Rais Magufuli aagiza daraja la Busisi limalizike kwa miaka 3 na sio 4. Awataka Wananchi kuongeza kulima

Tundu Lissu ni alama ya upinzani, kakosoa miradi mingi lakini ili Daraja sijawahi msikia. Sasa uchambuzi wako umeenda mbali Mkuu. Hongera
 
Usikariri; kila anaetetea kitu chochote hua mnadhani either ni wa huko au ni mwana ccm, sina vyote; mimi ni Mhehe wa Iringa, nimejenga Kigamboni. Upo hapo, naongelea muktadha wa kiuchumi. Nimetembea hi nchi almost mikoa yote so barabara zote kubwa za Tanzania ninazifahamu either kwa kupanda magari na dereva mwingine akiiendesha or nimeendesha mwenyewe, so hunidanganyi popote kuhusu barabara za Bongo. Hizo barabara zote ulizozitaja Bahati mbaya au nzuri nimepita, nikukumbushe tena, nimeolea Kigoma kwa kina Zitto Kabwe so najua barabara ya Kigoma via Kibondo, najua barabara ya Kigoma via Tabora, naifahamu pia barabara ya Tabora to Mbeya via Tabora. Coming back to your point; kwenye biashara kuna kitu tunaita time; hivi umewahi kweli kuvuka kupitia hicho kivuko cha Busisi au unaongea tu mkuu? Serikari imejitahidi sana kuweka vivuko vikubwa na vizuri, Mkapa alinunua though alizundua Kikwete, Kikwete nae alinunua kipya though alizindua Magufuli, vinafanya kazi vyote but ikitokea breakdown kimoja wapo, mnakaa ng'ambo nyingine Zaidi ya saa 2, wagonjwa wanao takiwa kwenda hospitali za rufaa wanaweza kufia njiani, wanaotaka kwenda na kurudi Mwanza kutoka hizo sehemu nilizozitaja mwanzoni nao wanweza wasifanikiwe. Labda nikuulize swali, hivi wakati daraja la Kigamboni (to me bado nasisitiza Kigamboni halikua lazima sana kujengwa though ni la muhimu ) tulipiga kelele kwamba why Kigamboni na sio barabara? Wengi mnaopinga ujenzi wa daraja hilo mnahusisha ujenzi wake na unyumbani wa mhe raisi na sio vinginevyo. Daraja la Busisi ni muhimu sana kwa uchumi wetu. Ningekuona unaongea point za maana kama ungeizungumzia sana barabara ya kwenda Ngara to Rwanda eneo la Rusahunga, yale ni mahandaki and is almost 81 km unatembea kwenye mahandaki. Moja kati ya sababu ya Rwanda kupitishia baadhi ya mizogo yake bandari ya Mombasa ni ubovu wa hicho kipande, tuongelee uchumi wa Tanzania na sio chuki na mapenzi ya mhe rais na nyumbani kwao.
 
Unaongea blaa blaa mingi saaaana,nimeuliza swali dogo wewe kutumia bln 700 kwa hicho kidaraja na kujenga km 700 za lami kipi ni chenye maana kwa Taifa?

Sasa nani unadhani hajavuka au kupanda hicho kiferry cha kigongo busisi? Kuvuka hapo kwa maji ni wastani wa 30 minutes by the time nilivuka ilikuwa 2014.Sasa hiyo nusu saa ndio inaua wagonjwa gani maana wagonjwa wa rufaa mara chache wanakuwa wa dharura afu vivuko hapo viko 2..Kwani kuna shida gani wakiviongezea speed Ili kupunguza muda badala ya kupoteza bln 700 kwa kidaraja cha maonyesho?

Kwa taarifa yako hiyo bln 700 ni vituo vya Afya 1400 hivi vinavyojengwa na akina Jafo kwa mil.500 au sawa na hospital za wilaya 70 kwa bln 10 ,pia ni sawa na hospital za rufaa za mikoa 10 Kila moja kwa 70 bln..Hayo yangefanyika mambo ya rufaa yangeishia huko huko Sengerema au Geita..Hiyo ndio hasara ya kutotumia akili vizur

Daraja la Kigamboni lilikuwa linatoa relief ya kutoa mizigo kwa uharaka bandarini afu gharama yake ni nafuu yaani nusu tu ya hilo la mwanza.Ukweli ndio huo linajengwa huko kwa sababu za kinyumbani kwamba nitakumbukwa kama tu lireli la sgr
 
