Rais, kivutio kikuu cha Wawejezaji Duniani ni utawala unaotabirika kisiasa na kisheria

Rais, kivutio kikuu cha Wawejezaji Duniani ni utawala unaotabirika kisiasa na kisheria

kifupi kirefu

JF-Expert Member
Joined
Oct 29, 2018
Posts
539
Reaction score
3,507
Naomba kumshauri Rais kwamba kwa mtazamo wangu Ni vigumu kupata wawekezaji walio serious kuja kuwekeza nchini kwa sababu nchi yetu haina mfumo mzuri wa kisheria na kikatiba. Haki Tanzania inapatikana kwa utashi wa Rais na si kwa kuzingatia misingi ya kisheria.

Ni kweli anaweza anaweza kuvutia wawekezaji lakini naomba nimtabirie kwamba wawekezaji wengi watakaokuja na waliopo ni wale wanaowekeza kwa lengo lakuchuma na kuhifadhi walichochuma nje ya mipaka yetu.

Tutegemee wawekezaji ambao mitaji yao mikubwa itawekezwa nchi jirani au kwenye mataifa yao na hapa watapafanya sehemu yakuchuma.

Ili tuwe na wawekezaji wenye confidence na Tanzania lazima tufanye mabadiliko ya sheria ikiwemo katiba. Maamuzi ya haki yaachwe kwenye muhimili na Mahakama na Rais aache kuwa chanzo Cha haki.
 
Siyo kwa mtazamo wako, hiyo ni fact. Tunahitaji katiba mpya ili tukuze uchumi wetu.Katiba mpya ni lazima atake asitake.
E49_.jpg
 
China ina siasa mbovu wawekezaji wamejaa.

Uarabuni wana sheria mbovu na unyanyasaji wawekezaji wamejaa.

Tanzania tuna kitu gani kibaya kuwazidi waarabu ama wachina?

Acheni siasa uchwara.
 
Back
Top Bottom