Rais Magufuli akamilisha uteuzi wa Baraza la Mawaziri, Makame Mbarawa abadilishiwa Wizara

Rais Magufuli akamilisha uteuzi wa Baraza la Mawaziri, Makame Mbarawa abadilishiwa Wizara

Ila wadau naona mnamsifia mama Joisi,lakini kuna mambo lazima tuyaangalie kwa mapana
KWANZA:Joisi anakuja wizarani tayar ameshaingia kwenye siasa,nafasi anayoshika ni ya kisiasa na si ya kiutendaji teeeena,so utendaji wake utakua ni wa kisiasa siasa,ni afadhali angekua Katibu Mkuu wa Wizara.
PILI:Joisi anaingia wizarani tayar kuna sera mbovu kabisa ya elimu ya mwaka 2014,so anakuja kuitekeleza sera mboooovu kabisa ambayo ukweli haina tija kwa mustakabali wa elimu Tanzania,je ataleta maajabu chini ya sera hii?tukukumbuke hii sera imepitishwa mwaka jana tu na hata wadau weengi wa elim bado hawajaijua,hiko ni kisiki kingine.
TATU:Joisi anakuja wizarani tayari viwango vya ufaulu kwa sekondari vimeshapangwa,je atavibadili tena?je mabosi wake watakubali? Ambao ni (CCM na MAMLAKA ZA JUU YAKE).
Nne:Mtihani wa kwanza kwa Joisi ni suala la ada elekezi kwa shule binafsi,sote tunajua hizi shule binafsi nyiiingi ni za hawa tunaowaita vigogo hukohuko kwenye system,je Joisi atafanikiwa hilo?
TAno:Ili Joisi afanikiwe yule profesa pale wizarani aondolewe kwanza (Katibu mkuu wizara ya elimu) maana haendani na spidi ya serikali hii,na ni chanzo cha changamoto kadhaa,lakini poa wizara ya elimu jamani ingepaswa kuwa na manaibu wawili,hilo halikwepeki kabisa,maana kuna.mambo ya shule za awali (nasari na praimari),kuna elim sekondari,kuna vyuo vya ufundi na ualim na kuna vyuo vikuu,pagumu hapo!!!
MWisho,namtakia kila la kheri mama Joisi,lakini namkumbusha now ameshakua mwanasiasa kamili,NEKTA ilikua taasisi ndogo nowana wizara,asije kuharibu hata ya NECTA tukayasahau

Sera mbovu ikoje? Umeisoma sera hiyo mbovu?
 
Hivi kwanini wanawake kama wewe hufurahii mwanamke mwenzenu kapewa wizara kubwa hiyo?
 
uteuzi mzuri hasa alivombadilisha Prof.Makame Mbarawa kutoka maji na mumrudisha mawasiliano. Tsubiri kuona kazi sasa maana uteuzi pekee hautoshi
 
Katibu mkuu wa wizara ya elimu lazima ang'oke hataweza kwenda na kasi ya mama ndalichako. Huyu Dr Ndlichako atarudisha heshima ya elimu
 
Ndalichako aache kuleta uroma na udini uliopindukia wizarani,vinginevyo anataaluma nzuri.

Jicho la Waislaam linamfuatilia hasa kipindi hiki ambacho Ponda Issa Ponda yupo huru.

Nchi haiendeshwi kwa mihemuko ya Waislam.
 
Dr magufuli anamjua lwenge siku nyingi asingeweza kumuacha wizara ya ujenzi na uchukuzi.
 
