Rais Macron aituhumu Urusi kuchafua jina la Ufaransa barani Afrika

Rais Macron aituhumu Urusi kuchafua jina la Ufaransa barani Afrika

Duh!, Ni zipi gizo?
Zile alizozotawala kule Afrika Magharibi ukitoa Guinea na hizi zilizofanya mapinduzi karibuni. Kuna mikataba ya uhuru walilazimishwa kusaini. Sekhou Toure wa Guinea peke yake ndo aligoma, alivyogoma Rais Charles de Gaulle akawaambia waharibu Kila kitu walichojenga ndo waondoke. Walioharibu hadi vijiko, hata banda la mabanzi waliharibu. Waliharibu barabara yaani kila kitu. Kaitafute hiyo mikataba usome .Usipolia basi wewe ni jiwe sio binadamu
 
Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron ameituhumu nchi ya Urusi kutumia mitandao ya kijamii kuchafua jina la Ufaransa barani Afrika.

Rais Macron alisema maneno hayo tarehe 6 Januari 2025 wakati akiwahutubia wanadiplomasia wa Ufaransa wanaohudumu nje ya nchi hiyo.

Akiongelea swala la kupungua ushawishi wa Ufaransa barani Afrika katika miaka ya hivi karibuni, Rais Macron alisema propaganda zinazoenezwa na Urusi kuhusu nchi yake kwenye mitandao ya kijamii ndio chanzo cha kupungua kwa ushawishi wa Ufaransa.

Vile vile, alisema wanaharakati wa Afrika wanaofahamika kama Pan Africanists ambao wana ushawishi mkubwa kwenye mitandao ya kijamii,hutumia kete ya kupinga ukoloni kuchafua taswira ya Ufaransa.

Miongoni mwa Pan Africanists hao ni Bibi Nathalie Yamb kutoka nchini Niger na Bwana Kemi Seba kutoka nchini Benin ambao mwaka 2023 Rais Macron aliwaita " waajiriwa wa Putin"

Source: FRANCE 24

Kemi Seba

Kémi Séba, whose real name is Stellio Gilles Robert Capo Chichi, is a prominent Pan-Africanist activist and political leader from Benin2. He is known for his strong opposition to French influence in Africa and his advocacy for African sovereignty. Séba has been involved in various movements and organizations, including the Nation of Islam and the New Black Panther Party2. He has also faced legal issues and controversies, particularly related to his anti-Semitic remarks and ties to pro-Russian networks3.
Recently, Kémi Séba announced his candidacy for the 2026 presidential election in Benin5. He aims to challenge the current administration and address issues such as economic inequality and foreign influence in the country5.
source: COPILOT
 
Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron ameituhumu nchi ya Urusi kutumia mitandao ya kijamii kuchafua jina la Ufaransa barani Afrika.

Rais Macron alisema maneno hayo tarehe 6 Januari 2025 wakati akiwahutubia wanadiplomasia wa Ufaransa wanaohudumu nje ya nchi hiyo.

Akiongelea swala la kupungua ushawishi wa Ufaransa barani Afrika katika miaka ya hivi karibuni, Rais Macron alisema propaganda zinazoenezwa na Urusi kuhusu nchi yake kwenye mitandao ya kijamii ndio chanzo cha kupungua kwa ushawishi wa Ufaransa.

Vile vile, alisema wanaharakati wa Afrika wanaofahamika kama Pan Africanists ambao wana ushawishi mkubwa kwenye mitandao ya kijamii,hutumia kete ya kupinga ukoloni kuchafua taswira ya Ufaransa.

Miongoni mwa Pan Africanists hao ni Bibi Nathalie Yamb kutoka nchini Niger na Bwana Kemi Seba kutoka nchini Benin ambao mwaka 2023 Rais Macron aliwaita " waajiriwa wa Putin"

Source: FRANCE 24
Nathalie Yamb is a Cameroonian-Swiss activist and businesswoman known for her strong opposition to French influence in Africa. She was born on July 22, 1969, in La Chaux-de-Fonds, Switzerland, and grew up in Cameroon. Yamb has been a vocal critic of what she describes as neo-colonialism by France in Africa2.

