Rais Magufuli akamilisha uteuzi wa Baraza la Mawaziri, Makame Mbarawa abadilishiwa Wizara

Rais Magufuli akamilisha uteuzi wa Baraza la Mawaziri, Makame Mbarawa abadilishiwa Wizara

Jpm usipoangalia lile jina watu wengi hususan washindani wako,yaan jina la "Wakukurupuka"litapita.Licha ya kusubir baraza lako la mawazir kwa muda mrefu,uliopokuja kutangaza baraza la mawazir halikukidhi ama kulandana na kas yako kwa kuwaweka mawazir waliokuwa na kashfa na wengine mavuvuzera tu,pamoja na uteuz huo ulikosa wabunge wa ccm wanaofaa kuwa na wewe kias cha nafac zingine kuwa waz.Nafas umezijaza kwa kuchagua/kuteua mawazir mizigo huku ukipangua baraza lako tena hii inaonesha una maamuz ya kukurupuka na ndio maana washindan wako wanakuita "Wakukurupuka"
 
Uteuzi wa Dr Joyce Ndalichako ni uteuzi bora hasa kutokana na taaluma yake kuendana na wizara aliyopewa.

Lakini Dr.Ndalichako anachangamoto kubwa ya kuaminiwa na Jamii ya waislaam Tanzania kama atatenda haki akiwa wizarani.

Mtakumbuka kuwa akiwa Katibu Mkuu wa Baraza la Mitihani alituhumiwa na Waislaam kuwa alihusika kuwafelisha vijana wao kwa makusudi na walipofuatilia kujua kwanini wamefeli,Dr.Ndalichako alitoa matokeo mapya haraka matokeo ambayo yaliakisi madai ya waislaam.


Kwa maoni yangu ,Ndalichako atapata changamoto kubwa katika utendaji wake kutokana na Dosari iliyomkabili kipindi hicho.

Ukiachana na hilo Dr Ndalichako ni Mchapa kazi na Mtu ambae anaweza kuleta mageuzi makubwa katika sekta ya Elimu.

Kila la kheri Dr Joyce Ndalichako,huu ni wakati wa kuonyesha weledi wako na uadilifu wako kwa Rais na watanzania.
 
Joyce Ndalichako, alikuwa katibu wa baraza la mitihani. Alishutumiwa na Waislamu kuwafelisha.

Nikiwa mwandishi wa habari za uchunguzi nililifuatilia suala hili na kulithibitisha.

Utetezi wake haukuwa na mashiko hata chembe.
Malalamiko ya Waislamu yalisababisha Rais Kikwete kumuondoa barazani.

Lakini leo hii Dk. John Pombe Magufuli amemteua kuwa Waziri wa Elimu. Tena kwanza amemteua kuwa mbunge kisha ndio kampa uwaziri.

Kuna wakati namuelewa Rais Magifuli lakini wakati mwingi napata shida kumuelewa.

Kuwapa uwaziri wenye tuhuma na wengine walioondolewa madarakani kuwarudisha mapata shida kidogo. Sijui dharau kwa Wananchi au haamini kama wanamakosa.

Mpaka sasa Rais ameshateua watu zaidi ya wanne kuwa wabunge na kuwapa uwaziri, sasa sijui wabunge alionao kwenye ccm hawaamini au laa.

Ngoja niendelee kusubiri labda nitamuelewa.

Mwandishi Mwanahalisi.

Wewe utakua muislam walahi,wahahi..mwandishi kanjanja
 
Yule msukuma nae hajapewa?,watu waliongea mpaka makoo yakapata sugu,wangempa hata umwenyekiti wa FAT,
 
alitaka kubalance kaskazini kwani mlilalamika sana.ila najua interest ya magufuri ni hao manaibu kwanza wapate uzoefu

Kweli mkuu kuna mawazili wengine sidhani hata mwaka kama utapita maana walishazoea upigaji hawa nadhani jpm kaamua kujivua lawama kwani wataijiondoa wenyewe.
Kwa bunge hili la vijana wenye damu changa.
Sijui kama watahimili vishindo.
 
Mchawi mpe mtoto wako akulelee, waislam mchawi ashajulikana, there no need to worry now!
 