BAKWATA Yataka Dk Joyce
Ndalichako Ajiuzulu:
Kisa Ukinyonga Katika Katokeo ya
Mitihani Form VI
BARAZA la Waislamu Tanzania
(Bakwata) limemtaka Katibu Mtendaji
wa Baraza la Mitihani (Necta), Dk
Joyce Ndalichako kujiuzulu wadhifa
huo akimtuhumu kuwafelisha mitihani
ya dini ya Kiislamu wanafunzi wa
kidato cha sita wa dini hiyo.
Kauli hiyo ya Bakwata imetolewa na
Mufti wa Tanzania, Sheikh Issa Bin
Shaaban Simba katika mkutano wake
na waandishi wa habari jijini Tanga jana
kuelezea msimamo wa Waislamu
nchini kuhusu matokeo ya kidato cha
sita, hujuma inayoandaliwa kufanyika
katika zoezi la sensa pamoja na
vurugu zilizotokea Zanzibar.
Kuhusu hujuma ya mtihani, Mufti
Simba alisema kuwa matokeo ya
mtihani ya dini hiyo ya Kidato cha Sita
yaliyotangazwa Mei Mosi 2012,
yaliwashtua wanafunzi Waislamu
waliofanya mtihani wa elimu ya dini ya
kiislamu (Islamic Knowledge), ambayo
yalionyesha kuwa asilimia 70 walifeli
kwa kupata daraja F.
Alisema matokeo hayo yalionyesha
kuwa ni asilimia 30 ndiyo waliofaulu
kwa kupata daraja D, ambapo
waliopata alama za juu kabisa nchi
nzima ni wanafunzi saba
pekee.?Matokeo haya yaliwashtua
wanafunzi na wazazi, taasisi
mbalimbali za kiislamu zilimua kukata
rufaa kuonyesha kutokubaliana na
matokeo hayo, hatimaye baraza hilo
likabaini kuwa lilikosea na likaidhinisha
kutolewa matokeo
mapya,? alisema Mufti Simba.
Tayari Ndalichako ametoa ufafanuzi
kuwa kosa lililotokea akisema si
hujuma bali ni la kiufundi lililotokana na
kubadili utaratibu wa kufanya mitihani
mitatu ya somo hilo kuwa miwili, lakini
mfumo wa ujumlishaji maksi
ulisahaulika kubadilishwa.
Ndalichako alilieleza gazeti dada la
Mwananchi, The Citizen, kuwa awali
matokeo ya mitihani mitatu yalikuwa
yanajumlishwa na kugawanywa kwa
tatu kwa kutumia mfumo wa kompyuta,
ili kupata alama rasmi za mtahiniwa,
lakini safari hii zilipojumlishwa alama
za mitihani miwili ya somo hilo
ziliendelea kugawanywa kwa tatu
badala ya mbili kimakosa.
Habari zilizopatikana kutoka Necta
zimesema kuwa baada ya kupata
malalamiko ya wanafunzi hao,
uchunguzi ulifanyika na kubaini kasoro
hiyo ambapo ilirekebishwa.Mei 30,
mwaka huu Necta ilikutana na Baraza
la Wakuu wa Shule za Kiisilamu na
kufafanua suala hilo, ambapo
ilionekana tatizo hilo si hujuma bali
kosa la kiufundi.
Mwenyekiti wa Islamic Education
Panel, Pilly H.H alimwandikia barua
Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu na
Mafunzo ya Ufundi na nakala kwa
Katibu Mtendaji wa Necta, Amir,
Jumuia na Taasisi za Kiislamu
Tanzania akishukuru wizara kwa hatua
zilizochukuliwa.
?Tunashukuru kwa jinsi Wizara ya
Elimu na mafunzo ya ufundi ilivyopokea
suala hili kwa uzito unaostahiki?Tun
atoa shukurani za pekee kwa katibu
mtendaji wa baraza la mitihani kwa
hatua alizochukua ndani ya muda
mfupi sana, nashukuru kwa
ushirikiano,? ilisema barua hiyo
iliyoandikwa na Mwenyekiti wa Baraza
la Wakuu wa Shule za Kiislamu.
Hata hivyo, akisistiza hoja yake Mufti
Simba alisema kuwa matokeo
yaliyotolewa upya yalionyesha
kwamba wanafunzi zaidi ya asilimia 70
ya wanafunzi walifaulu, jambo ambalo
Waislamu wanaamni kwamba ni
hujuma inayolenga kupunguza idadi ya
wanafunzi wa Kiislamu wa kujiunga na
vyuo vikuu.
Mufti huyo alisema jambo
lililomshangaza yeye pia pamoja na
Waislamu wote nchini ni tamko
lililotolewa na Ndalichako kupitia
vyombo vya habari Jumanne iliyopita
aliposema kuwa Baraza la Mitihani
halikukosea kutoa matokeo hayo kwa
kuwa waliosahihisha ni walimu wenye
sifa.
?Bakwata inamshangaa Katibu Mtendaji
wa Baraza la Mitihani, Ndalichako kwa
kauli yake aliyoitoa kupitia vyombo vya
habari juzi 5/6/2012 akisema hakuna
hujuma na mitihani inasahihishwa na
walimu wenye sifa na wanachaguliwa
na wakuu wa shule zao,?alisema Mufti
Simba.
Alisema hoja iliyotolewa na Ndalichako
kwamba wanaosahihisha ni wenye
uzoefu haina mashiko kwa sababu
Waisalmu wanacholalamikia ni mfumo
mzima wa ?Conveyor Belt?, aliodai
umewekwa kuwahujumu wanafunzi
Waislamu.
Alisema matokeo hayo ya mtihani wa
somo la kiislamu umeonyesha kuwa
upo wasiwasi kwamba kilichofanyika
huko ndicho wanachofanyiwa
wanafunzi wa kiislamu katika masomo
mengine kuanzia darasa la saba,
kidato cha nne na hata vyuo vikuu kwa
lengo la kupunguza idadi ya wasomi
waislamu.
?Waislamu tunaamini kwamba hila
kama hii inafanyika pia kwenye
masomo mengine, kwa maana hiyo
tunataka Ndalichako na watendaji
wengine wajiuzulu ili kuondoa kashfa
hii kwa Serikali, pia kuleta imani ya
Waislamu kwa Serikali yao, ?alisema
Mufti Simba.
Alifafanua kuwa baada ya kujiuzulu,
Serikali iunde tume ya kuchunguza
hujuma zilizotendeka katika baraza
hilo dhidi ya Waislamu kwa kipindi cha
miaka 10 iliyopita akieleza kuwa
Waislamu wanaamini kwamba
wanafunzi wengi
wamefelishwa kwa kusudi maalumu la
kuzorotesha kizazi chao.
SUALA LA SENSA YA WATU NA
MAKAZI.
Kuhusu Sensa, Mufti Simba alisema
kuwa kalenda iliyotolewa na Ofisi ya
Waziri Mkuu, takwimu zinaoonyesha
kuwa idadi ya Watanzania ni 43 milioni
ambapo Wakristo ni asilimia 52,
Waislamu asilimia 32 na dini nyingine ni
asilimia 16 akieleza kuwa takwimu hizo
si sahihi.
Alisema kuwa Bakwata inalaani kitendo
hicho alichosema kinapotosha
wananchi kwa kuwa sensa iliyofanyika
mwaka 2002 kipingele kinachobainisha
dini za Watanzania kiliondolewa.
MGOGORO WA ZANZIBAR
Akizungumzia matukio yauvunjifu wa
amani vilivyotokea visiwani Zanzibara
hivi karibuni Mufti Simba alisema
Bakwata inalaani kitendo inalaani
kitendo hicho ikiamini kwamba
waliofanya vurugu hizo siyo Waislamu
bali ni
wahuni.
Alishauri kuundwa kamati ya pamoja
kati ya Serikali na kikundi cha
Waislamu cha Uamsho ili kuchunguza
waliohusika na vurugu hizo na
waliohusika kuchukuliwa hatua.
Bakwata yataka Dk Ndalichako ajiuzulu
mwananchi.co.tz
June 7, 2012 at 4:59am ? Public