She has been involved in various political activities and was deported from Ivory Coast in 2019 after criticizing the government at a conference in Russia. Yamb has also been associated with Russian oligarch Yevgeny Prigozhin and has participated as an "independent international observer" during controversial referendums in Eastern Ukraine1.

Yamb remains active on social media, where she continues to advocate for African sovereignty and self-determination.
SOURCE : COPILOT
 
Angefunga mdomo wake tu, Waafrika wengi na hata wazalendo uchwara wana taswira mbaya sana na ukoloni wa Ufaransa
Yeah!... mapinduzi ya mara kwa mara na machafuko kwenye nchi zilizokuwa makoloni ya Ufaransa.....yanatosha kuichafulia jina Ufaransa.
 
Yeah!... mapinduzi ya mara kwa mara na machafuko kwenye nchi zilizokuwa makoloni ya Ufaransa.....yanatosha kuichafulia jina Ufaransa.
Ufaransa haijawahi kuwa na sifa zozote kwenye makoloni yake zaidi ya unyonyaji.
 
Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron ameituhumu nchi ya Urusi kutumia mitandao ya kijamii kuchafua jina la Ufaransa barani Afrika.

Rais Macron alisema maneno hayo tarehe 6 Januari 2025 wakati akiwahutubia wanadiplomasia wa Ufaransa wanaohudumu nje ya nchi hiyo.

Akiongelea swala la kupungua ushawishi wa Ufaransa barani Afrika katika miaka ya hivi karibuni, Rais Macron alisema propaganda zinazoenezwa na Urusi kuhusu nchi yake kwenye mitandao ya kijamii ndio chanzo cha kupungua kwa ushawishi wa Ufaransa.

Vile vile, alisema wanaharakati wa Afrika wanaofahamika kama Pan Africanists ambao wana ushawishi mkubwa kwenye mitandao ya kijamii,hutumia kete ya kupinga ukoloni kuchafua taswira ya Ufaransa.

Miongoni mwa Pan Africanists hao ni Bibi Nathalie Yamb kutoka nchini Niger na Bwana Kemi Seba kutoka nchini Benin ambao mwaka 2023 Rais Macron aliwaita " waajiriwa wa Putin"

Source: FRANCE 24
Ukiona hivyo, Africa ni kama Malaya/kahaba mzuri anayegombaniwa. Kahaba Hana mume. Africa pia haina mtu, jasiri wa kukatalia/kuwagomea wazungu kuchota mali zetu. My dear Africa is openly robbed.
 
Zile alizozotawala kule Afrika Magharibi ukitoa Guinea na hizi zilizofanya mapinduzi karibuni. Kuna mikataba ya uhuru walilazimishwa kusaini. Sekhou Toure wa Guinea peke yake ndo aligoma, alivyogoma Rais Charles de Gaulle akawaambia waharibu Kila kitu walichojenga ndo waondoke. Walioharibu hadi vijiko, hata banda la mabanzi waliharibu. Waliharibu barabara yaani kila kitu. Kaitafute hiyo mikataba usome .Usipolia basi wewe ni jiwe sio binadamu
Robo mbaya kweli.
 
Nawaza na wasiwasi wanguje hizo nchi zinaweza kujitegemea zenyewe kweli? Nchi nyingi za africa ukiachana na south afrika bado ni omba omba zinategemea pesa kutoka kwa wahisani je waowakimuacha mfaransa nani atawasaidia?
Wewe ni mpumbavu 🚮
 
Nchi Gani labda imewahi kusaidiwa na Ufaransa na ilisadiwaje? Ungejua Ufaransa ndio haiwezi kusurvive bila Afrika hata usingeongea. Kwani Ufaransa ina nini hasa ambacho Afrika inahitaji?
Sasa mbona Ufaransa ina maendeleo kuliko nchi ambazo unadai zina kila kitu na ambayo haina kitu ina maendeleo makubwa ?
 
