Rais Magufuli: Aliyetangaza ugonjwa wa ZIKA nchini alikuwa anatumika na ndiyo maana nilipomfukuza, waliomtuma wakamteua kuwa Mkurugenzi

Rais Magufuli: Aliyetangaza ugonjwa wa ZIKA nchini alikuwa anatumika na ndiyo maana nilipomfukuza, waliomtuma wakamteua kuwa Mkurugenzi

Return Of Undertaker

JF-Expert Member
Joined
Jun 12, 2012
Posts
4,572
Reaction score
26,885


Rais Magufuli amenukuliwa akisema haya..

Wakati tunaingia madarakani tuliambiwa Tanzania kuna ugonjwa wa Zika, aliyetangaza na aliyetumiwa kutangaza nikamfukuza kazi (bahati mbaya ni Mgogo); Baada ya kumfukuza yule Mgogo aliyesema Tanzania kuna Zika na waliomtuma wakamteua kuwa Mkurugenzi, mpaka leo miaka karibu mitano hapajawahi kuwa na kesi hata moja ya Zika hapa Tanzania.

Baada ya uzushi wa Zika kupita na kumfukuza kazi aliyesema kuna ugonjwa huo, tukakaa baadaye tukaambiwa kuna Ebola, walijua wakisema tuna Ebola Watalii hawatokuja, tukasema sisi hatuna Ebola wala Mjukuu au hawara yake Ebola, hatujaona Ebola wala nani amekufa kwa Ebola hapa Tanzania.


20200605_213722.jpg
Pia soma
1. Rais atengua uteuzi wa Mkurugenzi NIMR Dkt. Mwele Malecela

2. Dkt. Mwele Malecela aula Umoja wa Mataifa. Kuongoza vituo vya magonjwa Afrika

3. Safari itasonga Kwa msaada wa Mungu: Dr. Mwele Malecela

4. NIMR: Asilimia 45 ya watoto wachanga wakutwa na Virusi vya homa ya ZIKA Tanzania
 
Ndio MUNGU hakumuacha.

Akapewa cheo cha Director general of the national institute for medical research.
Till now and then hakuna mwenye concrete evidence kuwa alikuwa anatumika.

Alitolewa tu ili mtu fulani afaidike kisiasa.
 
“Wakati tunaingia madarakani tuliambiwa Tanzania kuna ugonjwa unaitwa Zika, aliyetangaza na aliyetumiwa kutangaza nikamfukuza kazi, bahati mbaya ni Mgogo, baada ya kumfukuza kazi siku chache akateuliwa na waliomtuma akatangaze kuna Zika akapewa Ukurugenzi”-JPM


“Baada ya kumfukuza yule Mgogo aliyesema Tanzania kuna Zika na waliomtuma wakamteua kuwa Mkurugenzi, mpaka leo miaka karibu mitano hapajawahi kuwa na kesi ya Zika hapa Tanzania”-JPM


“Baada ya uzushi wa Zika kupita na nilipomfukuza kazi aliyesema kuna Zika,tukakaa baadaye tukaambiwa kuna Ebola, walijua wakisema tuna Ebola Watalii hawatokuja,tukasema sisi hatuna Ebola, wala Mjukuu au Hawara yake Ebola, na kweli hatujaona mgonjwa amekufa na Ebola Tanzania”-JPM
 
Kumbe walimu mmeboreshewa maisha na hamsemi kabisa. Vibaya hivyo Jamani.

Mishahara yenu imepanda for 5 years hongereni sana.

Msitufiche hatutawaomba Walimu.

Magufuli alikuwa anatafuta cha kuongea kwa walimu.

Sidhani kama watakuwa wajinga kwa wakati huu.
 
Afu nilicho shangaa kwa mkuu kumtaja mtu kwa Kabila lake eti ‘Mgogo’ yaani namna ya kuwasilisha ya mzee baba kuna muda inakuwa kama ina tweza utu wa mtu, bora angesema hata cheo cha mtu alietolewa ktk hiyo nafasi, kama hataki kutaja jina la mtu husika
 
Kuna kitu zaidi ya hiyo Zika na jinsi maneno yanavyoendelea kutoka watu wazima tushapata majibu wacha tupotezee mbona waliofukuzwa kazi ni wengi anaendelea kutajwa huyo tuu...
Huyu ni mtoto wa Mzee John Samwel Malecella Waziri Mkuu mara mbili wa JMT na Makamu Mwenyekiti CCM Taifa mstaafu. Sio mtu mwepesi kama wanavyomchukulia
 
Kilichomumiza Magufuli ni huyo mama kupewa kazi WHO.

Alitaka akimfukuza ateseke
Of course kama mtu anaweza kutumika atangazie ulimwengu kuwa tanzania kuna epidemic wakati hata yeye mwenyewe haamini uwepo wake lazima imuume binadamu yeyote mtu kama huyo akiendelea kuaminiwa na yeyote popote kwa sababu hatujui huko mbeleni atafanya nini kwa faida ya watakaotaka kumtumia kwa maslahi yao
 
Back
Top Bottom