Rais Kikwete; Kaza Mkanda, Bana Matumizi, Punguza Ukubwa wa Serikali

Rais Kikwete; Kaza Mkanda, Bana Matumizi, Punguza Ukubwa wa Serikali

Naomba Wasaidizi wa Kikwete wampelekee hii makala yangu, labda anaweza kupata suluhisho la kuwa lipa Wafanyakazi na kutuepusha umwagaji damu!
 
Na sie wa pembeni jamani tunachangia kubariki matumizi mabaya ya Serikali. Wengi tunaona wtu wanavyotumia zaidi ya kipato chao, Mikataba ya bei ya juu kwenye halmashauri na Taasisi mbalimbali lakini hatunyooshi kidole. Mfano Halmashauri ya Kinondondi hivi karibuni imeingia mkataba na mkanadarasi kujenga kajiko cha kuchomea takataka(Incinerator) kwa Shs. milioni sita kwa ajili ya hospital ya kata moja wakati Mhandisi Mmoja Mtaalam akiri kwamba gharama yake hata Shs. Milioni Mbili haiwezi kufikiwa huku uongozi wa Hospitli ya kata hiyo wakilazimishwa kutia saini makataba ambao wao sio waliingia na mkanadarasi kwa pesa zinazokusanywa Hospitalini hapo. cha kushangaza wananchi wanalalamika tu " Ahh jamani hapa wamepitiliza". basi hapo imeisha na pesa zinaondoka. katika hali hii kama hamna" Whistle Blowers" tutafika?
 
REv. Kishoka,
Mkuu wangu unapigia mbuzi gitaa..hakuna kiongozi hata mmoja ndani ya CCM anaweza kukubaliana na mawazo yako -HAKUNA.
majuzi tu nimeona wabunge wakijisifia wao kwa kutoa misaada ama kupelekea maendeleo ktk wilaya zao kwa fedha zao za mfukoni na hakika wabunge hawa wanapendwa sana na kupongezwa hadi hapa kijiweni..Sasa tujiulize hivi? hivi kweli hiyo ndio kazi ya Mbunge? mbunge anapopeleka maendeleo kijijini kwake kwa kutumia fedha yake ndivyo inavyotakiwa ama ndio tunawapa mwanya wa wao kutumia Takrima kupata kura za wananchi.. Iweje leo jamani kazi ya mbunge isiwe kuwakilisha wananchi bungeni ila ni kuwaondolea adha na matatizo yao kiasi kwamba mbunge anafikia kujisifia kwamba kuanzia saa 11 asusubuhi hadi jioni watu hujipanga mlangoni kwake kupata kuondolewa matatizo yao ya kila siku.. Tena basi kuna mbunge mmoja mama Ghama alifikia kujisifia kwamba mishahara na posho wanazopata sii kubwa hata kidogo kutokana na kwamba fedha zao nyingi hutumika kuwasaidia watu wenye matatizo..
Sasa tunapopotosha manaa ya UBUNGE na kuruhusu watu kutoa michango yao kifedha na mali ktk jamii ili mradi wapate kuchaguliwa sijui nini faida ya wabunge kwenda bungeni! kwa nini tusiwachague matajiri kina Manji na Mengi wenye fedha tayari watatusaidia zaidi ya hao wabunge wanaosubiri posho zao kuwa ndio mtaji wa miradi ya jimbo...

Haya kuna watu wanaomsifia hata Lowawengine wakidai kwamba Lowassa ni kiongozi mzuri mchapa kazi ambaye Tanzania inamhitaji... kweli unaweza amini maneno kama haya? kuna mtu aliniuliza kama nafikiri Pinda ni Waziri mkuu mzuri kuliko Lowassa..ajabu sana kana vile nchi yetu haina tena watu zaidi ya Lowassa. Nikamjibu kwa nini unafananisha Pinda na Lowassa na sio Lowassa na Mwanri, Mwandosya, Magufuli na wengine wengi tu ambao pia wana sifa za uchapa kazi?..

Hivyo mkuu wangu sisi wenyewe akili zetu zimefungwa katika zizi la Ujinga. Tumekuwa kama kuku wa kienyeji walifungiwa usiku kucha ndani ya banda. asubuhi banda linapofunguliwa kutoka mkuku wakakimbia hovyo hovyo na huchua muda waka settle down na kujiona huru..Matatizo ya KIkwete ni matokeo ya upeo wetu sote ktk mitazamo mingi ya kisiasa na kiutawala...


Asante sana Mkuu mchango wako mzuri
 
Naomba Wasaidizi wa Kikwete wampelekee hii makala yangu, labda anaweza kupata suluhisho la kuwa lipa Wafanyakazi na kutuepusha umwagaji damu!

Tatizo hapa ni kwamba most of wasaidizi wa Kikwete ni wale waliokuwa wakimsifia na kumpigia debe in the last election. Rev how do you expect the "Apoologists" kumpelekea makala hii??? Am not just being negative but skeptical as to what we have already seen in this administration.

Sifa kubwa ya wasaidizi ambao ni apologists ni kumake sure hawamuudhi bwana wao, they will alwayz do lap dancing according to his tune no matter what.

As for this one ni bora kuitoa gazetini na kuiandika kama barua ya wazi kwa muheshimiwa mkulu!
 
Lakini itakuwa ni aibu kama rais hawezi hata kuingia JF na kusoma shauri mbali mbali zinazotolewa na wadau.
 
Back
Top Bottom