Hata Urusi asipoeneza propaganda kwani ukweli haujulikani? Kwani inahitaji uwepo wa Urusi kujua kwamba Ufaransa waliua watu kwa majaribio ya mabomu ya nyuklia kule Algeria? Inahitajika propaganda za Urusi kujua kwamba Ufaransa walimuua Thomas Sankara ? Inahitajika propaganda za Urusi kujua kwamba Ufaransa alikuwa anachota uranium ya bure pale Niger? Hata waziri mkuu wa Italia alisema hili jambo miaka 5 iliyopita kwamba unyonyaji wa Ufaransa ndo chanzo cha kuongezeka wahamiaji kule ulaya kutoka Afrika Magharibi na akasema suluhisho kuhusu tatizo la uhamiaji ni kuziokoa nchi za Afrika Magharibi kutoka kwenye mikono ya Ufaransa. Video zake akielezea hilo jambo ziko tele YouTube kama unahitaji. Kwahiyo na waziri mkuu wa Italia tuseme na yeye anaeneza propaganda dhidi ya Ufaransa?
Naomba jina la Mfaransa aliye muua Thomas Sankara.
 
Sasa mbona Ufaransa ina maendeleo kuliko nchi ambazo unadai zina kila kitu na ambayo haina kitu ina maendeleo makubwa ?
Ufaransa ilipataje hayo " maendeleo yake"? Jiulize.Nitakutolea mfano. Kabla ya mapinduzi ya Niger yaliyotokea 2023, Ufaransa ilikuwa inaingiza mabilioni ya Dollar kwa kuuza umeme kwenye nchi nyingine za Ulaya. Lakini Ili kupata huo umeme walikuwa wanabeba Uranium ya bure pale Niger wanapeleka kwao kwenye vinu vya Nyuklia wanatumia kuzalisha umeme wa uhakika kutumia kwenye nchi yao mwingine wanauza. Tangu mapinduzi ya Niger yatokee, hakuna Uranium imepelekwa Ufaransa. Matokeo yake, shirika la Ufaransa la Orano linalohusika na hayo masuala ya umeme limepata hasara balaa hadi serikali ikawapa ruzuku. Bei ya umeme imepanda na kodi inayotozwa kwenye gesi ya kupasha moto majumbani imeongezeka ( Takwimu Na taarifa zipo Google ukizitaka kuthibitisha )Sasa hapo unasema Ufaransa imeendelea au ni mwizi mzoefu ambae hawezi kuishi bila kuiba ? Swala sio maendeleo suala ni bila wizi angeendelea ? Au hukumuona Macron alivyokuwa anaongea kama mwehu baada ya kusikia kibaraka wake katolewa pale Niger. Alikuwa kabisa ugali wa bure unaondoka. Ndio maana hata ECOWAS walikuwa kimbelembele kwenda kuivamia Niger kisa mapinduzi wakati kwenye nchi za Afrika Magharibi mapinduzi ni kitu cha kawaida. ECOWAS walikuwa wanatetea ugali wa Ufaransa pale.

Je unajua hizo nchi za Afrika Magharibi zilizotawaliwa na Ufaransa zinatumia pesa zinazochapishwa Ufaransa na zinalazimishwa kutunza pesa kwenye Benki kuu ya Ufaransa na wakizitaka wanapewa kama mikopo na riba juu? Unajua ni kiasi gani cha pesa Ufaransa wanaingiza kwa kulazimisha hayo makoloni kutumia hiyo sarafu ya CFA Francs? Mifano ni mingi inahitaji uzi mwingine kuelezea Ufaransa anavyoyanyonya makoloni yake ya zamani hadi leo.Ufaransa kaendelea kwa sababu kawaibia halafu wao wameshindwa kumuibia. Upo?
 
