Rev. Kishoka
JF-Expert Member
- Mar 7, 2006
- 4,526
- 1,540
- Thread starter
- #21
Naomba Wasaidizi wa Kikwete wampelekee hii makala yangu, labda anaweza kupata suluhisho la kuwa lipa Wafanyakazi na kutuepusha umwagaji damu!
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
REv. Kishoka,
Mkuu wangu unapigia mbuzi gitaa..hakuna kiongozi hata mmoja ndani ya CCM anaweza kukubaliana na mawazo yako -HAKUNA.
majuzi tu nimeona wabunge wakijisifia wao kwa kutoa misaada ama kupelekea maendeleo ktk wilaya zao kwa fedha zao za mfukoni na hakika wabunge hawa wanapendwa sana na kupongezwa hadi hapa kijiweni..Sasa tujiulize hivi? hivi kweli hiyo ndio kazi ya Mbunge? mbunge anapopeleka maendeleo kijijini kwake kwa kutumia fedha yake ndivyo inavyotakiwa ama ndio tunawapa mwanya wa wao kutumia Takrima kupata kura za wananchi.. Iweje leo jamani kazi ya mbunge isiwe kuwakilisha wananchi bungeni ila ni kuwaondolea adha na matatizo yao kiasi kwamba mbunge anafikia kujisifia kwamba kuanzia saa 11 asusubuhi hadi jioni watu hujipanga mlangoni kwake kupata kuondolewa matatizo yao ya kila siku.. Tena basi kuna mbunge mmoja mama Ghama alifikia kujisifia kwamba mishahara na posho wanazopata sii kubwa hata kidogo kutokana na kwamba fedha zao nyingi hutumika kuwasaidia watu wenye matatizo..
Sasa tunapopotosha manaa ya UBUNGE na kuruhusu watu kutoa michango yao kifedha na mali ktk jamii ili mradi wapate kuchaguliwa sijui nini faida ya wabunge kwenda bungeni! kwa nini tusiwachague matajiri kina Manji na Mengi wenye fedha tayari watatusaidia zaidi ya hao wabunge wanaosubiri posho zao kuwa ndio mtaji wa miradi ya jimbo...
Haya kuna watu wanaomsifia hata Lowawengine wakidai kwamba Lowassa ni kiongozi mzuri mchapa kazi ambaye Tanzania inamhitaji... kweli unaweza amini maneno kama haya? kuna mtu aliniuliza kama nafikiri Pinda ni Waziri mkuu mzuri kuliko Lowassa..ajabu sana kana vile nchi yetu haina tena watu zaidi ya Lowassa. Nikamjibu kwa nini unafananisha Pinda na Lowassa na sio Lowassa na Mwanri, Mwandosya, Magufuli na wengine wengi tu ambao pia wana sifa za uchapa kazi?..
Hivyo mkuu wangu sisi wenyewe akili zetu zimefungwa katika zizi la Ujinga. Tumekuwa kama kuku wa kienyeji walifungiwa usiku kucha ndani ya banda. asubuhi banda linapofunguliwa kutoka mkuku wakakimbia hovyo hovyo na huchua muda waka settle down na kujiona huru..Matatizo ya KIkwete ni matokeo ya upeo wetu sote ktk mitazamo mingi ya kisiasa na kiutawala...
Naomba Wasaidizi wa Kikwete wampelekee hii makala yangu, labda anaweza kupata suluhisho la kuwa lipa Wafanyakazi na kutuepusha umwagaji damu!
Lakini itakuwa ni aibu kama rais hawezi hata kuingia JF na kusoma shauri mbali mbali zinazotolewa na wadau.