Rais Kikwete ateua mabalozi wapya. Marmo, Batilda na wengine ndani!

Rais Kikwete ateua mabalozi wapya. Marmo, Batilda na wengine ndani!

Maamuzi ya kuchagua viongozi ikiwamo mabalozi Tanzania yamekuwa ya ajabu ajabu kuanzia enzi za Nyerere. Nadhani haya ndiyo madhara makubwa sana yatokanayo na siasa za chama kimoja na demokrasia iliyo hasiwa.
Viongozi walipotokea kutofautiana kimawazo, au kugombana kwa sababu moja ama nyingine, ili kupooza mambo Mkuu alikuwa anawapeleka nje kuwa mabalozi ili wapishe wenzao na wale anaoelewana nao zaidi wafanye kazi kwa amani. Uteuzi mwingi wa mabalozi nchini Tanzania ulikuwa na vijisababu visivyo na tija kwa Taifa. Nakumbuka uteuzi wa M.Generali Sarakikya kipindi kile kuwa Balozi Nigeria ulikuwa na sababu kubwa, hata uteuzi wa Mwakawago kwenda UN ulikuwa na nia ya kurekebisha matatizo katika chama. Huu utaratibu wameeendelea kuufuata mpaka leo.
Sasa siasa za namna hii huwa haziendelezi nchi hata kidogo kinyume chake ni kuwa zinabomoa. Watanzania tuna bahati mbaya sana na tuna kazi kubwa mpaka tuje kupata katiba mpya isiyotokana na mabavu ya CCM na ujanja ujanja wake ndipo tutaanza kupiga hatua sahihi kuelekea maendeleo ya kweli kwa ajili ya Taifa zima.
 
Tuna mifano mingi sana!! South Korea hatuna balozi kabisaaa tuna kaki-consullar office kanakoendeshwa tena mkorea, ukienda kuulizia kitu wala hupati msaada wowote. Balozi wa japan ndo anacover hadi South Korea lakini sidhani kama alishawahi kufika.

Wakati South Korea wanatoa scholarships nyingi za graduate kwa wabongo, kuna makampuni mengi yanafanya kazi saizi tanzania mengine tunayaita ni ya kichina lakini ukweli ni kuwa ya kikorea bado hatuna ubalozi. Kampuni moja linalofanya utafiti wa mafuta pwani ya Bahari ya hindi juzi juzi Pindi kaja kufungua ile meli! wala hashtuki kuwa hatuna ubalozi. Only in Tanzania these happens!
 
Dah hii ni zaidi ya balaa............ Kwani JK hakuwaona wengine adi hawa walioexpire. kweli hii ni serikali ya kishikaji. AU inawezekana mkuu wenu huyu hakusoma Philosophy 111 (critical thinking and argumentation)
 
Tatizo sio Rais ila ni Wananchi Wake waliomchagua, ndio maana hawa walio teuriwa kuwa mabalozi walikataliwa na wananchi lkn bado wapo madarakani.
 
Rais JUHA ni aibu kwa Taifa..................Ivi CCm ikipigwa chini 2015 makada, viongozi wa chama nao mafisadi watakimbilia WAPI??????
 
Nashindwa nianzie wapi kumtafakari JK!
Natamani nitapike sasahivi!


Yaani mh! What can i say!! .....only a de facto president can do such a thing like this.......to me, a democratically elected president will never do such a mediocre thing like this.........tumeona hata juzi jinsi ambavyo president Sata wa zambia alivyowatimua (recall)mabalozi kadhaa waliokuwa wamewekwa kishkaji na Banda nchi za nje(akiwamo hata yule balozi mwanamke aliyekuwa tz)......hii kitu aliyofanya JK ni mojawapo ya misuse ya madaraka (kuteua ma rejects kuwakilisha our national interests abroad) na watu makini wanayahesabu haya........only time will tell.........yeye JK yaelekea hajifunzi hata kwa marais wenzake wanaomzunguka kina Kibaki na Sata (he was with them juzi tu!!).........anyway.....kweli sikio la kufa halisikii dawa........