Naomba jina la Mfaransa aliye muua Thomas Sankara.
French secret services wakishirikina na Blaise Compaoré ( msaliti). Kama ambavyo NATO walimuua Gaddafi tena hao Ufaransa ndo walipeleka silaha kwa wale waasi wa Libya.Au kama ambavyo Ubelgiji na CIA walivyomuua Patrice Lumumba.
 
Licha kwamba sipendi tabia ya kutembeza bakuri ughaibuni lakini jamaa ana hoja ni taifa gani Afrika ambalo sio omba omba ?
Kuomba ni sababu ya kujiendekeza wizi,rushwa,ufisadi n.k . Yaani tuna Kila kitu tumeshindwa kutumia wenyewe. Tuna mito na maziwa lakini eti tuna shida ya maji hadi leo.
 
Ufaransa ilipataje hayo " maendeleo yake"? Jiulize.Nitakutolea mfano. Kabla ya mapinduzi ya Niger yaliyotokea 2023, Ufaransa ilikuwa inaingiza mabilioni ya Dollar kwa kuuza umeme kwenye nchi nyingine za Ulaya. Lakini Ili kupata huo umeme walikuwa wanabeba Uranium ya bure pale Niger wanapeleka kwao kwenye vinu vya Nyuklia wanatumia kuzalisha umeme wa uhakika kutumia kwenye nchi yao mwingine wanauza. Tangu mapinduzi ya Niger yatokee, hakuna Uranium imepelekwa Ufaransa. Matokeo yake, shirika la Ufaransa la Orano linalohusika na hayo masuala ya umeme limepata hasara balaa hadi serikali ikawapa ruzuku. Bei ya umeme imepanda na kodi inayotozwa kwenye gesi ya kupasha moto majumbani imeongezeka ( Takwimu Na taarifa zipo Google ukizitaka kuthibitisha )Sasa hapo unasema Ufaransa imeendelea au ni mwizi mzoefu ambae hawezi kuishi bila kuiba ? Swala sio maendeleo suala ni bila wizi angeendelea ? Au hukumuona Macron alivyokuwa anaongea kama mwehu baada ya kusikia kibaraka wake katolewa pale Niger. Alikuwa kabisa ugali wa bure unaondoka. Ndio maana hata ECOWAS walikuwa kimbelembele kwenda kuivamia Niger kisa mapinduzi wakati kwenye nchi za Afrika Magharibi mapinduzi ni kitu cha kawaida. ECOWAS walikuwa wanatetea ugali wa Ufaransa pale.

Je unajua hizo nchi za Afrika Magharibi zilizotawaliwa na Ufaransa zinatumia pesa zinazochapishwa Ufaransa na zinalazimishwa kutunza pesa kwenye Benki kuu ya Ufaransa na wakizitaka wanapewa kama mikopo na riba juu? Unajua ni kiasi gani cha pesa Ufaransa wanaingiza kwa kulazimisha hayo makoloni kutumia hiyo sarafu ya CFA Francs? Mifano ni mingi inahitaji uzi mwingine kuelezea Ufaransa anavyoyanyonya makoloni yake ya zamani hadi leo.Ufaransa kaendelea kwa sababu kawaibia halafu wao wameshindwa kumuibia. Upo?
Asante kwa maelezo mengi lakini swali langu hauja jibu zaidi umetoa lawama tu kwa ufaransa.

Nchi zenye kila kitu za Afrika zimeshindwaje kuendelea kuliko nchi ambayo haina kitu ya Ufaransa? Kama Ufaransa ni mwizi shida Iko kwa anaye ibiwa kushindwa kutengeneza mazingira ya kuto hibiwa.

Nani kapiga marufuku bank za mataifa hayo kukwepa mtengo wa wafaransa ? Unaweza nipa takwimu ya hali ya maisha ya wananchi ya Niger Iko vipi licha ya kuwa na rasilimali muhimu za kuleta mageuzi.
 
French secret services wakishirikina na Blaise Compaoré ( msaliti). Kama ambavyo NATO walimuua Gaddafi tena hao Ufaransa ndo walipeleka silaha kwa wale waasi wa Libya.Au kama ambavyo Ubelgiji na CIA walivyomuua Patrice Lumumba.
Nipe jina\Majina ya hao France Secret service walio fanya mauaji kwa Thomas Sankara ?

