According to the dataz, mkulu ataondoka kesho na kufika bongo keshokutwa, sasa kazi kwa Chenge maana Sophia Simba, ni mmoja wa viongozi wasiozidi wawili wenye nia njema na mafanikio ya muungwana, na yeye anajua hilo sasa atakosa kumsikiliza?
Kwako mkulu Chenge, kwa nini usichomoe tu kabla mkulu hajafika ili kumuepusha na kujibu maswali yasiyojibika?, na pia kutuokoa taifa na kuunda tena tume ya kukuchunguza, please mzee do all of us a favor just go kwa kuanza kuandika barua ya kujiondoa, tizama umesababisha mkulu kutokwenda Europe kwa kuogopa maswali, imebidi Brown afunge safari ya ghafla kwenda kuonana na mkulu wetu, kisa wewe kwa nini usitoke tu yaishe!
Unjau ninaanza kuamini maneno ya mkulu mmoja leo, kuwa huenda hatutafika na viongozi wetu wote mpaka mwisho wa term mbili, wengi wataishia njiani, na tutaanza na wapya karibu wote soon!