Anataka liishe mapema ili alifunguae yeye na kulipa jina lake "daraja la Magufuli"
 
Hilo Daraja ni muhimu sio kwa uchumi wa nchi tu hasa Ukanda wa ziwa. Nchi za maziwa Makuu ukiongelea Uganda, Eastern Congo DRC, Rwanda na Burundi zinategemea njia mbili yaani central na northern corridor na Kenya anategemea zaidi Northern corridor, kukamilika kwa daraja kutafupisha umbali wa safari kwa mizigo kutoka Mashariki ya Congo kupitia bandari ya Mombasa, kuungana na nchi za mashariki ya kati na mbali kupitia bandari za DSM na Mombasa. Uwepo wa Daraja hili utapunguza umbali wa usafirishaji kwa kuunganisha Bandari ya Mombasa ambayo ndio lango la Northern corridor na nchi kama Congo na Rwanda, Burundi kama njia fupi zaidi kuliko hiyo ya Northern corridor. Itaongeza wingi wa transit goods kutoka na kwenda bandari ya Mombasa Kupitia Musoma, Mwanza, Geita, na Mwisho Rwanda/ Burundi / Congo DRC.

Najua tunafahamu sekta ya usafirishaji inavyokuza uchumi kuanzia kwenye matumizi ya mafuta, vipuri, huduma za msingi kama chakula na maradhi, kuongezeka kwa masoko ya bidhaa kwenye transit corridor. Hili daraja litapunguza mizigo na idadi ya malori yaliyokuwa yanaenda Rwanda/ Burundi / Congo kupitia Uganda na njia ya Kigongo Busisi itaongeza fursa hizo za kibiashara.

Kila liter 1 moja ya mafuta serikali ina TZS 52 kwa ajili ya mfuko wa barabara, kama sijakosea bado 18% ya VAT, Ewura. Unadhani nchi itaingiza TZS kwa kila leo kupitia usafirishaji wa Kigongo Busisi? Na bado magari kuvuka yatakuwa yanachajiwa kama ilivyo kwa daraja la Kigamboni

Billion 700 kitu gani bhuana kama return inaonekana kwa serikali na kwa wananchi?
 
Barabara ipi ambayo haina mkandarasi kwasasa mkuu? Nimekuuliza, wakati daraja la Kigamboni linajengwa, kuna mtu alidai lisijengwe kwasababu hakuna vituo vya afya au hizo barabra unazo zisema? Labda twende nyumbani kidogo; una pesa kiasi fulani, labda mwezi December, utaacha kuwanunulia watoto wako nguo za sikukuu tu kwasababu hujamaliza kupaua nyumba yako? Unajiita Opportunity cost, hivi unaelewa kweli maana ya hilo jina lako? Magufuli anaweza kulaumiwa kwa vitu vingine but sio vituo vya afya, miundombinu/barabara. Halafu, kuna barabara bila madaraja????? Remember, nimesema, Tanzania hi hakuna barabara kubwa sijapita, almost zote zina wakandarasi wanaendelea na KAZI so what's your point here brother?
 
Bado sijajua faida za hili saraja but nadhan inaweza kua ni moja kati ya miradi itayokufa punde tuu baada ya mheshimiwa Kuondoka
 
Bado sijajua faida za hili saraja but nadhan inaweza kua ni moja kati ya miradi itayokufa punde tuu baada ya mheshimiwa Kuondoka
Mkuu kati ya miradi ambayo Mimi ukiniuliza ni ipi iendelezwe na rais Samia nitakutajia huu mradi,

Mwaka Jana nikiwa naenda kwa majukumu Yangu nilishuhuhudia baba mmoja akipoteza uhai kisa kaachwa na kivuko ili kiweze kumfikisha ngambo na baadae apelekwe bugando,nilipoteza pia Mwalimu wangu ambaye alipata ajali ya pikipiki hivyo akapewa referral ya kwenda bugando,naye kutokana na matatizo ya kivuko alipoteza Maisha kwani alikuwa anavuja damu nyingi sana.Nina matukio mengi sana ya kukueleza ila basi tu,

Watu Wa kanda ya ziwa wanajua umuhimu Wa mradi huu katika Maisha yao ya kila siku.

Serikali Yangu ya ccm isiutelekeze tafadhari
 
Hili daraja Samia atalimaza Tu Alafu 2024 tunaanza la Zanzibar
 
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…