Walio fanya mauaji ya kanali Gaddafi sio NATO ni Walibya wenyewe kama sio Walibya kama unavyo dai thibitisha kwamba walio mpiga risasi Gaddafi ni NATO

Walio muua Patrice Lumumba ni Wacongomani wenyewe wabelgiji na CIA wanapewa lawama za Bure lakini ni mwafrika ndo alimuua Patrice Lumumba
 
Asante kwa maelezo mengi lakini swali langu hauja jibu zaidi umetoa lawama tu kwa ufaransa.

Nchi zenye kila kitu za Afrika zimeshindwaje kuendelea kuliko nchi ambayo haina kitu ya Ufaransa? Kama Ufaransa ni mwizi shida Iko kwa anaye ibiwa kushindwa kutengeneza mazingira ya kuto hibiwa.

Nani kapiga marufuku bank za mataifa hayo kukwepa mtengo wa wafaransa ? Unaweza nipa takwimu ya hali ya maisha ya wananchi ya Niger Iko vipi licha ya kuwa na rasilimali muhimu za kuleta mageuzi.
Kinachotokea ni kwamba Ufaransa akishirikiana n'a baadhi ya wanasiasa ambao ni chini ya asilimia kumi ya watu wanahakikisha hizo nchi haziendelei. Raia wa kawaida wenyewe watajinasuaje kwenye huo mtego? Na endapo akitokea kiongozi mwaminifu Ufaransa wanahakikisha huyo kiongozi anayeyushwa chap. Ndio maana kwenye kila koloni lake huko Afrika Magharibi kuna kambi ya kijeshi ya Ufaransa. Na kuhusu Niger, hivi wewe nikikuibia kila kitu halafu nikakuuliza mbona hauendelei utanielewaje? Niger wana raslimali lakini haiendelei kwa sababu hizo raslimali zinaishia Ufaransa tena kwa bei sawa na bure. Kwahiyo hapo wanaouhusika kwanza kabisa ni viongozi wasaliti wakishirikina na mwajiri wao ufaransa.
 
Nipe jina\Majina ya hao France Secret service walio fanya mauaji kwa Thomas Sankara ?

Walio fanya mauaji ya kanali Gaddafi sio NATO ni Walibya wenyewe kama sio Walibya kama unavyo dai thibitisha kwamba walio mpiga risasi Gaddafi ni NATO

Walio muua Patrice Lumumba ni Wacongomani wenyewe wabelgiji na CIA wanapewa lawama za Bure lakini ni mwafrika ndo alimuua Patrice Lumumba
My friend, my friend, my friend. Hata wakati jino la Patrice Lumumba linarudishwa kiongozi wa Ubelgiji aliyehutubia alikiri Ubelgiji ilihusika kumuua Patrice Lumumba na aliomba msamaha kwa familia ya Patrice Lumumba. Tena vidéos hadi leo zipo YouTube. Na kuhusu CIA, weka bando ingia online tafuta opération zilizofanywa na CIA kutoa madarakani viongozi wasiowapenda hapa Afrika na vizuri zaidi tumia Rumble badala ya YouTube maana YouTube sasahivi kuna namna taarifa kama hizi wanafanya isiwe rahisi kupata viewers.Ukilikosa jina la Patrice Lumumba nakusubiri hapa. Ni kama mimi nitume majambazi wakamuue mtu halafu niseme sijamuua waliomuua ni majambazi niliowatuma.
Halafu hayo majina ya secret services waliohusika kumuua Thomas Sankara unategemea mimi ninayo😂😂😂😂.
 
Ndio naanza kwanini nchi zilizokuwa zinatawaliwa na France/Belgium zilikimbilia Commonwealth mfano Check Rwanda then angalia Burundi na ndugu yake Drc na huyo Central Africa
 
Back
Top Bottom