Joyce Ndalichako, alikuwa katibu wa baraza la mitihani. Alishutumiwa na Waislamu kuwafelisha.
Nikiwa mwandishi wa habari za uchunguzi nililifuatilia suala hili na kulithibitisha.
Utetezi wake haukuwa na mashiko hata chembe.
Malalamiko ya Waislamu yalisababisha Rais Kikwete kumuondoa barazani.
Lakini leo hii Dk. John Pombe Magufuli amemteua kuwa Waziri wa Elimu. Tena kwanza amemteua kuwa mbunge kisha ndio kampa uwaziri.
Kuna wakati namuelewa Rais Magifuli lakini wakati mwingi napata shida kumuelewa.
Kuwapa uwaziri wenye tuhuma na wengine walioondolewa madarakani kuwarudisha mapata shida kidogo. Sijui dharau kwa Wananchi au haamini kama wanamakosa.
Mpaka sasa Rais ameshateua watu zaidi ya wanne kuwa wabunge na kuwapa uwaziri, sasa sijui wabunge alionao kwenye ccm hawaamini au laa.
Ngoja niendelee kusubiri labda nitamuelewa.
Mwandishi Mwanahalisi.