Rais Macron aituhumu Urusi kuchafua jina la Ufaransa barani Afrika

Rais Macron aituhumu Urusi kuchafua jina la Ufaransa barani Afrika

Strong ladg

Senior Member
Joined
Jul 15, 2021
Posts
170
Reaction score
445
Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron ameituhumu nchi ya Urusi kutumia mitandao ya kijamii kuchafua jina la Ufaransa barani Afrika.

Rais Macron alisema maneno hayo tarehe 6 Januari 2025 wakati akiwahutubia wanadiplomasia wa Ufaransa wanaohudumu nje ya nchi hiyo.

Akiongelea swala la kupungua ushawishi wa Ufaransa barani Afrika katika miaka ya hivi karibuni, Rais Macron alisema propaganda zinazoenezwa na Urusi kuhusu nchi yake kwenye mitandao ya kijamii ndio chanzo cha kupungua kwa ushawishi wa Ufaransa.

Vile vile, alisema wanaharakati wa Afrika wanaofahamika kama Pan Africanists ambao wana ushawishi mkubwa kwenye mitandao ya kijamii,hutumia kete ya kupinga ukoloni kuchafua taswira ya Ufaransa.

Miongoni mwa Pan Africanists hao ni Bibi Nathalie Yamb kutoka nchini Niger na Bwana Kemi Seba kutoka nchini Benin ambao mwaka 2023 Rais Macron aliwaita " waajiriwa wa Putin"

Source: FRANCE 24
 
Hakuna uwongo wowote ambao Urusi unaongea kuhusu Ufaransa. Ufaransa ni nchi inayowaangamiza Waafrika haswa zile nchi zilizotawaliwa na Ufaransa ambazo ni 18 hapa Afrika. We fikiria hii kitu, toka miaka ya 60 mpaka leo hizi nchi zinailipa Ufaransa hela za kutawaliwa nao kwa sababu Ufaransa inadai iliendeleza hizi nchi wakati wanazitawala. In reality, Ufaransa wanachukua hela zaidi ya walizotumia kwenye makoloni yao. As we speak, Ufaransa inajengwa na hela za hizi chi. Ufaransa ni wezi / majambazi na washitakiwe.
 
Nawaza na wasiwasi wanguje hizo nchi zinaweza kujitegemea zenyewe kweli? Nchi nyingi za africa ukiachana na south afrika bado ni omba omba zinategemea pesa kutoka kwa wahisani je waowakimuacha mfaransa nani atawasaidia?
 
Nawaza na wasiwasi wanguje hizo nchi zinaweza kujitegemea zenyewe kweli? Nchi nyingi za africa ukiachana na south afrika bado ni omba omba zinategemea pesa kutoka kwa wahisani je waowakimuacha mfaransa nani atawasaidia?
Nchi Gani labda imewahi kusaidiwa na Ufaransa na ilisadiwaje? Ungejua Ufaransa ndio haiwezi kusurvive bila Afrika hata usingeongea. Kwani Ufaransa ina nini hasa ambacho Afrika inahitaji?
 
Nawaza na wasiwasi wanguje hizo nchi zinaweza kujitegemea zenyewe kweli? Nchi nyingi za africa ukiachana na south afrika bado ni omba omba zinategemea pesa kutoka kwa wahisani je waowakimuacha mfaransa nani atawasaidia?
Duh!unafikirisha saana..
 
Nawaza na wasiwasi wanguje hizo nchi zinaweza kujitegemea zenyewe kweli? Nchi nyingi za africa ukiachana na south afrika bado ni omba omba zinategemea pesa kutoka kwa wahisani je waowakimuacha mfaransa nani atawasaidia?
Ufaransa haijawahi kuwa na msaada wowote nchi hizo bali Ufaransa ndo alikuwa ana faidika na hizo nchi.
 
Urusi anafanya ujinga fulani kule west Africa - kuchafua wengine ili yeye aonekane bora for nothing zaidi ya umbea wa kumataifa!
 
Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron ameituhumu nchi ya Urusi kutumia mitandao ya kijamii kuchafua jina la Ufaransa barani Afrika.

Rais Macron alisema maneno hayo tarehe 6 Januari 2025 wakati akiwahutubia wanadiplomasia wa Ufaransa wanaohudumu nje ya nchi hiyo.

Akiongelea swala la kupungua ushawishi wa Ufaransa barani Afrika katika miaka ya hivi karibuni, Rais Macron alisema propaganda zinazoenezwa na Urusi kuhusu nchi yake kwenye mitandao ya kijamii ndio chanzo cha kupungua kwa ushawishi wa Ufaransa.

Vile vile, alisema wanaharakati wa Afrika wanaofahamika kama Pan Africanists ambao wana ushawishi mkubwa kwenye mitandao ya kijamii,hutumia kete ya kupinga ukoloni kuchafua taswira ya Ufaransa.

Miongoni mwa Pan Africanists hao ni Bibi Nathalie Yamb kutoka nchini Niger na Bwana Kemi Seba kutoka nchini Benin ambao mwaka 2023 Rais Macron aliwaita " waajiriwa wa Putin"

Source: FRANCE 24
Huyu naye haeleweki sijui ni Bangee??
 
Urusi anafanya ujinga fulani kule west Africa - kuchafua wengine ili yeye aonekane bora for nothing zaidi ya umbea wa kumataifa!
Hata Urusi asipoeneza propaganda kwani ukweli haujulikani? Kwani inahitaji uwepo wa Urusi kujua kwamba Ufaransa waliua watu kwa majaribio ya mabomu ya nyuklia kule Algeria? Inahitajika propaganda za Urusi kujua kwamba Ufaransa walimuua Thomas Sankara ? Inahitajika propaganda za Urusi kujua kwamba Ufaransa alikuwa anachota uranium ya bure pale Niger? Hata waziri mkuu wa Italia alisema hili jambo miaka 5 iliyopita kwamba unyonyaji wa Ufaransa ndo chanzo cha kuongezeka wahamiaji kule ulaya kutoka Afrika Magharibi na akasema suluhisho kuhusu tatizo la uhamiaji ni kuziokoa nchi za Afrika Magharibi kutoka kwenye mikono ya Ufaransa. Video zake akielezea hilo jambo ziko tele YouTube kama unahitaji. Kwahiyo na waziri mkuu wa Italia tuseme na yeye anaeneza propaganda dhidi ya Ufaransa?
 
Back
Top Bottom