Ndalichako atakuwa makini sana na waislamu now! Amejifunza naamin
 
Mimi chochote atakacho fanya magufuli naunga mkono maana sisi wananchi wa chini tumenyanyasika saaana kwa mambo ya kichuki chuki tu na sio ya kiutendaji.WAISLAMU WANAPENDA KULALAMIKA SANA,WAFANYIE WAISLAM NA WAKRISTO JAMBO LA KUUMIZA KWA LEVEL SAWA,WAISLAM WATATOA MPAKA MATAMKO YA KULAANI,LAKINI WAKROSTO WATAMWACHIA MUNGU,ndo ilivyotokea kwa ndalichako,pamoja na albadri na laana zao bado ndalichako alimwachia MUNGU
 
Eti magembe amepewa maliasili!!! JPM imekuaje tena hapa umeenda chaka kabisa ....au umekosea
Lakini si amesomea mambo hayo hayo - misitu misitu,wanyama wanyama,mimea mimea nk, kwani tatizo liko wapi - kwa binadamu ambao hawana makuu na kujisikia basi Prof.Maghembe ni mmoja wapo,usikivu wake na kuheshimu binadamu wenzake kutamsaidia kufanya kazi kwa karibu na Dk.Maghufuli, hapo naona Rais amepatia sana - ila kwa Prof.Mbalawa naona ingekuwa vizuri kama angerudishwa kufundisha vyuo Vikuu - masuala ya Serikalini niliona wajanja walikuwa wanamzidi kete sana!

Wizara ya Mawasiliano chini ya Mbalawa it was a very sad story kusema kweli - makampuni ya simu yalipewa a leeway kupindukia, yaliendesha puta Wizara yenyewe na TCRA - kampuni hizi za simu Nchini zisijifanye kama Serikali imekwenda likizo inakuwaje nchi ndogo kama Rwanda ikusanye kodi kubwa kutoka makampuni ya simu ambayo hayazidi mawili sisi hapa wenye makampuni ya simu lukuki tunakusanya peanut!!!

Serikali yetu inapaswa kufanya tafiti kwa wenzetu Kenya na Rwanda ili wapate mbinu za kudhibiti ulipaji kodi stahiki,Nchi hizo zimefanikiwa sana kubana Makampuni ya simu,sisi hapa Wizara na TCRA walikuwa wana angahikia sana masuala ya semina elekezi,kuchapisha vipeperushi,study tour zisizo kuwa na kichwa wala miguu, kuipigia debe ViaTel na HaloTel,wakahisahau kabisa TTCL!! Makosa hayo yasirudiwe tena.
 
Kati ya mawazir ambao Jpm hahitaj kuwauliza,ambao wanajiongeza wenyewe ni wawil tu Dr.Ndalichako na Dr.Mahiga,sasa huyu maghembe moja ya mawazir mizigo waliotajwa kwenye serikal ya jk!budget yake mara mbili ilitishiwa kutopitishwa,proffesow wa nyuki duuh.
 
Uteuzi wa Dr Joyce Ndalichako ni uteuzi bora hasa kutokana na taaluma yake kuendana na wizara aliyopewa.

Lakini Dr.Ndalichako anachangamoto kubwa ya kuaminiwa na Jamii ya waislaam Tanzania kama atatenda haki akiwa wizarani.

Mtakumbuka kuwa akiwa Katibu Mkuu wa Baraza la Mitihani alituhumiwa na Waislaam kuwa alihusika kuwafelisha vijana wao kwa makusudi na walipofuatilia kujua kwanini wamefeli,Dr.Ndalichako alitoa matokeo mapya haraka matokeo ambayo yaliakisi madai ya waislaam.


Kwa maoni yangu ,Ndalichako atapata changamoto kubwa katika utendaji wake kutokana na Dosari iliyomkabili kipindi hicho.

Ukiachana na hilo Dr Ndalichako ni Mchapa kazi na Mtu ambae anaweza kuleta mageuzi makubwa katika sekta ya Elimu.

Kila la kheri Dr Joyce Ndalichako,huu ni wakati wa kuonyesha weledi wako na uadilifu wako kwa Rais na watanzania.
vijana walikua wamefaulu,yeye akaja na matokeo ya kwake,liliposanuka akarudisha matokeo halisi na ikabidi aachie ngazi,
 
Joyce Ndalichako, alikuwa katibu wa baraza la mitihani. Alishutumiwa na Waislamu kuwafelisha.

Nikiwa mwandishi wa habari za uchunguzi nililifuatilia suala hili na kulithibitisha.

Utetezi wake haukuwa na mashiko hata chembe.
Malalamiko ya Waislamu yalisababisha Rais Kikwete kumuondoa barazani.

Lakini leo hii Dk. John Pombe Magufuli amemteua kuwa Waziri wa Elimu. Tena kwanza amemteua kuwa mbunge kisha ndio kampa uwaziri.

Kuna wakati namuelewa Rais Magifuli lakini wakati mwingi napata shida kumuelewa.