Anzisha uzi wako...
 
mnafurahia kwa sababu yule mama ni mdini balaa, mnajua atakachowafanyia wanafunz wa kiislam

Watafeli kwa vipi tueleze kwani ye ndo msahihishaji mitihani. Mtu ana feli mwenyewe tuache tabia ya kubebana hasa kuelimu. Ukijaza vihiyo nchi itatawaliwa kuvihiyovihiyo na itaenda kivihiyo. Wanafunzi someni shule hatuendi kusoma dini.
 
David Mathayo hapana. Hawezi speed ya JPM. Yule waliposema ni waziri mzigo hawakukosea

Kwa kaskazini ccm ni Aggrey Mwanri peke yake. Very effective and efficient. Angemteua mbunge na waziri.
 
Hamna kitu kinaniuma kama divisheni 5,sitaisahau mpaka naenda kaburini.Mungu awape maisha marefu Dr. Kawambwa na prof. Mchome waone madudu yao waliotufanyia kwenye elimu.Hawa watu ilikuwa badala ya kuongeza ubora kwenye elimu yetu wao walikuwa wanang'ang'ania kubadilisha divisheni.
 
Rais Magu umenipa zawadi ya sikukuu kwa kumteua Dr. JOYCE kuwa waziri wa Elimu. Kati ya teuzi zote hapa umelamba dume. Naamini Elimu yetu sasa itatoka ICU

Amelamba dume au jike? Inamaana huyo mama amegeuka kuwa dume.
 
Atakuwa ametubu dhambi zake, maana ngazi aliachia mwenyewe. Ni heri ametubu kiukweli lakini kama ametubu kiuongo-uongo ataumbuka tu kama alivyoumbuka Lowassa.

Ametubu Kwa Nani? Kwa Magufuli, Shekh Simba, Waislamu, Allah, CCM,Jk Ama Yesu Kristo?. Double Standard!
 
Haya JF mmepewa Waziri mliyemlilia ....btw ni jembe haswa ...hongera dada Joyce
 
Uteuzi wa Maghembe Magufuli kachemka, huyu ni mmoja wa Mawaziri mizigo wa awamu ya 4, na kama alichemka Wizara ya Maji ataiweza Wizara ya Maliasili na Utalii yenye changamoto lukuki?
 
Atakuwa ametubu dhambi zake, maana ngazi aliachia mwenyewe. Ni heri iwe ametubu kiukweli lakini kama ametubu kiuongo-uongo ataumbuka tu kama alivyoumbuka Lowassa.

Hakuna cha kutubu, atubu kwa kosa gani?
 
Majini yanapigana vikumbo yakiongozwa na bidada FaizaFoxy Ndalichako huyoooooo uwaziri kamili! Ole yake majini yafeli tena lile somo!
 
Back
Top Bottom