balaz zetu zimetupa information gani za opportunities zilizopo kenya kwa watanzania, na how easy kuzi access hizo infor kwa raia wa kawaida.
 
Kutoka Angle hiyo nakubaliana nawe Mkuu

Itashangaza tunakumbatia wachina zaidi wakati jirani zetu wanabaniwa fursa ambazo kimsingi zitafanya mambo yawe mepesi kwetu.

Nilishangaa siku moja eti BoT wanawabania wakuu wa kampuni moja ya kikenya work permit wakati wao wameajiri watanzania mamia hapa Tanzania, kana kwamba haitoshi, kuna watanzania wengine wanapelekea nje kwenye ofisi za hiyo kampuni kufanya kazi huko.

Sasa unajiuliza, sisi hasahasa tunachotaka ni kitu gani??
 
Usiwe one sided...hata huko Kenya huwezo kufanya biadhara kiholela...ila nakubaliana na wewe kwamba custom Union ni maneno tu...nchi zote hazina political will...ziko very protective...
No..tanzania na burundi ndio hazina political will. Tangia enzi za kikwete kenya, uganda na rwanda wamekua wako tayari kufungua mipaka yao na kuruhusu raia waingie na national ID tu bila passport..tanzania na burundi tumekua tukijivuta vuta. Mpaka wao wakaamua kuanza kwa nchi zao. Mambo ya kufuta work permits wamekua tayari kwa miaka 10 sasa...TZ na Burundi ndio tumekua tunakataa
 
Hujanielewa. Ninasema tumedanganywa na viongozi wetu kwamba sisi ni wanyonge...sijui hatuna uzoefu..eti wakenya wako vizuri sana kwenye kazi na bishara na tukiwaruhusu kuja watachukua kazi na biashara zote. Sio kweli! Ni hofu tu ya kipumbavu
ulishawahi kufanya biashara na mkenya? ulishawahi kuishi hata Nairobi tu? ulishawahi kufanya kazi hata za kuajiriwa na mkenya? wabongo tupo polepole sana, visingizio kibao,upeo wa kimataifa mdogo etc, hapo tunatakiwa kurekebika. ukifika Nairobi tu watu unaokutana nao barabarani wako busy wanakimbia kwenda wanakoenda, bongo unakuta mtu anaenda kazini kwake au kwenye kibarua anatembea kama muda ni shemeji yake. huu ndio ukweli. tunatakiwa kubadilika. ndio maana investors wanaependa kuajiri wakenya kuliko sisi kwasababu hizi. bora tena hata bara, ukienda zenji ndio muda utafikiri nini sijui, wako poelpole mamwinyiiiii. unyonge sio wanyonge ila wazembe.
 
Kigelegele kwa Kenyatta aruhusu watanzania kuanzia sasa ruksa kufanya kazi na biashara kenya bila kuwa na work permit wala Business visa

Kasema mida hii mkutano wa wafanya biashara
Kuna watu wakiwa wanataka kuoa wanakuwa wakarimu kupindukia na hutoa michango mingi kwa wanaooa ili baadaye na wao waje kuchangiwa fedha nyingi.
 
Kigelegele kwa Kenyatta aruhusu watanzania kuanzia sasa ruksa kufanya kazi na biashara kenya bila kuwa na work permit wala Business visa

Kasema mida hii mkutano wa wafanya biashara
Hiyo tunaita ‘Mtama kwa watoto’ ni watanzania wangapi waweza kushindana na wakenya? Ni chambo ili nasi tujiingize kichwa kichwa; utakuta hata waziri mkuu ni Mkenya. Yangu macho na masikio
 
Wakenya wajanja, hata kama huna work permit, wala business visa, kazi hupati Kenya.. Mtanzania hawezi pewa nafasi na wakenya kufanya kazi.. Sisi tusiruhusu hilo, eti wakenya waje free huku, hilo litakuwa kosa kubwa sana kutokea
Acha uongo we jamaa mbona kuna watanzania kibao tu wanafanya kazi Kenya nina ndugu wanafanya kazi safaricom
 
Back
Top Bottom