Kuwapa uwaziri wenye tuhuma na wengine walioondolewa madarakani kuwarudisha mapata shida kidogo. Sijui dharau kwa Wananchi au haamini kama wanamakosa.

Mpaka sasa Rais ameshateua watu zaidi ya wanne kuwa wabunge na kuwapa uwaziri, sasa sijui wabunge alionao kwenye ccm hawaamini au laa.

Ngoja niendelee kusubiri labda nitamuelewa.

Mwandishi Mwanahalisi.

Hapa na wewe unayejiita mwandishi wa Mwanahalisi umeonyesha udhaifu mkubwa. Unajua mchakato wa usahihishaji ulivyo? Au hujashughulisha kalamu yako kufuatilia hili?
Lkn sishangai, maana ktk nchi hii ili uwe mwandishi wa habari sifa ya kwanza lazima uwe umekosa pa kwenda kimasomo. Yaani kwa maneno rahisi sharti uwe umefeli kidato cha nne. Kwahiyo uelewa wako ni Mdogo. Halafu hivyo vyuo vyenu vya asante Kayumba vilivyochipua kama uyoga havijawanoa vema. Mtu mmoja hawezi kufelisha mwanafuzi. Kwanza dhana ya kufelisha yenyewe unaijua? Nchi hii bhana wajinga ndiyo wasemaji.
 
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amemalizia kujaza nafasi za uteuzi wa Mawaziri na Naibu Waziri alizobakiza wakati akitangaza baraza la Mawaziri la kwanza katika awamu ya tano yautawala wake


Uteuzi huo ni kama ifuatavyo;

1. Profesa Jumanne Maghembe - Ameteuliwa kuwa Waziri wa Maliasili na Utalii.

2. Dkt. Philip Mpango - Ameteuliwa kuwa Waziri wa Fedha na Mipango (Ni baada ya kumteua kuwa Mbunge).

3. Mhandisi Gerson Lwenge - Ameteuliwa kuwa Waziri wa Maji na Umwagiliaji.

4. Dkt. Joyce Ndalichako - Ameteuliwa kuwa Waziri wa Elimu,Sayansi,Teknolojia na Ufundi.(Ni baada ya kumteua kuwa Mbunge)

5. Mheshimiwa Hamad Masauni - Ameteuliwa kuwa Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi

6. Prof.Makame Mbarawa - Amehamishwa kutoka Wizara ya Maji na Umwagiliaji na kwenda Wizara ya Ujenzi, uchukuzi na Mawasiliano

Katika hatua nyingine Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amewatakia heri watanzania wote katika Sikukuu za Maulid, Christmas na Mwaka Mpya na kuwataka washerehekee kwa amani na utulivu.

Gerson Msigwa
Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano, IKULU
23 Desemba, 2015

attachment.php


aaaa!!! profesa maghembe ni yule aliolazimisha wakulima wa kahawa wauze bado shels kwa bei ya chini sasa magufuli inabidi upata mshauri
 
Hatimaye Kaskazini imetoa Mawaziri Wawili

1. Mhe. Jumanne Maghembe
2. Mhe. Angela Kairuki

Hongera Mhe. Rais Dr. JPM kwa KUJALI maeneo yote.

Queen Esther


TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amemalizia kujaza nafasi za uteuzi wa Mawaziri na Naibu Waziri alizobakiza wakati akitangaza baraza la Mawaziri la kwanza katika awamu ya tano yautawala wake


Uteuzi huo ni kama ifuatavyo;

1. Profesa Jumanne Maghembe - Ameteuliwa kuwa Waziri wa Maliasili na Utalii.

2. Dkt. Philip Mpango - Ameteuliwa kuwa Waziri wa Fedha na Mipango (Ni baada ya kumteua kuwa Mbunge).

3. Mhandisi Gerson Lwenge - Ameteuliwa kuwa Waziri wa Maji na Umwagiliaji.

4. Dkt. Joyce Ndalichako - Ameteuliwa kuwa Waziri wa Elimu,Sayansi,Teknolojia na Ufundi.(Ni baada ya kumteua kuwa Mbunge)

5. Mheshimiwa Hamad Masauni - Ameteuliwa kuwa Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi

6. Prof.Makame Mbarawa - Amehamishwa kutoka Wizara ya Maji na Umwagiliaji na kwenda Wizara ya Ujenzi, uchukuzi na Mawasiliano

Katika hatua nyingine Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amewatakia heri watanzania wote katika Sikukuu za Maulid, Christmas na Mwaka Mpya na kuwataka washerehekee kwa amani na utulivu.

Gerson Msigwa
Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano, IKULU
23 Desemba, 2015

attachment.php

 
Back
Top Bottom