Ifike mahali sasa watanzania tukatae kabisa huu upuuzi kwa kupitia katiba mpya.......yaani pawepo na criteria au mechanisms za kupima teuzi zoote za rais...kuanzia mawaziri, makatibu wakuu, wakuu wa mikoa na wilaya na ma diplomats.... si mtu anakaa anaamka asubuhi eti kwa kuwa ni rais na katiba imemruhusu...basi anatuteulia mijitu ya hovyo hovyo tu kishkaji(mingine mihawara)ituongoze....hii kitu tuikatae yaani...this thing has to stop yaani.......otherwise hatutabadilika kama nchi....i swear......i can't wait for a new katiba.......................
 
Naona anazidi kujipa uhakika wa kuweka wenyeji wake ili siku akienda kubadilishiwa damu asipate shida kabisa!!
 
Tatizo mumesahau kuwa hawa jamaa hawakukutana na baba Ridh1 barabarani
 
Is ok as president ...... Ila.......Mabalozi waliokuwepo katika Hizo nchi kama Vile Omari Ramadhani Mapuri aliyewahi kuwa waziri wa mambo ya ndani akagombana na waandishi wa Habari...Kicha akapelekwa Ubalozi China...Wanaenda wapi sasa?? au ubunge wa kuteuliwaaaaa?????
 
Is ok as president ...... Ila.......Mabalozi waliokuwepo katika Hizo nchi kama Vile Omari Ramadhani Mapuri aliyewahi kuwa waziri wa mambo ya ndani akagombana na waandishi wa Habari...Kicha akapelekwa Ubalozi China...Wanaenda wapi sasa?? au ubunge wa kuteuliwaaaaa?????

Hata Omar Mapuri ulikuwa ni uteuzi tata aliofanya Mkapa kumpeleka China. Tumezungumzia zaidi uteuzi wa China lakini tunasahau kwamba hata uteuzi wa Batlida kwenda Kenya nao ni tata. Kenya ni jirani na mshirika wetu mkubwa kibiashara. Simuoni Batlida kama chaguo sahihi kutuwakilisha ktk Kenya.
 
Tuna mifano mingi sana!! South Korea hatuna balozi kabisaaa tuna kaki-consullar office kanakoendeshwa tena mkorea, ukienda kuulizia kitu wala hupati msaada wowote. Balozi wa japan ndo anacover hadi South Korea lakini sidhani kama alishawahi kufika.

Wakati South Korea wanatoa scholarships nyingi za graduate kwa wabongo, kuna makampuni mengi yanafanya kazi saizi tanzania mengine tunayaita ni ya kichina lakini ukweli ni kuwa ya kikorea bado hatuna ubalozi. Kampuni moja linalofanya utafiti wa mafuta pwani ya Bahari ya hindi juzi juzi Pindi kaja kufungua ile meli! wala hashtuki kuwa hatuna ubalozi. Only in Tanzania these happens!

Balozi 10 mpya alizosema waziri wa mambo ya nje kwamba zitafunguliwa Korea haimo?
 
3.jpg
custom_name_congratulations_phd_card-p137422218283970646q6ay_400.jpg

PHD ya Ukweli.
Kumbe ubongo wako Rejao una Gia ya Rivas tu..!!!!!!!!!.

Nimeipenda picha hii
 
jaani mie nina langu la kibinafsi kidogo

hebu mwenye profile ya huyu bini mtoto wa balozi wetu mpya Oman anipe taarifa zake

b21.jpg



Ndugu Ali A. SALEH, ameteuliwa kuwa Balozi nchini OMAN. Kabla ya hapo Bwana Saleh alikuwa Balozi Mdogo (Consul General) nchini Dubai.
 
b22.jpg



Mhe. Phillip MARMO, ameteuliwa kuwa Balozi nchini CHINA. Kabla ya hapo Mhe. Marmo alikuwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Uratibu na Bunge.
 
b23.jpg


Bwana Mohamed H. HAMZA, ameteuliwa kuwa Balozi nchini MISRI. Kabla ya hapo Bwana Hamza alikuwa Mkurugenzi wa Mambo ya Nje, ZANZIBAR, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.
 
b19.jpg


Bibi Grace J.E. MUJUMA, ameteuliwa kuwa Balozi nchini ZAMBIA. Kabla ya hapo Bibi Mujuma alikuwa Kaimu Mkurugenzi, Ushirikiano wa Kikanda (Regional Co-operation), Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.
 
Back
Top Bottom